Pep Guardiola na Mapinduzi ya Soka

Aaron Arsenal

JF-Expert Member
Jul 24, 2014
24,504
28,691
Kwasasa mpira umebadilika sana tofauti na enzi za kina Ferguson, Arsene Wenger n.k miaka ya 2000s.

Moja ya watu walioleta mapinduzi ya soka ni Pep Guardiolaz, huyu ana wanafunzi wake wengi sana aliokaa nao na wanaoiga uchezaji wake, kina Xavi Hernandez, Mikel Arteta, Erik Ten hag, n.k

Moja ya mapinduzi aliyoleta ni progressive football kuanzia kwa GK, Overload au Outnumbered kila eneo

Leo nitazungumzia Overload, hakuna kitu nakipenda ninapoangalia mpira na kufurahia ninapoona OVERLOAD, yaani hapa kila eneo unakuta umezidiwa, hiiinakuwaje? Fatana nami uone.

Timu nyingi huwa tunaona zinaingia na mifumo kama 4-3-3,4-4-2,4-2-3-1,3-4-3, n.k.

Hii kwa kawaida ni mifumo inatumika kuzuia, au timu ikishaingia uwanjani ikazuia kwa mfumo mwingine na kushambulia kwa mfumo mwingine.

Mifumo ya kushambulia imekuwa ikitumika kama 2-3-5, 3-1-6, 2-3-3-2, n.k.

Sasa twende pamoja ukaone jinsi Overload, hasa Pep Guardiola anavyoitumia pia makocha Kama Xavi, Arteta ,Erik Tan hag , Graham Potter jinsi wanavyocheza.

Ikiwa timu pinzani watacheza na mabeki wa 5, Guardiola atacheza na wachezaji 6 mbele.

Ikiwa timu pinzani itacheza na wachezaji wawili kwenye safu yao ya mbele(e.g 4-4-2,4-2-2-2,3-5-2,n.k) basi Guardiola utamuona atacheza na walinzi 3 (hivyo 3-1-6).

Ikiwa timu hiyo itacheza 5-4-1 (hivyo mchezaji mmoja katika safu yake ya mbele) Guardiola atacheza 2-2-6.

Man City walipocheza na Bournemouth , Bournemouth walilinda kwa shepu ya 5-4-1.

Manchester City walishambulia kwa uchezaji katika umbo la 2-2-6.

DM wa 2 ili kuwazidi idadi ya CF na 6 kwenye mstari wa mbele ili kuwazidi mabeki wao wa 5.

Angalia hapa,

IMG_20221010_203753.jpg

IMG_20221010_203750.jpg


CMs na Wingers/Full Backs kazi yao ni kuwezesha OVERLOAD katika maeneo mbalimbali.

Mfano mwingine huu hapa;

Nott’m Forest ililinda kwa 5-3-2 ilipocheza na Man City, Guardiola akaseti timu yake katika mfumo wa 3-1-6. Umbo hili linafanana sana na
3-Diamond-3.
IMG_20221010_204800.jpg

IMG_20221010_204752.jpg

Unaweza kuona jinsi wachezaji wa City wa kati wanavyoweza kuwazidi wachezaji wa Forest wa 5 na viungo wao wa 3.

CM ya kati (10) anakuwa huru ku OVERLOAD na kufanya yake.

Twende mfano Mwingine;
Mech ya Manchester City vs Man United.

Manchester Utd walijilinda kwa 4-2-3-1 lakini winga mmoja au AM ndio walitumika kupress CBs za City.

City walicheza 2-3-5 wakiwa na mabeki wa pembeni ili kuzuia mashambulizi ya kukabiliana ya Man U, lakini kama umegundua cha kwanza kama mpinzani atakubonyeza na mchezaji mmoja, basi unawekewa mabeki wawili ili waweze kufanya buildup watoke nyuma (hapa ndipo Kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na GK mwenye uwezo mguuni)

Shepu hii ya 2-3-5 ilimpa nafasi katika kiungo wa chini siku hiyo ambaye alikuwa Gundogan (DM) kupeleka mipira kwa Haaland pia KDB na B.Silva kushambulia au kutumia half spaces.

IMG_20221010_210551.jpg

IMG_20221010_210545.jpg


OVERLOAD EVERYWHERE

Mechi ya Arsenal vs Spurs ni mfano wangu wa mwisho.

Conte aliingia na 3-4-3, lakini akawa anacheza kwa 5-4-1.

Arteta akaiseti timu yake kwenye shepu ya 2-3-5, kwanza kuweza kutoka nyuma kwa buildup ya 2v1, halafu kwenye Midfield anaongezeka Zinchenko na kuungana na Xhaka Partey na kufanya 3v2, sababu hawa wingbacks wanatolewa au kuondolewa na winga mbili za pembeni(Saka & Martinell) ambazo watacheza kwa kutanua uwanja hivo wingbacks Emerson Loyal na Perisic inabidi wawafate, na kuacha viungo wao wawili dhidi ya watatu wa Arsenal.

OVERLOAD EVERYWHERE

images (1).jpeg


Note: HII OVERLOAD INAHITAJI WACHEZAJI MAALUM SIYO KILA MCHEZAJI ANAWEZA KUTEKELEZA MAJUKUMU HAYO.
 
Tupe uchambuz wa carlo anceloti,
Anabadika badilika mno yule mzee,

Timu haichezi soka la kuvutia Sana machoni, ila dkk 90 zikiisha lazima achukue point 3 muhimu
 
Guardiola ni mzuri team yake ikiwa na mpira ila akiwa hana mpira ni team mbovu tu ndo maana kwenye UEFA champions league wanampasua yaye kila mechi anashambulia mpaka fainali hana game plan yeye ni muumini wa attacking football iwe ugeni iwe nyumbani iwe UEFA champions league iwe premier league katika makocha ambao ni average wanapewa tu sifa ni Guardiola kama mwanaume kweli uchukue UEFA champions league sio kuwaonea Bournemouth na Brighton ndo maana Bayern's Munich walimtumua wakaana hamna kocha hapa kila mechi anafungua turbo
 
Ila kwa aina Ya Timu anazofundishaga Guardiola ni za Viwango vya juu sana (Top 5)

Ili ubora na uwezo wake uthibitike alipaswa Kupewa Timu kama Everton, Brighton au Watford zenye Budget ya kawaida kabisa ndipo ubora wake utaonekana.

Ile Barcelona ya akina Xavi, Iniesta Messi, katika ubora wa ujana wao hata Ungemuweka Mwijaku kuwa Head Coach lazima Wangebeba vikombe.

Hii Man City ya sasa iko kwenye Top 3 ya Timu zilizotumia Fedha nyingi zaidi kusajili wachezaji wakubwa.

Natamani Siku moja nimuone Guardiola akifundisha timu Kama Borrusia Dortmund, Monaco au AS Roma nione...
 
Ila kwa aina Ya Timu anazofundishaga Guardiola ni za Viwango vya juu sana (Top 5)

Ili ubora na uwezo wake uthibitike alipaswa Kupewa Timu kama Everton, Brighton au Watford zenye Budget ya kawaida kabisa ndipo ubora wake utaonekana.

Ile Barcelona ya akina Xavi, Iniesta Messi, katika ubora wa ujana wao hata Ungemuweka Mwijaku kuwa Head Coach lazima Wangebeba vikombe.

Hii Man City ya sasa iko kwenye Top 3 ya Timu zilizotumia Fedha nyingi zaidi kusajili wachezaji wakubwa.

Natamani Siku moja nimuone Guardiola akifundisha timu Kama Borrusia Dortmund, Monaco au AS Roma nione...
na Man u ni ya kwanza kutumia hela nyingi
 
Mpira anaofundisha pep guardiola, artet,...
Unahitaji players maalum. Sio kila mchezaji

Hawa wachezaji, control ya mpira ni chumba na sebule. Wao wanajua mbio na kupiga majaro
Ni ngumu sana kupiga mpira wa technically na skills

Pep anakukamata kwenye possession kwanza
Hapa ndio anaficha madhaifu yake
Ndio maana anapendelea sana midfielders ili awe na mpira muda wote

Kwenye mpira kuna kitu kinaitea patience
Upo na mpira lakini unasubiri right time to make attacks, ata ikikuchukua dakika 5 it's okey
Hii 90% ndio pep anachowashinda wengi

Liverpool akipata mpira anataka akupress, akipoteza anaanza kukaba
Man city yeye atakutafuta mdogo mdogo, anaweza fika hadi 18 ya mpizan then akarudi nyuma kuwavuta wachezaji ili aanze tena pressing anaweza kufanya hvyo ata mara 4
Hapo mpinzani ataona afunguke tu atafute mpira au atoke nyuma
Ndio pep na yeye anafanya runs zake

Na kitu kikubwa kwenye ball recovery ndio 100% yupo njema sana sana
City, barca ile 2012 ikipoteza mpira within a minute unajikuta mpira wanao wao
Wanakuja kukaba watatu watatu, kama nyuki
OVERLOAD kama ilivyoelezewa hapo juu


Ili uucheze huo mpira unahitaji watu sahihi sana,
Sharp, quickly, wanaonyumbulika, na ball brain
Ndio maana wachezaji weusi wanamuona pep mbaguzi
 
Mpira anaofundisha pep guardiola, artet,...
Unahitaji players maalum. Sio kila mchezaji

Hawa wachezaji, control ya mpira ni chumba na sebule. Wao wanajua mbio na kupiga majaro
Ni ngumu sana kupiga mpira wa technically na skills

Pep anakukamata kwenye possession kwanza
Hapa ndio anaficha madhaifu yake
Ndio maana anapendelea sana midfielders ili awe na mpira muda wote

Kwenye mpira kuna kitu kinaitea patience
Upo na mpira lakini unasubiri right time to make attacks, ata ikikuchukua dakika 5 it's okey
Hii 90% ndio pep anachowashinda wengi

Liverpool akipata mpira anataka akupress, akipoteza anaanza kukaba
Man city yeye atakutafuta mdogo mdogo, anaweza fika hadi 18 ya mpizan then akarudi nyuma kuwavuta wachezaji ili aanze tena pressing anaweza kufanya hvyo ata mara 4
Hapo mpinzani ataona afunguke tu atafute mpira au atoke nyuma
Ndio pep na yeye anafanya runs zake

Na kitu kikubwa kwenye ball recovery ndio 100% yupo njema sana sana
City, barca ile 2012 ikipoteza mpira within a minute unajikuta mpira wanao wao
Wanakuja kukaba watatu watatu, kama nyuki
OVERLOAD kama ilivyoelezewa hapo juu


Ili uucheze huo mpira unahitaji watu sahihi sana,
Sharp, quickly, wanaonyumbulika, na ball brain
Ndio maana wachezaji weusi wanamuona pep mbaguzi
Wewe jamaa unajua Sana ,napendaga Sana kusoma mawazo yako
 
Ila kwa aina Ya Timu anazofundishaga Guardiola ni za Viwango vya juu sana (Top 5)

Ili ubora na uwezo wake uthibitike alipaswa Kupewa Timu kama Everton, Brighton au Watford zenye Budget ya kawaida kabisa ndipo ubora wake utaonekana.

Ile Barcelona ya akina Xavi, Iniesta Messi, katika ubora wa ujana wao hata Ungemuweka Mwijaku kuwa Head Coach lazima Wangebeba vikombe.

Hii Man City ya sasa iko kwenye Top 3 ya Timu zilizotumia Fedha nyingi zaidi kusajili wachezaji wakubwa.

Natamani Siku moja nimuone Guardiola akifundisha timu Kama Borrusia Dortmund, Monaco au AS Roma nione...
Mzee baba hizo timu ulizotaja anaweza kuzifundisha vzr tu, ila wampe wachezaji anaowataka yeye , Sio wavunja kuni
 
Ila kwa aina Ya Timu anazofundishaga Guardiola ni za Viwango vya juu sana (Top 5)

Ili ubora na uwezo wake uthibitike alipaswa Kupewa Timu kama Everton, Brighton au Watford zenye Budget ya kawaida kabisa ndipo ubora wake utaonekana.

Ile Barcelona ya akina Xavi, Iniesta Messi, katika ubora wa ujana wao hata Ungemuweka Mwijaku kuwa Head Coach lazima Wangebeba vikombe.

Hii Man City ya sasa iko kwenye Top 3 ya Timu zilizotumia Fedha nyingi zaidi kusajili wachezaji wakubwa.

Natamani Siku moja nimuone Guardiola akifundisha timu Kama Borrusia Dortmund, Monaco au AS Roma nione...
Yaan unataka Pep awatumie kina Phil Jones na wavunja kuni wengine ?

Kuhusu kutumia pesa mnamuonea ,dirisha hili man u ,Chelsea, forest wamemwaga pesa kuliko Yeye ,Cha ajabu anawaacha mbali kimbinu
 
Back
Top Bottom