Penzi la Chuo Kikuu

Penzi la Chuo Kikuu

PENZI LA CHUO KIKUU 03

Mtunzi; Michaelray.

"Dapshan!!"
Mama alihamaki kisha simu ikakatika.
Mama hakuamini alichokuwa amekisikia kwenye simu. Alihisi kama anaota. Alimuita Baba aliyekuwa nje anafunga ndama.
"Baba Michael! Mume Wang"
Mama alimuita Baba akiwa anatoka nje na simu.
"Baba Micheal, Michael hajafa"
"Unasema!"
"Michael hajafa"
"Unaota mke Wang"
"Sioti wala sipo ndotoni"
"Na lile kaburi ni la nani?"
Baba alimuuliza mama akilinyooshea kaburi ambalo nilidhikwa Mimi miezi miwili iliyopita. Mama aliliangalia kaburi na kuishiwa na maneno. Kaburi ndilo lililokuwa ushahidi wa kifo cha Michaelray.
"Ina maana niliongea na nani sasa?"
"Kwani uliongea na nani?, unajua mke wangu utachanganyikiwa. Michael alishakufa na kijiji kizima kinajua. Sasa wee umeongea na nani?"
Baba aliongea akiwa amemaliza kuwafunga ndama kamba.
Simu ya mama iliita tena.
"Michael anapiga! Ee shika uongee nae si ulikuwa unabisha!"
Mama aliongea akimkabidhi Baba simu. Baba aliipokea na kuingalia namba iliyokuwa inaita na kukuta haina jina kuonyesha haijahifadhiwa kwenye Simu
 
Back
Top Bottom