Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Angekuwa na kiti mbinguni pembeni mwa Mungu ingekuwa sawa, Roma kama Dar tu sema yenyewe imejengwa kwa ustadi


Kama wewe siyo Mkatoliki hapo uko sawa, lkn kwa Wakatoliki ana nafasi ya kipekee kwa Mungu kwani kati ya Binadamu bilioni 1.23 Mungu kamteua yeye, huyo siyo upekee?
 
Mwanahabari Huru

Askofu Pengo unafiki sio sehemu yetu wakatoliki, sikutaka kuandika chochote kuhusiana na wewe, mimi nimebatizwa katika RC nimekuwa muumini mkubwa, nimesoma shule ya Upadri St Mary's Seminary, ninaijua Rc.

Nimesikitishwa sana na kauli zako za kipuuzi, zilizo jaa unafiki, tumekusikia sana ukijipambanua kuwa wewe si muumini wa mabadiliko, tuambie upande wako ni UPI.

Askofu wangu Pengo umemjibu Askofu Niwemugizi alie jitokeza hadhalani na kusema watanzania wanataka katiba mpya, umefufuka ulikotoka na kumshambulia Askofu kuwa katiba au maneno ya Askofu sio msimamo wa RC lakini hakusema kuwa ni msimamo wa RC. Lakini unajua Askofu Niwemugizi si msemaji wa Rc, maana yake alisema kama Mawazo yake kikatiba, na wewe unamjua msemaji wa RC ulitaka kutafuta uhalali wa kujibu mashambulizi la watawala, of target.

Naona umetoka kwa kasi sana kujibu shambulizi hill!,! Lakini hutoki hadhalani kuonya matukio ya kuuwawa kwa watanzania na kutupwa kwenye maji wakiwa wamefungwa mikono Nyuma, wanaopigwa Risasi kama kina tundu Lissu, kuonya viongozi wanao toa maneno ya kibaguzi na kikabila, huwezi kuonya kufokea au kushauri, kazi yako imekuwa ni kujibu mashambulizi kwa wanao ikosoa serikali,

Au unavyeti feki? Unamiliki Mali zisizo halali? Kiongozi wa kiroho unashindwa kujua nini wajibu wako? Sio mala ya kwanza kupingwa na maaskofu wenzio akiwepo Gwajima na kupelekana mahakamani ambapo Askofu Gwajima alikushinda kesi.

Viongozi wa dini simamieni haki na sio unafiki kujipendekeza kama mnataka ubunge, au teuzi za kina mama Lwakatale sawa, Hata mkitaka usemaji wa Ccm nafasi za kina polepole.

Swali la Kizushi: WATU WASIOJULIKANA WANATOKEA RWANDA TUMUOMBE TUNDU LISSU
Unataka alihamishie kanisa lote ufipa?
 
Nashauri uongozi wa jamiiforum ulete mfumo mpya kwa wanaojiunga na huu mtandao.....angalau kuwe na vi IQ test vitakavyochuja wenye below average score
 
Nashauri uongozi wa jamiiforum ulete mfumo mpya kwa wanaojiunga na huu mtandao.....angalau kuwe na vi IQ test vitakavyochuja wenye below average score
Naomba kupinga hii hoja Mkuu, tutaondokewa na celebrities humu na hakika patapooza!
 
Huwa hampendi kuambiwa ukweli.....
Mbna hamkumkosoa GWAJIMA kipindi kile yupo upande wenu....
Askofu PENGO yupo sahihi maana kaona mtu sahihi
Kama ambavyo Mbowe anavyosifia mazuri ya MAGUFULI....mbna hausemi ana kiharibu chadema?
1.Pole maana ww ndio huujui ukweli,Pengo anamsema askofu mwenzie kwamba siyo msemaji wa kanisa na kwamba yale ni mawazo yake binafsi na yeye anasahau kwa wakati huo huo kwamba pale alipo siyo msemaji wa kanisa na wala hajatumwa na kanisa,alipaswa kutohukumu maana makosa anayo muhukumu mwenzie naye yy ndio hayo kayarudia, na kwamba alipaswa kusema wazi kuwa kile anachokisema yy pia ni mawazo yake binafsi kwani bado hana hadhi ya kuwa msemaji wa kanisa katoliki tanzania.

2.Pengo anatumia vibaya ujinga/kutokujua kwa watanzania walio wengi ya kwamba yeye siyo mkuu wa kanisa katoliki tanzania na wala hana nafasi yoyote katika kanisa la tanzania zaidi ya kanisa katoliki jimbo la dar es salaam,yeye anapata sifa ya kuwa msemaji wa jimbo katoliki dar es salaam pekee ikibidi na siyo tanzania sawa na Niwemugizi kwa jimbo lake.

Na pia yeye siyo muwakilishi wa papa tanzania,papa anawakilishwa na balozi wake ambaye hutumwa kwa vipindi tofauti.
Hivyo asitufanye wajinga kutaka kuharibu kanisa kwa mitazamo yake akitaka ndio iwe mitazamo ya kanisa zima la tanzania, bado hajafikia hadhi hiyo.

Mkuu wa kanisa katoliki tanzania ni raisi wa balaza la maaskofu (TEC) huyo pekee ndio mwenye hadhi ya kuzungumza kwa niaba ya kanisa la tanzania na kauli yake ikawa kauli ya kanisa au ya maaskofu.

Hivyo kafanya makosa kumshambulia askofu mwenziekwamba kafanya makosa wakati akijua yeye pia anafanya makosa hayo hayo na hiyo ni hulka yenye unafiki,labda atuambie anatetea maslahi ya kundi fulani na si ya kanisa katoliki.
 
Kwa Wakatoliki Kardinali ni mtumishi wa Mungu, anateuliwa na Mungu baada ya kushukiwa na roho Mtakatifu hivyo sauti yake ni Sauti ya Mungu kwa Wakatoliki!

MKUU NAKUHESHIMU ILA HAPO UMEKOSEA,
PADRI AU ASKOFU HUWA SAUTI YA YESU, MUNGU MWANA AWAPO MBELE YA ALUTALE TU HUKO KWENGINE NI YEYE NA NAFSI YAKE.

SORRY KWA KUKUKOSO NDIO IMANI KATOLIKI
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Kwa cheo chake HIS EMINENCE Polycarp Cardinal Pengo (prospective Holy Father or Pope) ni raia wa VATICAN Kwa sheria za Tanzania anapaswa kuukana uraia wa Tanzania (kama bado hajaukana) mpaka Leo.
 
Ni swala la mtazamo tu, kwako ni kauli ya ukakasi kwa wengine ni kauli ya Mungu kwani Kardinali ni mtumishi wa Mungu ambaye ameteuliwa na Mungu kuwa Kardinali wa Kanisa Katoliki hivyo sauti yake ni sauti ya Mungu kwa wafuasi wa Kanisa Katoliki!
Mungu hawezi kufanya uteuzi wa kitumbafu hivo.
 
Mwanahabari Huru

Askofu Pengo unafiki sio sehemu yetu wakatoliki, sikutaka kuandika chochote kuhusiana na wewe, mimi nimebatizwa katika RC nimekuwa muumini mkubwa, nimesoma shule ya Upadri St Mary's Seminary, ninaijua Rc.

Nimesikitishwa sana na kauli zako za kipuuzi, zilizo jaa unafiki, tumekusikia sana ukijipambanua kuwa wewe si muumini wa mabadiliko, tuambie upande wako ni UPI.

Askofu wangu Pengo umemjibu Askofu Niwemugizi alie jitokeza hadhalani na kusema watanzania wanataka katiba mpya, umefufuka ulikotoka na kumshambulia Askofu kuwa katiba au maneno ya Askofu sio msimamo wa RC lakini hakusema kuwa ni msimamo wa RC. Lakini unajua Askofu Niwemugizi si msemaji wa Rc, maana yake alisema kama Mawazo yake kikatiba, na wewe unamjua msemaji wa RC ulitaka kutafuta uhalali wa kujibu mashambulizi la watawala, of target.

Naona umetoka kwa kasi sana kujibu shambulizi hill!,! Lakini hutoki hadhalani kuonya matukio ya kuuwawa kwa watanzania na kutupwa kwenye maji wakiwa wamefungwa mikono Nyuma, wanaopigwa Risasi kama kina tundu Lissu, kuonya viongozi wanao toa maneno ya kibaguzi na kikabila, huwezi kuonya kufokea au kushauri, kazi yako imekuwa ni kujibu mashambulizi kwa wanao ikosoa serikali,

Au unavyeti feki? Unamiliki Mali zisizo halali? Kiongozi wa kiroho unashindwa kujua nini wajibu wako? Sio mala ya kwanza kupingwa na maaskofu wenzio akiwepo Gwajima na kupelekana mahakamani ambapo Askofu Gwajima alikushinda kesi.

Viongozi wa dini simamieni haki na sio unafiki kujipendekeza kama mnataka ubunge, au teuzi za kina mama Lwakatale sawa, Hata mkitaka usemaji wa Ccm nafasi za kina polepole.

Swali la Kizushi: WATU WASIOJULIKANA WANATOKEA RWANDA TUMUOMBE TUNDU LISSU

Mkuu umenikumbusha TanzaGiza.Alikuwa anamalizia swali la kizushi Bashite anampa nini Mkulu.Ila nimependa ulivyojenga hoja Hekoo kwako [HASHTAG]#TzYaViwonderHii[/HASHTAG]
 
Siyo swala la ujinga au werevu ni swala la power, kuna Wakatoliki wengi Tanzania ambao hawawezi kuhoji ushauri wa Kardinali wao, kwao ni mtumishi wa Mungu na akisemacho kina baraka za Mungu, hivyo ndivyo ilivyo!

Waumini sawa nafasi ipo ila ndogo sana ya kuhiji, ila baraza la maaskof tanzania wanaweza na wamekuwa wakihoji na huwa wanaoji, kindly review track record, hatushindani mkuu twaelimishana.

kwa kiasi gani wanoji? ndhani kadri waonavyo sawa kulinda heshima ya kanisa na imani ya kanisa

hawawezi kunjana ndo uone wanahoji

kumbuka hayo kasema pengo kwa utashi wake akiwa chumbani kwake
 
Mungu hawezi kufanya uteuzi wa kitumbafu hivo.


Sawa lkn kumbuka Binadamu Bilioni 1.3 Duniani wanaamini hivyo ambayo ni zaidi ya18% ya Binadamu wote, kwa miaka karibia 2000, hivyo sidhani kama wewe unaweza kuwa more intelligent kiasi hicho, kumbuka Western civilization yote ambayo ndiyo Civilization inayotawala Dunia hii leo hii imetokana na Kanisa Katoliki, kuanzia mfumo wa Elimu ambao unatumika Duniani kote, hata mimi na wewe tunaweza kuwasiliana sasa hivi na kubishana bila ya western civilization labda isingewezekana kuwasiliana kama tunavyowasiliana sasa hivi, mfumo wa Kiuchumi ambao ni Capitalistic economic system yote ni western Civilization ambao chimbuko lake ni Kanisa Katoliki, Sheria na mifumo ya Utawala Duniani imetokana na Western Civilization ambao chimbuko lake ni Kanisa Katoliki hivyo kabla haujaiita Upumbavu chukua dakika kadha ufikirie wewe au Dini uliyo nayo imeleta ahueni gani kwa maisha ya binadamu kiasi cha kukupa haki ya kuuita Ukatoliki upumbavu!
 
Back
Top Bottom