Pengo aonya Mapadri kuji husisha na siasa

Pengo aonya Mapadri kuji husisha na siasa

kanda2

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2007
Posts
1,319
Reaction score
76

Naileta hii unedited......

Pengo aonya uhusiano wa mapadri na wanasiasa
Imeandikwa na Martha Mtangoo, Dodoma; Tarehe: 22nd August 2010 @ 22:30 Imesomwa na watu: 16; Jumla ya maoni: 0






MAPADRI nchini wameaswa kutodanganywa na wanasiasa wenye lengo la kujipatia mali.

Mwito huo ulitolewa jana mjini Dodoma na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo wakati wa kilele cha maadhimisho ya kongamano la mwaka wa upadri.

Askofu Mkuu huyo alisema Tanzania ina vyama vingi vya siasa na kuwataka mapadri wasitumie vyama hivyo vya siasa katika kuwasaidia maskini kwani ni hatari, ila wahubiri habari njema za ukombozi wa Yesu kristo.

Alibainisha kuwa endapo padri yeyote hapa nchini atajiunga na wanasiasa atakuwa hana akili.

Alifafanua kuwa ni vyema mapadri wasidanganyike wala kurubuniwa na wanasiasa kama ilivyokuwa kwa mapadri wa nchini Rwanda ambao walisababisha maafa mwaka 1994 na hivyo kuishia gerezani.

Alisema baadhi ya mapadri hao wa Rwanda walikubali kuburuzwa na wanasiasa hao kwa ajili ya kutaka kujipatia mali na hivyo kusababisha maafa kutokana na ujinga wao.

Alifafanua kuwa ni dhahiri kuwa mapadri hao chimbuko lao halikuwa la upadri kutokana na wao kukubali kudanganywa na wanasiasa hao wapumbavu hali ambayo imesababisha mapadri wote kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa ajili ya vitendo vyao viovu.


Naomba kuwasilisha



 
Haya ndo mambo unayo yapenda sana! umesikika ustaadhi....Ngoja niripoti kwa Maxence
 
Pengo aonya uhusiano wa mapadri na wanasiasa
Imeandikwa na Martha Mtangoo, Dodoma; Tarehe: 22nd August 2010 @ 22:30 Imesomwa na watu: 39; Jumla ya maoni: 0


Habari Zaidi:
# Mgombea CCM awapongeza wapinzani wake kura za maoni
# CUF yatamba kudumisha Muungano
# JK ngangari, afunika Mwanza
# Pengo aonya uhusiano wa mapadri na wanasiasa
# Majimarefu atatafsiriwa Kiingereza bungeni
# Kondakta akutwa amekufa ndani ya daladala
# Mchungaji kizimbani kwa kumtorosha ‘mbakaji’
# Mwenyekiti wa Chadema ajiuzulu kwa ‘fitna’
# Mamia wamzika aliyewahi kuwa mbunge
# 20 walazwa hospitalini kwa kuharisha
# Chadema wakata rufaa Morogoro
# ‘Vijana sikilizeni sera za kila chama’
# UV-Bakwata, CUF wampa pole Kikwete
# Kikwete augua, wananchi walia
# CCM yaanza kampeni na wabunge 13
# Mabalozi wa heshima kukaguliwa
# CCM yaanza kampeni kwa kishindo
# Aliyetangazwa kugombea aikana Chadema
# CCM,we acha tu
# Mke wa Slaa, Shibuda kusaka ubunge Chadema

Habari zinazosomwa zaidi:
# Balaa lingine kwa Chenge
# Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
# Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
# ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa
# Vatican yamvua jimbo Askofu
# Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
# Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
# Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
# Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
# JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
MAPADRI nchini wameaswa kutodanganywa na wanasiasa wenye lengo la kujipatia mali.

Mwito huo ulitolewa jana mjini Dodoma na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo wakati wa kilele cha maadhimisho ya kongamano la mwaka wa upadri.

Askofu Mkuu huyo alisema Tanzania ina vyama vingi vya siasa na kuwataka mapadri wasitumie vyama hivyo vya siasa katika kuwasaidia maskini kwani ni hatari, ila wahubiri habari njema za ukombozi wa Yesu kristo.

Alibainisha kuwa endapo padri yeyote hapa nchini atajiunga na wanasiasa atakuwa hana akili.

Alifafanua kuwa ni vyema mapadri wasidanganyike wala kurubuniwa na wanasiasa kama ilivyokuwa kwa mapadri wa nchini Rwanda ambao walisababisha maafa mwaka 1994 na hivyo kuishia gerezani.

Alisema baadhi ya mapadri hao wa Rwanda walikubali kuburuzwa na wanasiasa hao kwa ajili ya kutaka kujipatia mali na hivyo kusababisha maafa kutokana na ujinga wao.

Alifafanua kuwa ni dhahiri kuwa mapadri hao chimbuko lao halikuwa la upadri kutokana na wao kukubali kudanganywa na wanasiasa hao wapumbavu hali ambayo imesababisha mapadri wote kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa ajili ya vitendo vyao viovu.


Source: Habari Leo

Hiyo ni habari kamili sasa kimsingi ni kwamba kama viongozi wa dini wakijihusisha na kukitetea chama fulani ni hatari kwa nchi na mustakbali wa nchi nzima. Kwani hata kama chama kitakuwa na itikadi nzuri ya chama kitaonekana ni chama cha kidini tu. Ni vema maaskofu na masheikh wakae mbali na siasa kwani watahatarisha amani ya nchi
 
Je kusema hivyo anatoa maana gani kwa dr.slaa ambaye ni padri kitaaluma aliyejiunga na siasa?......?
 
Kanda2 anajulikana kuna kitu hapo ameficha angalia alimobold! Mdini sana huyoooo mugope

Basi wacha nijitoe katika hii thread nilidhani tunaargue kwa hoja kumbe kuna udini ndani yake mijadala hiyo nimewaachia malaria sugu na wenzie nilikuwapo.
 
Je kusema hivyo anatoa maana gani kwa dr.slaa ambaye ni padri kitaaluma aliyejiunga na siasa?......?

Kwani Dr.Slaa bado anafanya kazi ya kiroho? Tofautisha baina ya kiongozi wa dini na kiongozi wa serikali hapo unadeal na vitu viwili tofauti.
 
Kwani Dr.Slaa bado anafanya kazi ya kiroho? Tofautisha baina ya kiongozi wa dini na kiongozi wa serikali hapo unadeal na vitu viwili tofauti.
Dr. Slaa alishatoka huko. Kwake ni sawa kujishughulisha na siasa. Kardinali alikuwa akionya wale wanaotoa bado huduma ya kipadre kwamba wasijihusishe na siasa kwani kwa kufanya hivyo wataweza kuwagawa waamini ambao ni wanachama wa vyama mbalimbali. Wao ni wachungaji wa wote kuegemea chama fulani kutaleta mgawanyiko Kanisani kwa misingi ya itikadi. Kumbe wao wanatakiwa kuwa neutral.
 
Naileta hii unedited......

Pengo aonya uhusiano wa mapadri na wanasiasa
Imeandikwa na Martha Mtangoo, Dodoma; Tarehe: 22nd August 2010 @ 22:30 Imesomwa na watu: 16; Jumla ya maoni: 0






MAPADRI nchini wameaswa kutodanganywa na wanasiasa wenye lengo la kujipatia mali.

Mwito huo ulitolewa jana mjini Dodoma na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo wakati wa kilele cha maadhimisho ya kongamano la mwaka wa upadri.

Askofu Mkuu huyo alisema Tanzania ina vyama vingi vya siasa na kuwataka mapadri wasitumie vyama hivyo vya siasa katika kuwasaidia maskini kwani ni hatari, ila wahubiri habari njema za ukombozi wa Yesu kristo.

Alibainisha kuwa endapo padri yeyote hapa nchini atajiunga na wanasiasa atakuwa hana akili.

Alifafanua kuwa ni vyema mapadri wasidanganyike wala kurubuniwa na wanasiasa kama ilivyokuwa kwa mapadri wa nchini Rwanda ambao walisababisha maafa mwaka 1994 na hivyo kuishia gerezani.

Alisema baadhi ya mapadri hao wa Rwanda walikubali kuburuzwa na wanasiasa hao kwa ajili ya kutaka kujipatia mali na hivyo kusababisha maafa kutokana na ujinga wao.

Alifafanua kuwa ni dhahiri kuwa mapadri hao chimbuko lao halikuwa la upadri kutokana na wao kukubali kudanganywa na wanasiasa hao wapumbavu hali ambayo imesababisha mapadri wote kudharauliwa na kuonekana hawana maana kwa ajili ya vitendo vyao viovu.


Naomba kuwasilisha

Kinachoongelewa kwenye hayo maandishi ni kutodanganyika. Ni kwa wahusika kuwakabili wanasiasa wadanganyifu ili waache kuwaonea watu. Sioni neno lolote linalosema wahusika wasiwarekebishe wanasiasa au wasibadili siasa za udanganyifu na kuzifanya ziwe siasa za haki na zenye ukweli.
 
Haya Wagalatia munaanza tena yaani Muadhama anamaana ya Mungu mpe Mungu na ya Kaisari mpe.........au kwa tafsiri yake ni kuwa DINI NA SIASA ISICHANGANYWE au nimemuelewa vibaya? kama ndiyo hivyo basi kwa namna moja nadhani yuko sawa lakini kwa Waislamu itakuwa kinyume kwani kutochanganya DINI na SIASA ni HARAMU! na ukiangalia historia Mashehe hawajawahi kushiriki au kupanga mauwaji ya kimbari huko Rwanda na sehemu zingine badala yake Misikiti ilikuwa ndio kimbilio la wahanga wa mauwaji ama ni Watusi au Wahutu wa siasa baridi!

Hivyo naam namuunga mkono na miguu yote muhashamu kwa kuwaonya Mapadre wasijiingize ktk siasa kwani huenda wakashindwa kujidhibiti na kuamua kuleta machafuko nchini na mungu aepushe mbali hayo yasijetokea kwani utakuwa msiba mkubwa! hivyo namshauri Padre Wilberd Slaa ajitoe kugombea urais kwani mtu hajiuzulu Upadre lakini Siasa anaweza kuwacha!
 
Mapadiri sasa wameshituka mtu wao hana nafasi ya kupewa Urais katika mazingira yeyote yale, hali hiyo imewafanya kujigeuza vinyoga na kurejesha majeshi huku wakionesha kufurahia uwepo wa JK kuendelea kuliongoza taifa,ni matokeo ya hizi siku mbili zidi wabunge wa Chadema yamewafanya wabadili nyaraka zao kama wangendelea na hiyo miwaraka yao wangeumbuka vibaya sana baada ya Uchaguzi ,nafikiri na hiyo halaiki ya jana imezidi kuwakatisha tamaa .Yaliyotokea Ruwanda hayana tafauti na Uandikaji WARAKA.
:mad2:





Sicily
 
Mapadiri sasa wameshituka mtu wao hana nafasi ya kupewa Urais katika mazingira yeyote yale, hali hiyo imewafanya kujigeuza vinyoga na kurejesha majeshi na kufurahia uwepo wa JK kuendelea kuliongoza taifa ,matokeo ya hizi siku mbili zidi wabunge wa Chadema yamewafanya wabadili nyaraka zao kama wangendelea na hiyo miwaraka yao wangeumbuka vibaya sana baada ya Uchaguzi ,nafikiri na hiyo halaiki ya jana imezidi kuwakatisha tamaa .Yaliyotokea Ruwanda hayana tafauti na Uandikaji WARAKA.
:mad2:


Sicily

Bange na swaumu ni balaa lazima upumbike!
 
Haya Wagalatia munaanza tena yaani Muadhama anamaana ya Mungu mpe Mungu na ya Kaisari mpe.........au kwa tafsiri yake ni kuwa DINI NA SIASA ISICHANGANYWE au nimemuelewa vibaya? kama ndiyo hivyo basi kwa namna moja nadhani yuko sawa lakini kwa Waislamu itakuwa kinyume kwani kutochanganya DINI na SIASA ni HARAMU! na ukiangalia historia Mashehe hawajawahi kushiriki au kupanga mauwaji ya kimbari huko Rwanda na sehemu zingine badala yake Misikiti ilikuwa ndio kimbilio la wahanga wa mauwaji ama ni Watusi au Wahutu wa siasa baridi!

Hivyo naam namuunga mkono na miguu yote muhashamu kwa kuwaonya Mapadre wasijiingize ktk siasa kwani huenda wakashindwa kujidhibiti na kuamua kuleta machafuko nchini na mungu aepushe mbali hayo yasijetokea kwani utakuwa msiba mkubwa! hivyo namshauri Padre Wilberd Slaa ajitoe kugombea urais kwani mtu hajiuzulu Upadre lakini Siasa anaweza kuwacha!

Mwenye kifafa hafai kuwa rais hata katiba yasema hivyo!
 
Dr. Slaa alishatoka huko. Kwake ni sawa kujishughulisha na siasa. Kardinali alikuwa akionya wale wanaotoa bado huduma ya kipadre kwamba wasijihusishe na siasa kwani kwa kufanya hivyo wataweza kuwagawa waamini ambao ni wanachama wa vyama mbalimbali. Wao ni wachungaji wa wote kuegemea chama fulani kutaleta mgawanyiko Kanisani kwa misingi ya itikadi. Kumbe wao wanatakiwa kuwa neutral.
Mchungaji Bibi Rwakatare???????????????
 
Shoga wa kiume huyu ! Upadri si taaluma wewe boga!


Loh labda nitakuwa tango! Kwa sisi Waswahili anaekwenda darasani huambiwa anafuata elimu na kupata elimu ni kutaalamka, sasa iwapo Mapadre huenda kupata elimu ya upadri tafsiri hubadilika? Naam buyu unasemaje?
 
Loh labda nitakuwa tango! Kwa sisi Waswahili anaekwenda darasani huambiwa anafuata elimu na kupata elimu ni kutaalamka, sasa iwapo Mapadre huenda kupata elimu ya upadri tafsiri hubadilika? Naam buyu unasemaje?


Endelea kuwa boga! Elimu hata mjinga kama wewe unaweza ipata kama vile BSc, MSc ama PhD. Upandre ni daraja na wito. Ndo maana Maalimu ama Immam hata asome vipi hawezi kuwa padre. Umeeelewa wewe boga?

Ngekewa are you a blonde with big ass?
 
Kadinali Pengo ni alichoongea ni sahihi lakini amesahau kuwakumbusha mapdri wawe mstari wa mbele kukemea maovu kama vile rushwa, wizi na ubadhirifu. Lamsingi mashahe na mapadri wasijihusishe na siasa bali wanapaswa kukemea maovu; hasa ukitilia maanani wanasiasa wote wa Tanzania (ukiachia Ngombale Mwiru na Paul Sozigwa ) wana imani za kidini. Kadinali anatakiwa kuwa muwazi vinginevyo itaonekana anampiga vijembe Dr. Slaa kwa hofu iliyopo ya ukatoliki na mgombea Slaa. Bahati nzuri udini hauna nafasi kwenye siasa za Tanzania.
 
Back
Top Bottom