Pendekezo: Prof. Kabudi awe Naibu Waziri Mkuu

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,977
Nakumbuka enzi za awamu ya pili ya mzee Mwinyi, baada ya Waziri wa mambo ya ndani mh Augustino Lyatonga Mrema kuonyesha utumishi uliotukuka " alitunukiwa" cheo kipya sawia na alichokuwa nacho akawa Naibu Waziri mkuu na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi.

Vivyo hivyo kwa utumishi uliotuka wa Prof. Palamagamba Phillip Aidan Kabudi napendekeza pamoja na cheo chake cha sasa awe pia Naibu Waziri mkuu.

Nina hakika ndani ya Bunge la sasa mchakato utakuwa rahisi.

Nawatakia Dominica yenye baraka

Maendeleo hayana vyama
 
Duh Wabunge 364, Mawaziri na manaibu Waziri 40+, Wakuu wa Wilaya zaidi ya 60, wakuu wa Mkoa 28+ bado unahisi vyeo havitoshi?
 
UKIZEEKA UTAKUWA KAMA PASCAL MAYALLA.

AMA UTAKUWA MALLAYA.

Huwa unaandika utopolo sana.
KABUDI AMEONYESHA UMAHIRI MKUBWA SANA AKIWA UDSM.
NJE YA HAPO AMEIFANYIA NINI WIZARA ALIZOZIONGOZA 5 YEARS.

Jifunze ku digest.
Huo ni mtazamo wako manka!
 
Bora awe Makamo wa Rais no. 2 na Naibu Waziri Mkuu na Mkuu wa Tume ya Uchaguzi na Mwenyekiti wa kusajili vyama
 
Tatizo lako unataka kusikia yale unayoyapenda tu!
Sasa niwe tayari kusikia hoja isiyoungwa mkono na sheria yoyote nchini halafu huyo mtu niendelee kumpa heshima anayostahili? Kwa huu utopolo wako ni sahihi hata Mimi nikipendekeza Shamsi Vuai Nahodha awe Waziri Mkuu wa Zanzibar?
 
Back
Top Bottom