meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,349
- 4,674
ni wiki kama moja hivi tumetoka kwenye mgomo wa kihistoria nchini,mgomo wa madaktari.kuna madai mengi yaliwasilishwa na madaktari ingawa kipropaganda tuliishia kuona madai mawili yakiongelewa sana,ni kuhusu maslahi na kuondolewa kwa mawaziri wa afya.
Kwa sasa hali ni ''shwari'' ingawa sina uhakika na tija ya ufanyaji kazi huko mahospitalini.
Kuna dai moja la msingi ambalo sikutegemea serikali au wananchi kulipuuzia kama kweli tunataka maendeleo. Dai hilo ni kuhusu kuboreshwa kwa mazingira ya kazi hasa hasa katika kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana mahospitalini.
MSD ni chombo cha serikali kilichopewa dhamana ya kuhakikisha dawa na vifaa tiba muhimu na bora vinapatikana katika mahospitali yetu.
Kumekuwepo na malalamiko mengi yanayoshutumu utendaji kazi wa MSD lakinu sijaona hatua stahiki iliyochukuliwa mpaka sasa.
Kwa maoni yangu naona ni wakati muafaka wadau mbalimbali kuishinikiza serukali itoe fursa ya kumpata mshindani wa MSD. Hii ni njia muhimu ya kuhakikisha tunapata huduma nzuri hasa katika hospitali za serikali.
Kwa sasa hali ni ''shwari'' ingawa sina uhakika na tija ya ufanyaji kazi huko mahospitalini.
Kuna dai moja la msingi ambalo sikutegemea serikali au wananchi kulipuuzia kama kweli tunataka maendeleo. Dai hilo ni kuhusu kuboreshwa kwa mazingira ya kazi hasa hasa katika kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana mahospitalini.
MSD ni chombo cha serikali kilichopewa dhamana ya kuhakikisha dawa na vifaa tiba muhimu na bora vinapatikana katika mahospitali yetu.
Kumekuwepo na malalamiko mengi yanayoshutumu utendaji kazi wa MSD lakinu sijaona hatua stahiki iliyochukuliwa mpaka sasa.
Kwa maoni yangu naona ni wakati muafaka wadau mbalimbali kuishinikiza serukali itoe fursa ya kumpata mshindani wa MSD. Hii ni njia muhimu ya kuhakikisha tunapata huduma nzuri hasa katika hospitali za serikali.