Heche ni muziki mwingine kabisa mkuu; kwake yeye manenomaneo 19% ila kwa utendaji kazi uliotukuka ni 91%.
Hata siku moja mtu asidhani kwamba hatuwaoni hawa wana-CDM wanaokesha wakijituma kila leo kwa faida ya WaTanzania wote lakini bila kujikweza kila leo kwenye vyombo vya habari pasipo na ulazima.
Huyu kijana anastahili promotion kwa maoni yetu sisi tunaowatazameni huku nje ya uwanja.
hivi mbona una dharau sana we msomi mav*?
Kwani Boda boda na vijiweni sio watz??
Mfumo wa kubebana haupo,mbowe hajawa mbunge 2010 pekee, unataka kuwadanganya watu bila kaka yake heche kupiga kampeni mr mbowe angepigwa chini? Je 2000~2005 ubunge alipewa na nani?
Unavoamini eti ubunge wa mbowe haukutoka kwa wananchi? Jikaze we mtoto utachumbiwa!
halafu wala si wengi ni wawili ama watatu kikubwa wana ac nyingi na kila moja anakot mwenzake wanajaza page pumba kibao matusi saana ila mi nasikitika mdogo wangu ZITTO kwa nini apendwe na hawa jamaa!!!!! mungu ongeza nguvu uilinde chadema dhidi ya maadui wa ndani na nje
Pichani ni katika mikutano mbalimbali inayoendeshwa na Mwenyekiti BAVICHA huko mkoani Kagera. Kijana huyu ameonyesha njia ya nini kinatakiwa sasa hivi kufanya badala ya kuhangaika na kulalakinia serikali kama Zitto afanyavyo.
Kwa mtazamo wangu afanyacho Zitto anataka serikali ya CCM ijirekebishe na hivyo kukosa uhalali wa kujenga hoja ya kuikosoa makosa yao wakati wa uchaguzi mkuu ujao, ndo maana naona viongozi wengi wa Chadema taifa hawako na ajenda za kulalamikia serikali au kuinyooshea vidole, ila kuwaelewesha wananchi.
Adui mkubwa wa CCM ni yule anayeingia vijijini kuwafungua akili wananchi, hawa wa kulalamika mjengoni hawainyimi serikali na CCM usingizi.
Zitto anatakiwa aelekeze nguvu huko kwenye kujenga chama matawini kama wenzake wanavyofanya. Kufanya afanyayo yamefanywa miaka nenda rudi na vyama vya upinzani kuanzia NCCM Mageuzi, CUF na vinginevyo bila kubadili sura ya wapiga kura kwa sababu hawakuingia kwenye source kubwa ya wapiga kura vijijini ambako CCM wamejichimbia kujihakikishia turufu ya kura kwenye uchaguzi mkuu.
Neno mwanamapinduzi limepoteza maana sasa Heche naye ni mwanamapindunzi.
Kama walivyokupa ukurugenzi wa halmashauri na bunge wakati hata kuwa mwenyekiti wa mtaa wa vunjo hujawahi!
Mbowe aka disco joka aka mkwe wa mtei aka mjasilia mali wa kisiasa.
Ha ha haaaa! unanikumbusha mzoea vya kunyonga....
Kama alivyo uwawa chacha zakayo wangwe!
Mkuu umenifurahisha kwa mapointi yako uliyomwaga hapa..
Mbowe anasomesha mtoto chekechea kwa milion 15 vp wewe unakulipa sh ngapi kwa kazi ya chadema TV?
Kula posho bwamdogo maana mwakani huna chako ila boss wako analijua hilo.
WanaJF,
Kiongozi wa Bavicha Taifa John Heche ni kati ya wanamapinduzi waliojitolea na kufanya kazi kubwa sana ya kupigiwa mfano.
Kila tunaposoma vyombo vya habari John Heche anaripotiwa yuko vijijini kufungua mashina, ofisi na kuingiza wanachama wapya. Ni mwezi uliopita tu alikuwa mikoa ya nyanda za juu kusini na kuingiza maelfu ya wanachama.
Wiki hii mwanzoni alikuwa Morogoro na leo yuko vijijini Kagera akifanya kazi kubwa ajabu. Hata anapokuwa mapumzikoni Dar John Heche hatulii ofisini bali anazunguka kila kona ya Dar akifanya mikutano na kuzindua mashina.
Ni wazi kabisa kwamba kiongozi anayependwa na nyota wa chama hicho kwa sasa Katibu Mkuu Dr Willibrod Slaa amekuwa na majukumu mengi kiasi kwamba pengo la Naibu katibu mkuu Bara linaonekana wazi.
Naibu Katibu mkuu Zitto Kabwe amekuwa na majukumu mengi ya kibunge kiasi kwamba anashindwa kumsaidia Katibu mkuu majukumu yake.Zitto awe tu mjumbe wa Kamati kuu ambaye atakuwa hana majukumu ya kila siku ndani ya Sekretariati.
Ninatoa mapendekezo kwa viongozi wa chama kwamba ikiwezekana katika uchaguzi wa sekretariati mpya mwakani John Heche akabidhiwe mikoba ya Zitto Kabwe kwa ufanisi zaidi.Ikumbukwe kutokana na majukumu mengi ya kibunge ya Zitto ameshindwa karibu mara 4 mfululizo kuhudhuria vikao muhimu vya chama hicho vilivyotoa maamuzi mazito.
John Heche ni Jasiri, mpambanaji, anayefanya kazi usiku na mchana na aliyejitolea maisha yake kwa ajili ya CHADEMA.
Hakika John Heche ni jembe kwelikweli anayepaswa kupandishwa daraja zaidi.
Nawasilisha.
Mkuu Candid Scope umeupitia huu uzi wa mwenzako https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/327840-pendekezo-john-heche-amrithi-zitto-kabwe.html
Swali; why Heche vs Zitto? na sio Heche vs wengine au Zitto vs wengine
Kunawatu humu ndani wanatuhumiwa kulipwa na Nape kufanya kazi fulani, sasa je na ninyi mnalipwa na nani kufanya nini?
paulss
Achana na hao, sisi wengine ni mahiri katika uchambuzi, na tumeshawahi kuwa na uzoefu katika vyombo vya kimataifa. Nafasi niliyofanya katika moja ya magazeti ya Marekani katika kipindi cha uchaguzi wa Bush nikiwa mwanafunzi huko nilipata kujifunza mengi ambayo waandishi tunatakiwa kufanya tofauti na tufanyavyo Tanzania.
Waandishi na vyombo vingi vya habari Tanzania kinachofanyika zaidi ni uhabarishaji, lakini uchambuzi katika mambo kama ninayofanya ni wachache sana, na ndio maana wanahitimisha kwamba unafanya kwa kulipwa na fulani. Vyombo vingi vinawoga, waandishi wengi wanafanya kazi zao kwa wasiwasi na kujaa woga. Woga huo ndio unaotumiwa na watawala kuwapumbaza kwa bahasha za kaki na kuishia kunyamazia habari muhimu.
Umegundua habari moja muhimu sana ya kuhusu mauaji ya Mwangozi ambayo Umoja wa nchi za Ulaya wameishuku Tanzania na kutaka haki itendeke kwa uwazi na uchunguzi uwe kwa uwazi na wahusika wachukuliwe hatua, utaona habari hiyo imenywea kabisa katika vyombo vyote vya habari, ni IPP tu ndio waliotoka kifua mbele katika hili. Huu ndio uanahabari wa Tanzania.
Unaweza kukumbuka mada kadhaa nyingi ambazo nilizileta kuhusu utendaji wa Mbunge Filikunjombe, wengi walinituhumu kuwa:
Ukweli umekuja kujithihirika baada ya wengi kujua undani wa Mbunge huyo na sasa kauli zile zimepotea baada ya kusoma ukweli.
- Filikunjombe mwenyewe anajitangaza
- Nafanya kazi ya kumtangaza kwa malipo
Tulio na uwezo wa kuchambua mambo haya tunatakiwa tujitahidi ili kuwaelimisha watanzania wengi ambao bado wanamwangalia mtu kwa upande mmoja tu bila kuangalia pande zote, matatizo ndiyo yanajitokeza mtu akishashika madaraka na kujutia, lakini kasoro tunazoziona na kuwatahadhalisha hawazioni na kuishia kuwa majuto ni mjukuu.
Hata vyombo vingi vya habari utakuta wanapomwita mhusika au kukutanisha jopo la watu kujadili jambo fulani, utakuta maswali muhimu ya msingi hayaulizwi ambayo hata mwanafunzi wa shule ya msingi angeweza kuuliza, na hivyo kukosa uwazi wa tukio na kukosa kupata msimamo na ukweli wa kitu halisi kutoka kwa wahusika. Hapo ndio utakapoona udhaifu huu wanautumia kujibu kwa majigambo na bila wasiwasi kwa vile hakuna wa kuwanyooshea vidole.
Mbowe huwa hataki tuandamane posta maana tutavunja billcanas kwa hio atakosa soko la kuuza madada zetu.
WanaJF,
Kiongozi wa Bavicha Taifa John Heche ni kati ya wanamapinduzi waliojitolea na kufanya kazi kubwa sana ya kupigiwa mfano.
Kila tunaposoma vyombo vya habari John Heche anaripotiwa yuko vijijini kufungua mashina, ofisi na kuingiza wanachama wapya. Ni mwezi uliopita tu alikuwa mikoa ya nyanda za juu kusini na kuingiza maelfu ya wanachama.
Wiki hii mwanzoni alikuwa Morogoro na leo yuko vijijini Kagera akifanya kazi kubwa ajabu. Hata anapokuwa mapumzikoni Dar John Heche hatulii ofisini bali anazunguka kila kona ya Dar akifanya mikutano na kuzindua mashina.
Ni wazi kabisa kwamba kiongozi anayependwa na nyota wa chama hicho kwa sasa Katibu Mkuu Dr Willibrod Slaa amekuwa na majukumu mengi kiasi kwamba pengo la Naibu katibu mkuu Bara linaonekana wazi.
Naibu Katibu mkuu Zitto Kabwe amekuwa na majukumu mengi ya kibunge kiasi kwamba anashindwa kumsaidia Katibu mkuu majukumu yake.Zitto awe tu mjumbe wa Kamati kuu ambaye atakuwa hana majukumu ya kila siku ndani ya Sekretariati.
Ninatoa mapendekezo kwa viongozi wa chama kwamba ikiwezekana katika uchaguzi wa sekretariati mpya mwakani John Heche akabidhiwe mikoba ya Zitto Kabwe kwa ufanisi zaidi.Ikumbukwe kutokana na majukumu mengi ya kibunge ya Zitto ameshindwa karibu mara 4 mfululizo kuhudhuria vikao muhimu vya chama hicho vilivyotoa maamuzi mazito.
John Heche ni Jasiri, mpambanaji, anayefanya kazi usiku na mchana na aliyejitolea maisha yake kwa ajili ya CHADEMA.
Hakika John Heche ni jembe kwelikweli anayepaswa kupandishwa daraja zaidi.
Nawasilisha.