Kiwi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 1,054
- 990
Mr. Paul Sozigwa, aliyewahi kuwa Mwandishi wa Habari katika serikali ya Mwalimu Nyerere, amepotea tangu jana mchana katika mazingira ya kitatanishi. Mara ya mwisho alionekana kanisani Mbezi Beach BCIC (kwa Gamanywa) jana Jumapili saa nane mchana. Kupotea huku kunaleta mashaka hasa kwa kuwa Mzee Sozigwa ni mgonjwa wa Alzheimer, na mara nyingi anapoteza kumbukumbu. Taarifa ya kupotea kwake imeshatolewa polisi na kupatiwa RB.
Vilevile kupotea huku kunasadikiwa kunahusiana na suala la mauzo ya nyumba yake ya Kurasini ambayo iliuzwa kinyemela na aliyekuwa mkewe Monica Kuga. Huyo mama aliachana na Mzee Sozigwa kwa takriban miaka 34 kuanzia mwaka 1973 mpaka mwaka 2009, aliporudi kwa madai ya kuja kusaidia matunzo ya Mzee Sozigwa. Wakati huo huo akafanya utapeli na kuuza nyumba ambayo tayari Mzee alishaandika wosia kabla ya kuugua na kumkabidhi mtoto wake wa kiume anayeitwa Moses Sozigwa. Hiyo nyumba bado ina kesi kwa kuwa tayari wakati inauzwa na Mama Monica Kuga ilishakuwa na zuio la mahakama.
Mara ya mwisho Mzee Sozigwa alikuwa amevaa shati jeupe lenye mistari ya bluu na kijivujivu, suruali nyeusi na viatu vyeusi. Anapoulizwa anakaa wapi hujibu Kisarawe ama Vidunda, wilaya ya Kisarawe. Atakayemuona anaombwa kupiga simu zifuatazo:
Mch. Moses Sozigwa 0712 379818, 0755 716158
Mrs. Irene Yussuf 0784 300418
Ms. Lucy Paul Sozigwa 0755 564080, 0717 310783
Mrs. Judith Mlawa 0712 834737
Unaweza pia kuwasiliana nao kwa Whatsapp na Viber
Namkumbuka mzee Paul Sozigwa ndiye aliyemshauri Mwalimu Nyerere astaafu ili apishe watu wengine wasimamie mageuzi ya kiuchumi kwani asingeweza kupingana na misimamo yake.
Baada ya maelezo ya Sozigwa, mawaziri wanafiki kama Malechela walitegemea mwalimu angehamaki na kumfuta kazi mwalimu, badala yake mwalimu alikuwa mpole na kumsifu sozigwa kwa ushauri wake.
Baada ya kikao kile mwalimu alimwita Cleopa Msuya na kumpatia kazi ya kusimamia mageuzi kama alivyopendekezwa na tume ya Paul Bomani. Msuya akapewa kazi ya kuzungumza na world bank na IMF juu ya reforms za kiuchumi na hapo mzee akaanza safari ya kung'atuka.
Kwangu mie mzee Sozingwa kupotea kama mlevi wa kimpumu sikubaliani hata kidogo, nakumbuka mara ya mwisho nilimwona akiwa na Majidd Mjengwa Sweden alikokuwa kwa matibabu, chonde JK hakikisha huyu mzee anapewa heshima inayostahili.
===========================
===========================
Tunawashukuru wote waliokuwa pamoja na familia katika suala hili. Mzee Sozigwa amepatikana jana usiku na amesharudi mikononi mwa familia!
Tuendelee kuombeana na kutiana nguvu katika kumtunza Mzee wetu. Anahitaji uangalizi wa hali ya juu sana, na hili limetupa fundisho litakalotusaidia siku zijazo. Pia nawaomba wanajamvi tuendelee kuelimishana na kuwaelimisha watu wengine ya kuwa kuna ugonjwa huu unaoitwa Alzheimer, ambao unakula ubongo na kufanya mtu kupoteza kumbukumbu. Ugonjwa hauna dawa ya kuuponya mpaka sasa, ila kuna dawa za kutumia mtu anapokuwa katika hatua za awali kuzuia usiendelee! Tafadhali tuwatazame na kuwachunguza wazazi na ndugu tulio nao ili kama mtu akionyesha dalili kama hizo awahi kupata dawa ili usiendelee.
Sina namna ya kuwashukuru zaidi ya kusema kutoka moyoni, ASANTENI SANA!