Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam awataka Wananchi kutuma taarifa za watu wanaojihusisha na ushoga na mapenzi ya jinsia moja waliopo kwenye mkoa wake
Paul Makonda amesema kuwa wamekuwepo 'mashoga' wanaojinadi kupitia Mitandao ya Kijamii, ataka wananchi wamtumie taarifa zao kuanzia siku ya leo hadi Jumapili
Kosa hili liko wazi ndio maana hukumu yake ni kifungo cha maisha au miaka 30 jela hii kuonesha kuwa serikali iko makini na haitaki maadili yaharibike
Makonda asema kuwa majina yote ya watu wanaovunja maadili ya Mtanzania watume kwenye namba yake ya 0682009009
Asema kuwa mwanadada Amber Ruty na mpenzi wake wako chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi tangu alipotangaza wajisalimishe kituoni
“Tayari Amber Rutty na Bwana yake wapo chini ya Polisi, pia nimepata taarifa kuwa kuna mashoga kazi yao kujinadi mitandaoni, kuanzia leo Jumatatu hadi Jumapili napokea taarifa ya jina lolote la anayefana vitendo kinyume na maadili ya kitanzania, yapo makundi mengine WhatsApp kazi yake kuhamasisha tendo la ngono, tumeamua kulivalia njuga suala la makosa ya kimtandao” RC Makonda.