Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,621
- 6,512
Niliwahi kuanzisha uzi siku za nyuma nikisema huyu kijana anaandaliwa kuitawala Dar es Salaam kwa jinsi Bwana mmoja anayeitwa Robert Moses alivyoitawala New York. Nakumbuka kuna jamaa mmoja alikuwa anabisha anasema nisimlinganishe kijana kama Makonda na mtu mzito aliyejenga historia kama Robert Moses.
Base ya post yangu ilikuwa kuwa Makonda yupo na ataendelea kuwepo kwa muda mrefu sana na kila mradi wowote mkubwa utapitishwa kwenye ofisi yake na sifa nyingi atakuwa anapewa yeye. Tayari tunashuhudia hayo. Kuna wanaosema amekuwa kama Naibu Rais kwa sababu si cha waziri, Waziri Mkuu au Makamu wa Rais mwenye sauti juu yake. Sitashangaa kuendelea kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa miaka 30 ijayo.
Robert Moses alikuwa na mamlaka makubwa sana, yeye ndiye alikuwa kila kitu na alirundikiwa mavyeo kibao tu. Kwa kiasi ilirahisisha utendaji wake wa kazi kwa sababu iliondoa urasimu. Tofauti kubwa ni kuwa kwa Makonda mamlaka alizopewa hazijarasimishwa. Kila mtu ameshaliona hilo.
Ule uzi nimejaribu kuutafuta siuoni, kwa kweli kuna wakati mods wa JF wanakatisha tamaa sana. Nakumbuka kama walikujaga kuuunganisha na uzi mwingine wa Makonda ambao ulikuwa hauhusiani na nilichokuwa naongelea mimi. Kuna wengine hata tukiwa na nondo ya kuleta humu, huwa tunajiuliza mara mbili mbili na mara nyingi na mara nyingi tunaamua kupotezea tu.
Base ya post yangu ilikuwa kuwa Makonda yupo na ataendelea kuwepo kwa muda mrefu sana na kila mradi wowote mkubwa utapitishwa kwenye ofisi yake na sifa nyingi atakuwa anapewa yeye. Tayari tunashuhudia hayo. Kuna wanaosema amekuwa kama Naibu Rais kwa sababu si cha waziri, Waziri Mkuu au Makamu wa Rais mwenye sauti juu yake. Sitashangaa kuendelea kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa miaka 30 ijayo.
Robert Moses alikuwa na mamlaka makubwa sana, yeye ndiye alikuwa kila kitu na alirundikiwa mavyeo kibao tu. Kwa kiasi ilirahisisha utendaji wake wa kazi kwa sababu iliondoa urasimu. Tofauti kubwa ni kuwa kwa Makonda mamlaka alizopewa hazijarasimishwa. Kila mtu ameshaliona hilo.
Ule uzi nimejaribu kuutafuta siuoni, kwa kweli kuna wakati mods wa JF wanakatisha tamaa sana. Nakumbuka kama walikujaga kuuunganisha na uzi mwingine wa Makonda ambao ulikuwa hauhusiani na nilichokuwa naongelea mimi. Kuna wengine hata tukiwa na nondo ya kuleta humu, huwa tunajiuliza mara mbili mbili na mara nyingi na mara nyingi tunaamua kupotezea tu.