OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,191
- 103,715
Wakati wa utawala wa Hayati Magufuli iliwahi kuibuliwa kashfa ya kughushi vyeti vya elimu ya sekondari kwa Paul Makonda. Paul akiwa mkuu wa mkoa wa mkoa nyeti sana alipata kashfa hii pasipo mamlaka ya uteuzi wala elimu kumshughulikia.
Lakini tena limeibuka sakata la umiliki wa kiwanja kati yake na GSM. Katik kujitetea Makonda ameonyesha hati ya mauziano ambayo nimeambatanisha kwenye uzi.
Ukiitazama hati hiyo inaonekana na kasoro kadhaa
1. Mihuri imepigwa chini ya picha badala ya kupigwa juu ya picha
2. Hati haijakamilika kwa sababu kamishna wa ardhi hakuidhinisha mauziano hayo
Wataalamu wenzangu naomba tujadili kwa mustakabali wa kujielimisha. Je, Bashite ameghushi tena?