Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,607
- 3,187
Tiba
Nijuavyo mimi (and I stand to be corrected) Ukuu wa wilaya ni kazi ya kisiasa na kazi za kisiasa kiuhalisia hazina kitu kinachoitwa KUSTAAFU. Utendaji wa serikalini ndio una kitu kiitwacho kustaafu. Ukuu wa wilaya, mkoa au hata uwaziri ni swala la maamuzi ya mtu mmoja kuamua akuteue au akuache kwa mapenzi yake. Na ni swala la wewe kukubali au kukataa lakini sio KUSTAAFU.
Kuna mama mmoja Mwanza alikuwa anateuliwa kila wakati na Che Nkapa katika nafasi za ukuu wa wilaya lakini alikuwa haendi sababu alikuwa anafanya kazi ya maana Unicef iliyokuwa ikimpa mapesa mengi. Nadhani na naamini kazi za kisiasa (ukiondoa urais kwa sababu baada ya kuchaguliwa hubadilika kuwa kama mtendaji na mwajiri mkuu wa watumishi wote wa serikali) huwa hazina KUSTAAFU kwa sababu hazina hata umri wa mwisho kuziomba hata ukiwa na miaka 90 unaweza kuteuliwa ama kuchaguliwa na wapigakura.
Nachelea kukubali kuwa Jenerali Ulimwengu ALISTAAFU Ukuu wa wilaya. Nadhani usahihi ni kuwa alikataa kupokea mabadiliko ya kuhamishwa ama uteuzi aliopewa na hivyo kuachana na siasa.
As I've said earlier, I stand to be corrected!
Mkuu bibikuku, kimsingi nakubaliana na maelezo yako. Basi tuseme Ulimwengu alijiuzulu nafasi ya ukuu wa Wilaya.
Tiba