Patrick Rutabanzibwa: UKWELI ni upi?

Patrick Rutabanzibwa: UKWELI ni upi?

Ahahahahahah... Bukya. umemsikia TAYADI? Nimekua nawaambia ndugu zangu kuweni na tahadhari kubwa na hizi operesheni za chuki,wakimaliza wenye asili ya Rwanda itakua zamu yetu Wahaya! Dhambi hii haitatuacha salama.
Bukyanagandi, hawezi kuona mpaka ulink kwa kutumia kitu kama dunia chenye macho mawili kwenye box la tatu baada ya B I U
 
Kaka katika maisha yangu yote tokea enzi za mwalimu sijawahi kusikia mtu anaestaafu kwa hiari kama kweli alikuwa mchapakazi hodari, wachapakazi hodari hawastaafu kwa hiari hata wakifika umri wa kustaafu wanaongezewa muda
Crapppppp....
 
Wakati IPTL inaingia Tanzania baada ya kukataliwa Kenya yeye ndiye alikuwa katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini,alihusika sana na kuandaa mikataba mibovu iliyoenda kujadiliwa na baraza la mawaziri na leo tumeona jinsi TANESCO na watanzania tulivyokamuliwa...Kubenea ipi ajenda ya siri unayotaka kutuaminisha watanzania?
 
Ahahahahahah... Bukya. umemsikia TAYADI? Nimekua nawaambia ndugu zangu kuweni na tahadhari kubwa na hizi operesheni za chuki,wakimaliza wenye asili ya Rwanda itakua zamu yetu Wahaya! Dhambi hii haitatuacha salama.
Mkuu Timbilimu, we're used to these kinds of tirade - uzuri tunajua kinacho sababisha yote haya - mkuu unajua kuna baadhi ya Watanzania wenzetu wenye latent ... ya raia wanao toka kanda fulani bila ya sababu za msingi! Hata kama wanajua jina lako awalisemi, utawasikia wanasema yule 'MCHAGA' au yule 'MHAYA' yaani inakuwa raisi kwao kutamka kabila badala ya kutamka jina!! Mimi niliuliza swali dogo tu kwamba mbona Jenerali Ulimwengu aliwahi kuomba kustaafu kazi mapema, na bila shaka alitoa sababu za msingi ndio maana alikubaliwa kustaafu mapema - ni hilo tu! Sasa kulikuwa na sababu gani ya baadhi ya wanaJF kunijia juu - kama wana issues binafsi na mzalendo Rutabanzibwa waseme na sio ku-vent hasira zao kwa watu wengine.
 
Generali Ulimwengu sijui sababu hasa zilizomfanya astaafu mapema lakini najua wajuzi watadadavua hili
Mkuu Taifa letu lilipo ruhusu raia kumiliki vyombo vya habari/magazeti, ndugu Ulimwengu alikuwa ni among ya jamaa walio anzisha makampuni za media.
 
Kaka katika maisha yangu yote tokea enzi za mwalimu sijawahi kusikia mtu anaestaafu kwa hiari kama kweli alikuwa mchapakazi hodari, wachapakazi hodari hawastaafu kwa hiari hata wakifika umri wa kustaafu wanaongezewa muda
Sio kweli.
Wapo wachapa kazi wengi tu ambao wali-resign kwa hiyari yako si Tanzania tu bali dunia nzima
 
Wakati IPTL inaingia Tanzania baada ya kukataliwa Kenya yeye ndiye alikuwa katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini,alihusika sana na kuandaa mikataba mibovu iliyoenda kujadiliwa na baraza la mawaziri na leo tumeona jinsi TANESCO na watanzania tulivyokamuliwa...Kubenea ipi ajenda ya siri unayotaka kutuaminisha watanzania?
Hapa hii habari inanichanganya.
Kuna report niliisoma juu ya hiyo IPTL saga, ambapo inasisitiza kuwa Patrick ndio alimfuata na kumshauri Mkapa kwa kumwambia waachane na IPTL then watafute alternative nyingine other than IPTL, na kam hiyo alternative nyingine inge-fail then yeye Patrick ali-offer kujiuzulu, ila Mkapa alikataa.
Sasa sijui which is which.
Anyways, hii mikanganyiko inanifanya ni-dive deep hata ktk ile issue ya Richmond-Dowans-Symbion..........nikijumlisha moja jumlisha moja napata 2, meaning hata huyo Lowassa nakuwa-convinced kuwa hakuwa na kosa lolote.
Kama Lowassa ana kosa kwenye Simbion basi hata Barrack Obama anakosa.
 
Kaka katika maisha yangu yote tokea enzi za mwalimu sijawahi kusikia mtu anaestaafu kwa hiari kama kweli alikuwa mchapakazi hodari, wachapakazi hodari hawastaafu kwa hiari hata wakifika umri wa kustaafu wanaongezewa muda
Kutokusikia kwako kusifanye hiyo ndiyo iwe ukweli halisia kwa kila Mtanzania. Kwanza kutokusikia kwako kunategemea na angle ya maisha yako ilipo. Jaribu kufanya research kwanza kutafuta ukweli kuliko kusubili kusikia.

Kuna watu vile vile hawakuwahi kumsikia 'Yesu au Mtume Muhammad (S.A.W)' mpaka wamekufa lakini haina maana kuwa hawa jamaa hawakuwahi kuwepo hapa duniani kama ilivyobainishwa na research na maandiko ya kale.
 
Ishu hapa ni hili gazeti la kubenea kusema DR Slaa amekiri huyu jamaa sio fisadi
natamanikusikia chadema wanasemaje na hili

Mbona inajulikana kuwa suala la list of shame ilitolewa kwa malengo ya kisiasa na kujitafutia cheap popularity.
 
Nadhani upo umuhimu wa kumtendea haki mtu hasa kama ametumikia vyema taifa.Patrick Rutabanzibwa kwa watu wa karibu wanajua misimamo yake na haogopi mtu.

Kama upo ufisadi wake wekeni wazi ili tumtendee haki badala ya kumuita fisadi tu kwa maneno.Issue kubwa kama ya IPTL nadhani inapotoshwa sana pia.Nimuombe Invisible aongee na Patrick aje humu tuzungumze naye ili tumtendee haki maana ukipata habari zake kwa ukaribu utashangaa jinsi watu wengine wanavyomzungumza humu.

Binafsi najua jinsi alivyoingia kwenye mgogoro mkubwa na Mhaya mwenzake mmoja baada ya kuwatibulia issue yao ya IPTL lakini kuna watu bado wanasema vingine.Pengine hatuna taarifa za kutosha kumtendea haki.
 
Last edited by a moderator:
Jenerali Ulimwengu alistaafu cheo kipi??????? Ubunge au????????????

Alistaafu ukuu wa Wilaya. Alikuwa mkuu wa Wilaya ya Ilala na baada ya kuishushua serikali juu ya rushwa bungeni alipigwa transfer kwenda Singida. Sina uhakika kama kweli alikwenda Singida lakini ni kipindi hicho hicho alitangaza kustaafu.

Tiba
 
Si katika miradi mikubwa tu kama hiyo uliyoitaja tu, hata sisi wananchi wanyonge wa maeneo ya Luguruni, Kwembe n.k ambao watumishi wa wizara ya ardhi walikuwa wametupora fidia na ardhi zetu tunamtakia mapumizko mema kwani bila yeye fidia na ardhi za wananchi wanyonge visingepatikana kabisa
 
acha kuzusha maneno bila ushahidi.......una ushahidi wa hili unalosema? .... maana documents tulizoona sisi ni kuwa yeye aliipinga na akamshauri mkapa aikatae lakini kukawa na wajanja wengine ndio waliomsukuma Mkapa kuikubali IPTL akiwemo JK!

Msimamo wake kuhusu IPTL ulikuwa wazi lakini kibao kageuziwa yeye!!!
 
Wakati IPTL inaingia Tanzania baada ya kukataliwa Kenya yeye ndiye alikuwa katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini,alihusika sana na kuandaa mikataba mibovu iliyoenda kujadiliwa na baraza la mawaziri na leo tumeona jinsi TANESCO na watanzania tulivyokamuliwa...Kubenea ipi ajenda ya siri unayotaka kutuaminisha watanzania?

CHASUZY wew ni mzushi na haujui historia ua IPTL. Kama sisi Rutabnzibwa nchi hii ingeibiwa milele mikataba hiyo ilingiwa wakati yeye akiwa katika matibabu ya ugonjwa kiharusi (stroke) na aliporejea kama Katibu Mkuu ndiye aliyefanya uchunguzi na kuagiza kama serikali mitambo kama hiyo hiyo na kampuni iliyouza mitambao kwa IPTL kuipatia serikali bei ya chini kuliko ile IPTL waliyodai kununulia mitambo hiyo ndipo akalipua bomu la IPTL na mpaka sasa watanzania kunusurika na mafisadi hawa
 
Si katika miradi mikubwa tu kama hiyo uliyoitaja tu, hata sisi wananchi wanyonge wa maeneo ya Luguruni, Kwembe n.k ambao watumishi wa wizara ya ardhi walikuwa wametupora fidia na ardhi zetu tunamtakia mapumizko mema kwani bila yeye fidia na ardhi za wananchi wanyonge visingepatikana kabisa

Huyu bwana alivyomkali hakuna mtumishi anayeweza kumpenda hasa kwa mazoea yetu.
 
Huyu bwana alivyomkali hakuna mtumishi anayeweza kumpenda hasa kwa mazoea yetu.

watumishi Wizara ya Ardhi walikuwa wakija kufanya upimaji eneo la Satellite City Luguruni wanajilipa posho kama vile wanakwenda mkoani, alipoingia kama Katibu Mkuu walikatwa fedha hizo katika mishahara yao. Hii ndiuo maoja ya sababu ya kufanya viwanja vinavyopimwa na Serikali kuwa bei ya juu mno ni kutokana na ufisadi kama huu
 
Wakati IPTL inaingia Tanzania baada ya kukataliwa Kenya yeye ndiye alikuwa katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini,alihusika sana na kuandaa mikataba mibovu iliyoenda kujadiliwa na baraza la mawaziri na leo tumeona jinsi TANESCO na watanzania tulivyokamuliwa...Kubenea ipi ajenda ya siri unayotaka kutuaminisha watanzania?

Wewe hujui hii nchi,mtu unaweza kuletewa mkataba na wakuu zako wanakwambia kazi yako ni kusign tu!! Labda tuseme ukiamua kufanyakazi na corrupt gov't you will be part of the problem hata kama moyo wako hauko huko!!
 
Mkuu Timbilimu, we're used to these kinds of tirade - uzuri tunajua kinacho sababisha yote haya - mkuu unajua kuna baadhi ya Watanzania wenzetu wenye latent ... ya raia wanao toka kanda fulani bila ya sababu za msingi! Hata kama wanajua jina lako awalisemi, utawasikia wanasema yule 'MCHAGA' au yule 'MHAYA' yaani inakuwa raisi kwao kutamka kabila badala ya kutamka jina!! Mimi niliuliza swali dogo tu kwamba mbona Jenerali Ulimwengu aliwahi kuomba kustaafu kazi mapema, na bila shaka alitoa sababu za msingi ndio maana alikubaliwa kustaafu mapema - ni hilo tu! Sasa kulikuwa na sababu gani ya baadhi ya wanaJF kunijia juu - kama wana issues binafsi na mzalendo Rutabanzibwa waseme na sio ku-vent hasira zao kwa watu wengine.

Ukabila na Udini unazidi kua kwa kasi ktk Tanzania kadri ujinga na umasikini unavyo zidi kita mizizi ktk nchi yetu. Baadhi yetu wamejaa chuki na hasira. Wanaangalia matatizo yao yamesababishwa na wageni siyo wao!

Mkuu mimi nadhani ni jukumu la makabila haya makubwa kuchukua hatua ya kuongoza nchi badala ya kuwaachia waswahili ambao wametufikisha hapa!
 
Alistaafu ukuu wa Wilaya. Alikuwa mkuu wa Wilaya ya Ilala na baada ya kuishushua serikali juu ya rushwa bungeni alipigwa transfer kwenda Singida. Sina uhakika kama kweli alikwenda Singida lakini ni kipindi hicho hicho alitangaza kustaafu.

Tiba
Tiba

Nijuavyo mimi (and I stand to be corrected) Ukuu wa wilaya ni kazi ya kisiasa na kazi za kisiasa kiuhalisia hazina kitu kinachoitwa KUSTAAFU. Utendaji wa serikalini ndio una kitu kiitwacho kustaafu. Ukuu wa wilaya, mkoa au hata uwaziri ni swala la maamuzi ya mtu mmoja kuamua akuteue au akuache kwa mapenzi yake. Na ni swala la wewe kukubali au kukataa lakini sio KUSTAAFU.

Kuna mama mmoja Mwanza alikuwa anateuliwa kila wakati na Che Nkapa katika nafasi za ukuu wa wilaya lakini alikuwa haendi sababu alikuwa anafanya kazi ya maana Unicef iliyokuwa ikimpa mapesa mengi. Nadhani na naamini kazi za kisiasa (ukiondoa urais kwa sababu baada ya kuchaguliwa hubadilika kuwa kama mtendaji na mwajiri mkuu wa watumishi wote wa serikali) huwa hazina KUSTAAFU kwa sababu hazina hata umri wa mwisho kuziomba hata ukiwa na miaka 90 unaweza kuteuliwa ama kuchaguliwa na wapigakura.

Nachelea kukubali kuwa Jenerali Ulimwengu ALISTAAFU Ukuu wa wilaya. Nadhani usahihi ni kuwa alikataa kupokea mabadiliko ya kuhamishwa ama uteuzi aliopewa na hivyo kuachana na siasa.

As I've said earlier, I stand to be corrected!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom