Mi ntaendelea kuwa kwenye kundi la member wakawaida ambao tunatoa michango ya mawazo na sio fedha kwani kila siku nanunua kifurushi cha 250 toka voda na chote kinaishia JF ila siyo mbaya na sisi mkatutumia hizo sms tuepuke kuwekwa katika madaraja kwani matangazo yanayowekwa humu yanatosha kuiendesha jf na pia mnapata matangazo kwa kuwa kuna watu wengi wanatembelea mtandao huu ili kuufanya uzidi kuku nchini tz na duniani kwa ujumla ili uje kuwa km facebook au tweeter, msiwagawe member wenu in term of vipato. Samahani kama nimewakwaza
Hata Maaskofu, Mapadri, Mashehe wana madaraja na privilege zao. Nasikia hata peponi ndio hivyo. Kama kwa sasa huwezi kulipia baki hivyo hivyo usijali, na umeona kusudio au lengo ni kuweza kuifanya JF iweza kulipa gharama za uendeshaji na kuweza kutuhudumia. Imagine kama jamaa wakishindwa kulipa maintanance fees na ikafungwa utashinda wapi na Shs. 250 zako?
Any way nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akuwezeshe ili na ww uweze kuchangia hii Shs. 30,000/= na mimi najiombea hivyo hivyo maana sijatoa lakini umuhimu nauona na nia ninayo....