Partnership kwenye ufugaji kuku

kayanda01

JF-Expert Member
Feb 14, 2014
1,086
913
Habari wana JF wote.
Natumai mu wazima wa afya. Poleni na majukumu ya kila siku katika kutafuta riziki ili maisha yaendelee.

Mimi nina shamba kidogo lenye ukubwa wa ekari 3. Eneo lina maji (kisima), na umeme upo (solar power). Halina fence. Eneo lipo kata ya Toangoma (maeneo ya Mbagala - DAR).

Nikafikiria namna ya kulifanya eneo hilo liwe productive. Nimepata idea ya kufanya ufugaji wa kuku. Hata hivyo, changamoto kubwa ni uhaba wa mtaji kuanzisha mradi wa kufuga kuku. Pia sina utalaamu wowote wala uzoefu kwenye ufugaji kuku.

Hivyo, natafuta mtu mwenye uzoefu kamili kwenye ufugaji kuku ambaye yeye labda changamoto ni eneo. Natafuta mtu ambaye ana physical experience kabisa kwenye kufuga kuku na masoko yake. Tufanye partnership, kwa maana ya kwamba mie mchango wangu ni eneo, huyo partner mchango wake ni utalaamu/uzoefu kwenye ufugaji kuku. Pia MTAJI (financial capital) kamili utachangiwa kutoka pande zote mbili nusu kwa nusu (by 50%).

Kuhusu USIMAMIZI wa mradi, itakuwa ni joint supervision, kwamba wote tutashiriki kwenye kuusimamia mradi bila kutegea, na kutafuta soko. Cha muhimu ni kwamba mradi uwe beneficial to both of us. Kama tutaamua kuweka kijana wa kusaidia kazi ama uangalizi, chumba kipo available kimoja kwenye shamba hilo. Mimi ninaishi Mbagala pia, ila sio karibu na shamba husika. So ningependa kupata business-partner ambaye yupo tayari, kwa pamoja, tuji-commit fully kwenye mradi huu.

Kuhusu benefits: Tukishafanya mauzo, MTAJI unatolewa kwanza, tunagawana FAIDA (net profit) nusu kwa nusu (by 50%). MTAJI unaendelea na phase inayofuata. Kama mradi ukienda vizuri, kuupanua zaidi iwe ni moja ya malengo yetu.

N.B: Tutaingia Joint Venture Agreement ambayo ni rasmi kabisa so that to create sense of ownership ya mradi kwa pande zote mbili. So hatufanyi mambo kienyeji !

Wakuu, hilo ndiyo wazo langu. Kwa yeyote who is interested na maelezo hayo, karibu sana tulisongeshe. Pia mpendwa yeyote mwenye constructive advice kwenye hili, karibuni pia mnijenge kimawazo maana penye wengi pana mengi.

Vijana tuungane kujikwamua kimaisha.

Natanguliza shukrani za dhati. Mwenyezi Mungu atubariki sote.
 
Nachoona hapa wewe umepungukiwa Uzoefu katika ufugaji na mtaji pia,
What if Mradi ukikua ukapata uzoefu na hela ya mtaji?? Hutomfukuza partner mwenzio kwenye eneo lako??


Ahsante sana mkuu kwa mchango wako. Swali zuri umeuliza. Kimsingi, huwa naamini sana kwenye umoja. Pia hii ni business partnership ambayo ni rasmi, kwa maana ya kwamba tunaingia Agreement ambayo ni legally binding, na tutaandaa agreement yenye manufaa pande zote.

Kama mradi ukienda vizuri, ni kuukuza kwa umoja na partnership ile ile. Pia kwenye Agreement hiyo tunaweza kuweka possibility ya ku-review terms from time to time, lakini ni muhimu terms hizo ziwe zenye manufaa kwa pande zote. Ndiyo maana ni MAKUBALIANO with voluntary consent. Sipendi biashara ya kugandamizana wala kuleteana magumashi.

Naamini nimejibu hoja yako mkuu wangu.
 
Ndio maana akasema wataingia makubaliano ya kisheria hivyo swala la kufukuzana halipo wazo zuri nadhani utapata mtu makini


ahsante sana mkuu kwa hiyo enlightening comment. Umenena vyema haswa. Ubarikiwe
 
you need a complete valid business plan with a verified market study before inviting anyone for possible joint venture


ahsante sana mkuu Bluetooth kwa angalizo hilo la kuwa na 'Business Plan' kwanza. I will endeavor to comply with the same.

ubarikiwe
 
Umesema 50% kwa 50%, labda wewe mwenyewe umepanga kuweka sh ngapi ktk huo mradi?


Mkuu hilo linategemea na tutavyoamua kuwa tuanze na scale production ya kiasi gani. Ila kwavile ni start-up, ni vizuri kuanza na small scale. So, the minimum/maximum contribution is open for discussion sisi wenyewe wawili as per our decision tuanze na kuku wangapi.

Nadhani ni vyema zaidi hilo likaongelewa PM.

Ahsante.
 
Nakushauri uanze mwenyewe hata kwa hicho kidogo ulichonacho...utapata uzoefu as you go along. Mi pia nipo kwenye mradi huo nimeenda taratibu sana na sasa nipo kwenye hatua za mwisho. Tatizo la kufanya kazi na mtu mnaweza kurudishana nyuma na hata kuingia kwenye migogoro ya kutafutana ubaya japo Partnership nyingine huwa zinaenda vizuri
 
Nakushauri uanze mwenyewe hata kwa hicho kidogo ulichonacho...utapata uzoefu as you go along. Mi pia nipo kwenye mradi huo nimeenda taratibu sana na sasa nipo kwenye hatua za mwisho. Tatizo la kufanya kazi na mtu mnaweza kurudishana nyuma na hata kuingia kwenye migogoro ya kutafutana ubaya japo Partnership nyingine huwa zinaenda vizuri


Asante sana Mkuu, umenipa hints muhimu mno. Pamoja kaka
 
Kama unataka kupata uzoefu anza na kuku wachache ya nyama km 200 , niko tayari kukupa free consultation; nina uzoefu wa 10 yrs sasa nilianza kidogo kidogo lkn nimekuwa naongeza idadi ya kuku wa nyama na mayai na kununua vyakula direct toka viwandani
 
Habari wana JF wote.
Natumai mu wazima wa afya. Poleni na majukumu ya kila siku katika kutafuta riziki ili maisha yaendelee.

Mimi nina shamba kidogo lenye ukubwa wa ekari 3. Eneo lina maji (kisima), na umeme upo (solar power). Halina fence. Eneo lipo kata ya Toangoma (maeneo ya Mbagala - DAR).

Nikafikiria namna ya kulifanya eneo hilo liwe productive. Nimepata idea ya kufanya ufugaji wa kuku. Hata hivyo, changamoto kubwa ni uhaba wa mtaji kuanzisha mradi wa kufuga kuku. Pia sina utalaamu wowote wala uzoefu kwenye ufugaji kuku.

Hivyo, natafuta mtu mwenye uzoefu kamili kwenye ufugaji kuku ambaye yeye labda changamoto ni eneo. Natafuta mtu ambaye ana physical experience kabisa kwenye kufuga kuku na masoko yake. Tufanye partnership, kwa maana ya kwamba mie mchango wangu ni eneo, huyo partner mchango wake ni utalaamu/uzoefu kwenye ufugaji kuku. Pia MTAJI (financial capital) kamili utachangiwa kutoka pande zote mbili nusu kwa nusu (by 50%).

Kuhusu USIMAMIZI wa mradi, itakuwa ni joint supervision, kwamba wote tutashiriki kwenye kuusimamia mradi bila kutegea, na kutafuta soko. Cha muhimu ni kwamba mradi uwe beneficial to both of us. Kama tutaamua kuweka kijana wa kusaidia kazi ama uangalizi, chumba kipo available kimoja kwenye shamba hilo. Mimi ninaishi Mbagala pia, ila sio karibu na shamba husika. So ningependa kupata business-partner ambaye yupo tayari, kwa pamoja, tuji-commit fully kwenye mradi huu.

Kuhusu benefits: Tukishafanya mauzo, MTAJI unatolewa kwanza, tunagawana FAIDA (net profit) nusu kwa nusu (by 50%). MTAJI unaendelea na phase inayofuata. Kama mradi ukienda vizuri, kuupanua zaidi iwe ni moja ya malengo yetu.

N.B: Tutaingia Joint Venture Agreement ambayo ni rasmi kabisa so that to create sense of ownership ya mradi kwa pande zote mbili. So hatufanyi mambo kienyeji !

Wakuu, hilo ndiyo wazo langu. Kwa yeyote who is interested na maelezo hayo, karibu sana tulisongeshe. Pia mpendwa yeyote mwenye constructive advice kwenye hili, karibuni pia mnijenge kimawazo maana penye wengi pana mengi.

Vijana tuungane kujikwamua kimaisha.

Natanguliza shukrani za dhati. Mwenyezi Mungu atubariki sote.

Kwa nini usianze small,mradi wa kuku unakupa nafasi kubwa sana ya kuanza kidogo,japo hujataka ushauri lkn naomba nikushauri usitafute partnership kwny ufugaji hasa km ww mwnyw huna experience na hii kitu,give urself time to learn about chicken before u start thinking about making a profit,anza hata na kununua vifaranga 100,kabla ya hapo soma threads za ufugaji humu jf,ujifunze jinsi ya kulea vifaranga.
 
Kwa nini usianze small,mradi wa kuku unakupa nafasi kubwa sana ya kuanza kidogo,japo hujataka ushauri lkn naomba nikushauri usitafute partnership kwny ufugaji hasa km ww mwnyw huna experience na hii kitu,give urself time to learn about chicken before u start thinking about making a profit,anza hata na kununua vifaranga 100,kabla ya hapo soma threads za ufugaji humu jf,ujifunze jinsi ya kulea vifaranga.


ahsante kwa ushauri mzuri mkuu. nimepata kitu kwenye maelezo yako
 
Kama unataka kupata uzoefu anza na kuku wachache ya nyama km 200 , niko tayari kukupa free consultation; nina uzoefu wa 10 yrs sasa nilianza kidogo kidogo lkn nimekuwa naongeza idadi ya kuku wa nyama na mayai na kununua vyakula direct toka viwandani


Mkuu, ubarikiwe sana kwa moyo wako wa kusaidia. naamini consultation yako itanijenga sana. Nakuja PM kaka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom