Kiminyio 01
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 1,353
- 1,933
Wana Jf Wasalaam,
Tukielekea katika kipindi hiki cha kufunga Mwaka pamoja na kusheherekea Christmas & Mwaka Mpya Tuchukue Tahadhari hasa kuhusiana na kundi la vijana wahalifu wanaotembea kwa Makundi (Panya Road)
Update;
-Jana wamefanya Ukabaji Maeneo ya Karakata Airport ,mmoja Kati ya panya road aliuliwa na Wananchi na kuchomwa moto.
Hata hivyo Askari wetu walijitahidi kufanya Doria maeneo mbalimbali Amani ikarejea na Utulivu
-Leo Hadi hivi Sasa Vijana wapatao 15&26 Wanaendelea na Ukabaji wakiwa Ktk kikundi.Wananchi wanakimbizana Ovyo ,Eneo Ni Karakata Mtaa wa Majukumu..
Ukabaji Bado Unaendelea ..
=====
POLISI WAANZA MSAKO WA WEZI WALIOJERUHI WATU CHANIKA
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeanza kuwasaka wahalifu wanaodaiwa kuvamia nyumba zaidi ya 20 zilizopo Chanika na kuwajeruhi watu kwa mapanga kisha kufanya uporaji wa mali na fedha.
===========================
Operesheni yanasa ‘Panya Road’ waliovunja nyumba 23
Kundi la watoto wenye umri kuanzia miaka minane hadi 12 maarufu ‘panya road’ wamepita nyumba kwa nyumba maeneo ya Zingiziwa kata ya Chanika, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakiwa na mapanga na kujeruhi kisha kupora mali na fedha.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, aliyasema hayo jana na kueleza kuwa tukio hilo limetokea Jumapili usiku baada ya kundi hilo kuvamia nyumba 23.
“Vitoto vidogo sitaki kuviita ‘panya buku’, ‘panya road’ vinapita kwenye nyumba za watu kuvunja vioo, kuiba kujeruhi nimeagiza Jeshi la Polisi wafanye operesheni wengi wamekamatwa.
“Niwaase wazazi, Mkuu wa wilaya ulitoa tamko mara baada ya tukio, niwaase wazazi muulize mwanao anaporudi jioni, ulikwenda kufanya kazi gani leo au anaporudi asubuhi ulikuwa wapi na nani, asije akarudi nyumbani na TV akakwambia amebeti, asije akarudi na simu akakwambia amepata kwenye promosheni mwongo.”
Makalla alisema katika msako huo wamekamata simu nyingi, runinga karibu 13 na fedha 1,260,000.
“Watoto wenyewe ni wengi, operesheni iliyofanyika jana (juzi) na leo (jana) wazazi mkawatambue watoto wenu kule, wengi wamekamatwa halafu miaka minane mpaka 12 huyu si bado anasoma, wazazi muwe walinzi wa kwanza wa kuwalinda watoto,” aliagiza.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wawaulize watoto wao shughuli wanazozifanya na wasipokee mali wanazokwenda nazo nyumbani.
Chanzo: Nipashe
Tukielekea katika kipindi hiki cha kufunga Mwaka pamoja na kusheherekea Christmas & Mwaka Mpya Tuchukue Tahadhari hasa kuhusiana na kundi la vijana wahalifu wanaotembea kwa Makundi (Panya Road)
Update;
-Jana wamefanya Ukabaji Maeneo ya Karakata Airport ,mmoja Kati ya panya road aliuliwa na Wananchi na kuchomwa moto.
Hata hivyo Askari wetu walijitahidi kufanya Doria maeneo mbalimbali Amani ikarejea na Utulivu
-Leo Hadi hivi Sasa Vijana wapatao 15&26 Wanaendelea na Ukabaji wakiwa Ktk kikundi.Wananchi wanakimbizana Ovyo ,Eneo Ni Karakata Mtaa wa Majukumu..
Ukabaji Bado Unaendelea ..
=====
POLISI WAANZA MSAKO WA WEZI WALIOJERUHI WATU CHANIKA
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeanza kuwasaka wahalifu wanaodaiwa kuvamia nyumba zaidi ya 20 zilizopo Chanika na kuwajeruhi watu kwa mapanga kisha kufanya uporaji wa mali na fedha.
===========================
Operesheni yanasa ‘Panya Road’ waliovunja nyumba 23
Kundi la watoto wenye umri kuanzia miaka minane hadi 12 maarufu ‘panya road’ wamepita nyumba kwa nyumba maeneo ya Zingiziwa kata ya Chanika, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakiwa na mapanga na kujeruhi kisha kupora mali na fedha.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, aliyasema hayo jana na kueleza kuwa tukio hilo limetokea Jumapili usiku baada ya kundi hilo kuvamia nyumba 23.
“Vitoto vidogo sitaki kuviita ‘panya buku’, ‘panya road’ vinapita kwenye nyumba za watu kuvunja vioo, kuiba kujeruhi nimeagiza Jeshi la Polisi wafanye operesheni wengi wamekamatwa.
“Niwaase wazazi, Mkuu wa wilaya ulitoa tamko mara baada ya tukio, niwaase wazazi muulize mwanao anaporudi jioni, ulikwenda kufanya kazi gani leo au anaporudi asubuhi ulikuwa wapi na nani, asije akarudi nyumbani na TV akakwambia amebeti, asije akarudi na simu akakwambia amepata kwenye promosheni mwongo.”
Makalla alisema katika msako huo wamekamata simu nyingi, runinga karibu 13 na fedha 1,260,000.
“Watoto wenyewe ni wengi, operesheni iliyofanyika jana (juzi) na leo (jana) wazazi mkawatambue watoto wenu kule, wengi wamekamatwa halafu miaka minane mpaka 12 huyu si bado anasoma, wazazi muwe walinzi wa kwanza wa kuwalinda watoto,” aliagiza.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wawaulize watoto wao shughuli wanazozifanya na wasipokee mali wanazokwenda nazo nyumbani.
Chanzo: Nipashe