Panya road azinduka akiwa Mortuary

Panya road azinduka akiwa Mortuary

Kijana maarufu kama Panya Road mwenye umri wa miaka 16 ambaye pia ni mwanafunzi wa kidati cha tatu amezinduka baada ya kuhifadhiwa katika mortuary ya Temeke hospital akidhaniwa amefriki kufuatia kipigo cha wananchi.
Miaka 16 tu tena ni mwanafunzi wa kidato cha tatu! Watu muwe na busara na siyo kushambulia binadamu wenzenu kama wanyama namna hiyo.! HUKO HOSPITALI: Hivi ilishindikanaje kujua kuwa huyu mtu bado yuko hai.?! Kweli vyeti vikaguliwe!
 
wanaume wa dar hamna kitu, yaan mnatishiwa aman na dogo under 18
 
Wazazi leheni watoto wenu kwa kuwasimamia na kuwatetea mnawapa shida walimu hasira zao za mapunjo ya mishahara wanamalizia kwa watoto watukutu kama haoASIE FUNZWA NA MAE HUFUNZWA NA ULIMWENGU
 
waafrica wengi tunafia kwenye mochwari baada ya kufia wodini inashangaza sana mtu eti anatoka mochwari kupelekwa wodini baada ya kutoka wodini kwenda mochwari
 
Yule panya road wa mbeya aliyeshushiwa kibano na mwalimu wamafunzo mkatoka mapovu kama togwa ya dodoki leo mnawaona hawa Taifa jipya heri wauwawe
 
Madaktari wa dar bhana eti wamemruhusu kutoka mortuary ingekuwa tarime wangemlazimisha kubaki mortuary au sio mikuria katili
 
Dar es Salaam. Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Lumo wilayani Temeke, Isack Ernest alionja mauti baada ya kupigwa na wananchi kiasi cha kufikiriwa kwamba amekufa, akapelekwa chumba cha maiti ambako alizinduka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alisema jana kwamba kijana huyo alipigwa hadi kupoteza fahamu na alipofikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke aliwekwa kwenye chumba cha maiti pamoja na kijana mwingine aliyeuawa katika tukio hilo.

“Mwanafunzi huyo hali akiwa amelazwa pamoja na maiti nyingine zinazosubiri kuwekwa katika majokofu, alitikisika kutokana na baridi ya chumba cha maiti, wahudumu wakamwona na kumtoa, wakamvalisha nguo za maiti nyingine, akarudishwa hospitalini kwa ajili ya huduma,” alifafanua Kamanda Muroto.
 
hao paka waliomuwinda panya road inaonekana ni lelemama
 
Back
Top Bottom