Panya road azikwa kifahari Buguruni kisiwani

Panya road azikwa kifahari Buguruni kisiwani

Grader

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2009
Posts
445
Reaction score
65
Nilipewa taarifa tangu wiki iliyopita ya kuwa aliyekuwa muasisi wa panya road Mkoa wa Dar es salaam ambaye amekufa kwa kupigwa risasi Afrika Kusini akiwa anaiba kwenye duka huko Johanesburg . Taarifa zaidi zikaletwa huku Dar nami zikanifikia nikaona nifuatilie kwa karibu kwani hawa panya road walishawahi kutingisha jiji letu japo kwa kiasi fulani wamezibitiwa na jeshi letu la kamanda Kova.

Kikundi cha panya road chenye uongozi thabiti kikatoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumsafilisha mwasisi wao aliyefia bondeni, kijana huyo ana umri wa miaka 30 na jina lake anaitwa HAMISI SEIF alikuwa anakaa Telaviv Buguruni kwa wale wanaojua Buguruni wanatambua eneo korofi kwa uharifu kwa magenge ya walevi, watumiaji wa dawa za kulevya,ukahaba,bangi,ukabaji,wizi na mengine mengi.

Taarifa ikatoka ya kuwa mwili wa marehemu ungewasili Dar ijumaa lakini wakashindwa kupata usafiri badala yake ukawasili leo na shirika la ndege la South Africa Airline na baada ya uchunguzi wa kipolisi ili kuhakiki haukubeba madawa ya kulevya then ulikabidhiwa kwa jamaa hawa kwa mazishi.

Mazishi yalifanyika Buguruni Ghana kwenye makabuli karibu na kwa Mzee maarufu sana Mtaa huo anayeitwa Mzee Shauri (Fundi redio), mazishi hayo yalifanyika kwa mkusanyiko wa vijana wengi sana wa Buguruni na sehemu nyingine za Dar kwa kuletwa na mabasi ya kukodi na bodaboda. Mazishi yalianza saa 2 usiku mpaka 3 usiku.

Kwenye mazishi hayo nimeshuhudia watu wakipora sana watu wanaopita mbele yao na kuzua tahatuki ndani ya muda huo mpaka muda wa mazishi kwisha na hali kurejea kawaida.

Maswali mazito yafuatayo nilitafakari sijayapatia majibu ni mtandao huu bado upo hivi jeshi letu la polisi na usalama wa taifa wapo wapi?, je kikundi hiki kinapata wapi ufadhili?,je sheria iko wapi na taratibu za kuzika muda wa usiku,mbona polisi hawaonyeshi ushirikiano kwenye vitendo vya kudhibiti uharifu pindi wanapotoa taarifa za kiharifu,kwa nini matukio haya yapo sana uswahilini, hivi hawa viongozi wa mitaa wana kazi gani kuhusu kuzuia uharifu kwenye maeneo hayo. Tujadiliane ili tupate suluhisho.

Najua wengi wangependa kuona picha za eneo la tukio lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani simu yangu pamoja na kamera yangu nilifungia ndani ya gari na kupaki Buguruni sheli na nikaenda kuzika kwa ajili ya kuogopa kuporwa.
 
Too sad,maombolezo ya mwemzao,yanaendana na kuwaibia watu.
 
Nilipewa taarifa tangu wiki iliyopita ya kuwa aliyekuwa muasisi wa panya road Mkoa wa dar es salaam ambaye amekufa kwa kupigwa risasi Afrika kusini akiwa anaiba kwenye duka huko johanesburg . Taarifa zaidi zikaletwa huku dar nami zikanifikia nikaona nifuatilie kwa karibu kwani hawa panya road walishawahi kutingisha jiji letu japo kwa kiasi fulani wamezibitiwa na jeshi letu la kamanda kova.
Kikundi cha panya road chenye uongozi thabiti kikatoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumsafilisha mwasisi wao aliyefia bondeni, kijana huyo ana umri wa miaka 30 na jina lake anaitwa HAMISI SEIF alikuwa anakaa telaviv Buguruni kwa wale wanaojua Buguruni wanatambua eneo korofi kwa uharifu kwa magenge ya walevi, watumiaji wa dawa za kulevya,ukahaba,bangi,ukabaji,wizi na mengine mengi.
Taarifa ikatoka ya kuwa mwili wa marehemu ungewasili dar ijumaa lakini wakashindwa kupata usafiri badala yake ukawasili leo na shirika la ndege la south Africa airline na baada ya uchunguzi wa kipolisi ili kuhakiki haukubeba madawa ya kulevya then ulikabidhiwa kwa jamaa hawa kwa mazishi. Mazishi yalifanyika Buguruni ghana kwenye makabuli karibu na kwa Mzee maarufu sana Mtaa huo anayeitwa Mzee shauri(Fundi redio), mazishi hayo yalifanyika kwa mkusanyiko wa vijana wengi sana wa Buguruni na sehemu nyingine za dar kwa kuletwa na mabasi ya kukodi na bodaboda. Mazishi yalianza saa 2 usiku mpaka 3 usiku. Kwenye mazishi hayo nimeshuhudia watu wakipora sana watu wanaopita mbele yao na kuzua tahatuki ndani ya muda huo mpaka muda wa mazishi kwisha na hali kurejea kawaida.
Maswali mazito yafuatayo nilitafakari sijayapatia majibu ni mtandao huu bado upo hivi jeshi letu la polisi na usalama wa taifa wapo wapi?, je kikundi hiki kinapata wapi ufadhili?,je sheria iko wapi na taratibu za kuzika muda wa usiku,mbona polisi hawaonyeshi ushirikiano kwenye vitendo vya kudhibiti uharifu pindi wanapotoa taarifa za kiharifu,kwa nini matukio haya yapo sana uswahilini, hivi hawa viongozi wa mitaa wana kazi gani kuhusu kuzuia uharifu kwenye maeneo hayo. Tujadiliane ili tupate suluhisho. Najua wengi wangependa kuona picha za eneo la tukio lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani simu yangu pamoja na kamera yangu nilifungia ndani ya gari na kupaki Buguruni sheli na nikaenda kuzika kwa ajili ya kuogopa kuporwa.

= uhalifu
= makaburi
= kihalifu

Hongera kwa kwenda kumzika kiongozi wa panya road.
 
Kuna siku nilienda kumzika rafiki yangu wa utotoni ambaye aliuwawa kwenye tukio la ujambazi, polisi walitoa taarifa kuwa jambazi sugu kauliwa,

Siku hiyo niliamini kuwa wahalifu wa dar wana mitandao mikubwa maana waombolezaji walikuwa kama 2000 hivi Kutoka kila Kona ya mji wa dar wote ukiangalia ni vibaka tu.
Mdogo wa marehemu akanitonya kuwa tuondoke haraka kabla ya mazishi kuisha, kumbe walipanga mazishi ya kiisha waanze kupora vitu kwa waombolezaji. Baada ya sheikh kumaliza ibada aliporwa, baba wa marehemu , magari waliiba vifaa , maduka pembeni ya makaburini waliporwa mwisho risasi zikafyatuliwa.
Tulipowataarifu polisi walisema hayo ni matukio ya kawaida kwenye msiba ya wahalifu dar es salaam
 
Kuna siku nilienda kumzika rafiki yangu wa utotoni ambaye aliuwawa kwenye tukio la ujambazi, polisi walitoa taarifa kuwa jambazi sugu kauliwa,

Siku hiyo niliamini kuwa wahalifu wa dar wana mitandao mikubwa maana waombolezaji walikuwa kama 2000 hivi Kutoka kila Kona ya mji wa dar wote ukiangalia ni vibaka tu.
Mdogo wa marehemu akanitonya kuwa tuondoke haraka kabla ya mazishi kuisha, kumbe walipanga mazishi ya kiisha waanze kupora vitu kwa waombolezaji. Baada ya sheikh kumaliza ibada aliporwa, baba wa marehemu , magari waliiba vifaa , maduka pembeni ya makaburini waliporwa mwisho risasi zikafyatuliwa.
Tulipowataarifu polisi walisema hayo ni matukio ya kawaida kwenye msiba ya wahalifu dar es salaam

Bongo movie wanasema scene za kuigiza zimeisha..
 
Bw.Grader ulienda kuzika kama nani?

Soma vizuri habari nzima kuhusiana na panya road. Mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi nafanyia shirika moja la habari la nchi(jina kapuni). Pia ni mtafiti kwenye social & relations matters
 
Hahaaa panya road =boko haram
 
Aisee kama ni hivyo usalama wa raia daima utakuwa mashakani
 
cha ajabu unaweza mkuta huyo panya buku kwenye mkono wa kuume wa bwana alaf nyie mnasukumwa na na fidi fosi wa mungu kuelekea motoni
 
mateja wa unga wakikamatwa baadae uachiwa maana wameshindikanika...

pia ni mtaji kwa police ktk kuchochea uhalifu...
 
Soma vizuri habari nzima kuhusiana na panya road. Mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi nafanyia shirika moja la habari la nchi(jina kapuni). Pia ni mtafiti kwenye social & relations matters

Kumbe? Nilidhani wewe ndio CRO/PRO wao
 
Nilipewa taarifa tangu wiki iliyopita ya kuwa aliyekuwa muasisi wa panya road Mkoa wa dar es salaam ambaye amekufa kwa kupigwa risasi Afrika kusini akiwa anaiba kwenye duka huko johanesburg . Taarifa zaidi zikaletwa huku dar nami zikanifikia nikaona nifuatilie kwa karibu kwani hawa panya road walishawahi kutingisha jiji letu japo kwa kiasi fulani wamezibitiwa na jeshi letu la kamanda kova.

Kikundi cha panya road chenye uongozi thabiti kikatoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumsafilisha mwasisi wao aliyefia bondeni, kijana huyo ana umri wa miaka 30 na jina lake anaitwa HAMISI SEIF alikuwa anakaa telaviv Buguruni kwa wale wanaojua Buguruni wanatambua eneo korofi kwa uharifu kwa magenge ya walevi, watumiaji wa dawa za kulevya,ukahaba,bangi,ukabaji,wizi na mengine mengi.

Taarifa ikatoka ya kuwa mwili wa marehemu ungewasili dar ijumaa lakini wakashindwa kupata usafiri badala yake ukawasili leo na shirika la ndege la south Africa airline na baada ya uchunguzi wa kipolisi ili kuhakiki haukubeba madawa ya kulevya then ulikabidhiwa kwa jamaa hawa kwa mazishi.

Mazishi yalifanyika Buguruni ghana kwenye makabuli karibu na kwa Mzee maarufu sana Mtaa huo anayeitwa Mzee shauri(Fundi redio), mazishi hayo yalifanyika kwa mkusanyiko wa vijana wengi sana wa Buguruni na sehemu nyingine za dar kwa kuletwa na mabasi ya kukodi na bodaboda. Mazishi yalianza saa 2 usiku mpaka 3 usiku.

Kwenye mazishi hayo nimeshuhudia watu wakipora sana watu wanaopita mbele yao na kuzua tahatuki ndani ya muda huo mpaka muda wa mazishi kwisha na hali kurejea kawaida.

Maswali mazito yafuatayo nilitafakari sijayapatia majibu ni mtandao huu bado upo hivi jeshi letu la polisi na usalama wa taifa wapo wapi?, je kikundi hiki kinapata wapi ufadhili?,je sheria iko wapi na taratibu za kuzika muda wa usiku,mbona polisi hawaonyeshi ushirikiano kwenye vitendo vya kudhibiti uharifu pindi wanapotoa taarifa za kiharifu,kwa nini matukio haya yapo sana uswahilini, hivi hawa viongozi wa mitaa wana kazi gani kuhusu kuzuia uharifu kwenye maeneo hayo. Tujadiliane ili tupate suluhisho.

Najua wengi wangependa kuona picha za eneo la tukio lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani simu yangu pamoja na kamera yangu nilifungia ndani ya gari na kupaki Buguruni sheli na nikaenda kuzika kwa ajili ya kuogopa kuporwa.

Sasa USA akitaka gesi ndio huwapa zana za kivita vijana kama hao na kisha anawavisha kanzu na kuwabatiza majina kama IS, BOKO, SHABAB nk. Kijana anayekaba kwa kutumia kisu uje umkabidhi ndinga na mashine si ataona kama kapata nini sijui.na kusini kwetu wataingia kwa gia hiyo hiyo!!.muda utaongea
 
Watu kuporwa ndio ufahari? Nadhani heading ilitakuwa kusomeka Wapita njia waporwa kiongozi wa Panya Road akizikwa
 
Watu kuporwa ndio ufahari? Nadhani heading ilitakuwa kusomeka Wapita njia waporwa kiongozi wa Panya Road akizikwa

Jamaa kama kweli ni muandishi basi uandishi hauna maana yeyote anakuza mambo sana kidaku kabisa. . . . .
1. Hivi South Africa unaenda kwa fedha nyingi sana???!!!
2. Ufahari uko wapi katika hayo mazishi??!!
3. Hajuai hata Kisutu tunazika usiku??!!!

Muandishi hovyo kabisa huyu Grader. . . . . . . ati habari za kiuchunguzi
 
Last edited by a moderator:
Soma vizuri habari nzima kuhusiana na panya road. Mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi nafanyia shirika moja la habari la nchi(jina kapuni). Pia ni mtafiti kwenye social & relations matters
Acha mbwembwe bhana. . . . . . Mtafiti huna supporting data (alisafirishwa kwa kiasi gani??!!) unatumia maneno yanayopimika na huweki scale ili kuthibitisha. . . . .Ufahari unaanzia wapi mpaka wapi na hapo umeupima kwa kipimo gani?????

Spineless reporting. . . . . . .,shirika gani lina waandishi wepesi hivi??!!
 
= uhalifu
= makaburi
= kihalifu

Hongera kwa kwenda kumzika kiongozi wa panya road.
Soma vizuri habari nzima kuhusiana na panya road. Mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi nafanyia shirika moja la habari la nchi(jina kapuni). Pia ni mtafiti kwenye social & relations matters
Huyu ni mwandishi wa habari za kiuchunguzi wa chombo cha habari cha kimataifa, shangaa sasa...
 
Nyerere hawa ndo watafiti uliotuachia... ningekuona ningekushangaa
 
Back
Top Bottom