Pamoja na ushindi mzito wa CCM: Sisi kama Watanzania tunapaswa kutafakari kwa kina juu ya hili

kajekudya

JF-Expert Member
Sep 24, 2015
2,469
4,904
Tanzania ni moja ya Nchi ambayo baada tu ya Uhuru ilifanikiwa kujenga msingi Imara wa kiutawala kupitia TANU na baadae CCM. Msingi ambao unaifanya Tanzania kuwa moja ya Nchi chache Barani Afrika zenye uimara wa hali ya juu kiutawala.

Sasa ni miaka 20 tangu mfumo wa vyama vingi uanze, na hakuna shaka huu ndio mfumo ambao kwa sasa unakubalika Kama mfumo sahihi. Ndani ya miaka hiyo 20 Tanzania tunayo bahati ya kuwa na moja ya vyama bora vya Siasa duniani, CHAMA CHA MAPINDUZI na kupitia Chama hiki tumeendelea kuwa Taifa Madhubuti sana.

Ni bahati Mbaya kuwa ndio Chama pekee chenye mlengo unaoeleweka, Sera zinazoeleweka, Muundo unaoeleweka na kinachoendeshwa kisomi na kwa tafiti. Vyama vingine ni aidha vimejengwa juu ya Migongo ya watu au ni vikundi vya watu wachache ambao wakichuja kisiasa vyama vyao navyo huchuja. Mifano ni Mingi, leo CUF ni Kama imekufa baada ya Maalim Seif kuhamia ACT, CDM hadi leo wanamg'ang'ania Mbowe kwakuwa hawajui hatima yao bila yeye, ACT Kila ukiiangalia unamuona Zitto Zuberi Kabwe, hivyo hivyo kwa NCCR Mageuzi na Mbatia.

Udhaifu huu wa vyama hivi pamoja na kuwa fursa kwa CCM kuendelea kutawala, kwangu naouna kama wenye hatari Sana kwa Mustakabali wa Taifa hili. Lazima tukubaliane si Watanzania wote wanaoukubaliana na Sera za CCM Wala wanaipenda CCM. Mshkaji ninaye kaa naye Mimi haielewi CCM kabisa tarehe 28/10/2020, nilimuamsha asubuhi tukaongozana kwenda kupiga kura, yeye alikwenda kumpigia kura Lissu mimi nikaenda kumpigia kura Magufuli na tuliondoka tukifahamu hilo. Kwenye Group langu la Whataup O level tulikuwa na jamaa mmoja yeye alikuwa amekuwa Kama kichaa kwa Lissu, humwambii chochote, kila sekunde anaposti mpaka Wana group mnakereka. Na Hawa wapo wengi sana.

Ninachotaka kusema watu hawa wanahitaji kupatiwa sehemu ya kupumulia, sehemu hiyo iwe sehemu Madhubuti, inayoeleweka na inayoaminika. Wasiwe watu wa hovyo hovyo au kikundi Cha hovyo hovyo.

CCM pamoja na mambo mengine inaendelea kushinda Uchaguzi kwakuwa inaaminika. Hivo Kama Taifa tunahitaji kupata Chama kingine ambacho kitakuwa Cha Ki taasisi, Chama kinachoendeshwa kiweledi na chenye watu wanaoeleweka na Cha Kizalendo Kama na kiaminike kama kilivyo CCM lakini chenye mlengo tofauti na CCM.

Kuendelea kuwa na vyama dhaifu ndicho kinapelekea kuwa na Wagombea aina ya Lissu, ambao hawajui kwanini wanagombea lakini waliondaliwa ughaibuni na kwakuwa watu wenye mlengo tofauti na CCM hawana sehemu sahihi ya kupeleka machaguo yao wanalazimika kuwafata watu wa aina hiyo.Hivi tumejiuliza inaweza kuwa Inchi ya Namna gani!? Rais Lissu, Makamu Salumu Mwalimu, Mwenyekiti wa Chama Mbowe, Katibu mkuu wa Chama Mnyika, wajumbe wa CC, Halima, Lema, Msigwa, Sugu, Prof Jay, Bulaya na Boniface Jacob.Yes Hawa ndio walikuwa wanatafuta Dora na hakuna shaka kwa kiasi kikubwa walipata uungwaji mkono ni mjinga pekee anaweza kubeza Hilo.Kwa lugha rahisi Hawa ndio walikuwa wanaomba kuliongoza Taifa, Hawa ndio wangekuwa wanatoa maamuzi mazito juu ya Mustakabali wa Taifa.

Sasa ili kuondoa wasiwasi wa kuwa na vyama vinavyojengwa juu ya watu, na kuhatarisha ustawi wa Taifa hasa pale watu watakapoamua kuvichagua baada ya kuichoka CCM, kama Taifa na hasa Kitengo, wafanye uratibu wa kupata Chama kingine Cha Kizalendo na ambacho kitakuwa na mfumo Imara wa kitaasisi na kinachoeleweka ili kiweze kuwa Chama shindani kwa CCM na kiwape Watanzania wasiovutiwa na kukubaliana na Sera za CCM mbadala lakini pia kiwape nafasi Watanzania chaguo pale wanapokuwa wameichoaka CCM, na chaguo Hilo liwe ni Taasisisi inayoaminika na yenye uwezo Kama CCM, ili kuepuka hatari ya kupata mbadala wa aina Lissu ambao kiukweli ni hatari kwa maslahi ya Taifa.

Na kwakuwa sasa tutakuwa na Chama au vyama Mbadala visivyotiliwa shaka, kitaasisi, kimuundo, Kizalendo na kuiuwezo, basi na mfumo mzima wa Uchaguzi ufumuliwe hasa ikiwemo Tume ya Uchaguzi na mfumo mzima wa usajiri wa vyama ili kuondoa minongona na hisia zinazotokana na ground level isiyo na uwiano, na hii itasaidia mtu anaposhindwa akose visingizio na hata akivitoa watu waone havina msingi.

Kwa Sasa hata Chama kingepata kipigo Cha Mbwa Koko Kama walichopata Mwaka huu na ambacho kipo dhahiri na ambacho wengi tulikiona Mapema na kukitarajia bado wakitoa Malalamiko yanaweza yakaonekana yana mantiki. Hadi Uchaguzi unafanyika Rais alikuwa ni Magugufuli na ambaye alikuwa anagombea katika Uchaguzi uliosimamiwa na Tume aliyoichagua yeye, Wakurugenzi, Wakuu wa Mikoa na Wilaya aliowachagua yeye na Majaji aliowaachagua yeye. Hakuna shaka ushindi wa aina yeyote Katika Mazingira haya lazima watu wauhoji. Yaani ni sawa na Simba ya Haji Manara Leo icheze na Buyern Munich na wafungwe Goli 100, lakini Refa wa Kati akiwa ni Mwenyekiti wa Buyern Munich, navibendera wakiwa CEO wa Buyern na Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Ujerumani, Ushindi huo pamoja na tofauti kubwa ya ubora Kati ya timu hizi bado unaweza kuhojiwa.

Kwahiyo sisi Kama Taifa tunayo fursa kwakuwa tayari tunacho Chama kimoja Imara na Madhubuti sana, na ambacho kimefanya tuwe na Taifa Madhubuti. Lakini ukweli unabaki kuwa Watanzania hawawezi kuwa milele wanaichagua CCM, ipo siku wataamua tofauti, hivyo tunao wajibu wa kuhakikisha tunajenga Taasisisi za kisiasa Imara na zinazoaminika ambazo Kama ilivyo CCM zitakuwa na uwezo wa kuliongoza Taifa hili kwa Uzalendo pale Watanzania watakapoamua kuipumuzisha CCM.

Nimevaa ngao
 
Ni mfululizo wa kuteseka kwa wana Ccm baada ya mbereko la mahera kuwafikisha ikulu

Sisi tupo bize tunaanza ujenzi wa ofisi za chama j3
Tatizo la kufikiria kwa kutumia Masaburi. Anyways huwa siandiki kwa ajiri ya Ngedere wa Serengeti!
 
Hapa ni kama unapima upepo. Kwa taarifa yako hao TISS wana mpango wa kuanzisha chama kingine cha upinzani, nje ya cdm. Na hata huu uhayawani uliofanyika hivi sasa ni katika kujaribu kufanikisha hilo. Tatizo ni moja, wanaotaka kuanzisha hicho chama wote ni wanaccm waliopoteza ushawishi kwa umma, na wanataka waanzishe chama chenye mitazamo ya kiccm. 2/3 ya tatu ya watanzania hawajajitokeza kupiga kura, na hiyo 1/3 wote hawajaipa kura ccm, achia mbali uhuni wa wazi uliopelekea ccm kutangazwa washindi. Ni wazi kuwa ccm imechokwa, na hata sasa haishindi, ila wanaweza kupora ushindi kwa kutumia vyombo vya dola, kwani watanzania ni waoga wa kupambania haki zao.

Tatizo ni kuwa wananchi wanachagua watakacho na sio mnachotaka nyie ccm/Tiss. ACT ilikuwa ni moja ya vyama vilivyoanzishwa kwa mlengo huo wa kuiua cdm, lakini haijapata uungwaji mkono. Na hata mkianzisha chama kingine, bado hakitapita uungwaji mkono maana watu wana utashi wao. Ccm inataka ianzishe chama mbadala, huku yenyewe ikiwa haikubaliki, chama mbadala huja automatically na sio chama au taasisi zilizochoka chini ya mfumo wa ccm ndio zianzishe chama mbadala.
 
Hapa ni kama unapima upepo. Kwa taarifa yako hao TISS wana mpango wa kuanzisha chama kingine cha upinzani, nje ya cdm. Na hata huu uhayawani uliofanyika hivi sasa ni katika kujaribu kufanikisha hilo. Tatizo ni moja, wanaotaka kuanzisha hicho chama wote ni wanaccm waliopoteza ushawishi kwa umma, na wanataka waanzishe chama chenye mitazamo ya kiccm. 2/3 ya tatu ya watanzania hawajajitokeza kupiga kura, na hiyo 1/3 wote hawajaipa kura ccm, achia mbali uhuni wa wazi uliopelekea ccm kutangazwa washindi. Ni wazi kuwa ccm imechokwa, na hata sasa haishindi, ila wanaweza kupora ushindi kwa kutumia vyombo vya dola, kwani watanzania ni waoga wa kupambania haki zao.

Tatizo ni kuwa wananchi wanachagua watakacho na sio mnachotaka nyie ccm/Tiss. ACT ilikuwa ni moja ya vyama vilivyoanzishwa kwa mlengo huo wa kuiua cdm, lakini haijapata uungwaji mkono. Na hata mkianzisha chama kingine, bado hakitapita uungwaji mkono maana watu wana utashi wao. Ccm inataka ianzishe chama mbadala, huku yenyewe ikiwa haikubaliki, chama mbadala huja automatically na sio chama au taasisi zilizochoka chini ya mfumo wa ccm ndio zianzishe chama mbadala.
Shukrani kwa kuja na kwa hoja inayoeleweka!
 
Unaanzisha uzi mrefu na maelezo mengi, nikajua unajitambua, unatolewa kidogo kwenye reli unaishia kujibu kwa kupanick, halafu unategemea mawazo yako yaonekana ya maana!
Najielewa Sana. Ila nikiandika vitu vya maana ukaleta upumbavu nami nakujibu upumbavu, hiyo ni principle yangu mhimu Sana, ukitoka tufanyeje arguements za maana tunafanya, ukileta matusi nakurudishia matusi. Simple, every one is handled accodingly!
 
Tulikuwa na mwendelezo walau wenye kuridhisha wa kuijenga demokrasia yetu licha ya mapungufu mengi tu yaliyokuwepo. Zaidi ya miaka 25 ya mfumo wa vyama vingi watu wamekufa, watu wamepotezwa, watu wamepoteza ajira zao n.k katika mapambano ya demokrasia ya nchi yetu kwa hiyo basi hakuna sababu ya kuendelea kuitetea CCM katika uharamia huu uliofanyika eti taasisi imara.
 
Najielewa Sana. Ila nikiandika vitu vya maana ukaleta upumbavu nami nakujibu upumbavu, hiyo ni principle yangu mhimu Sana, ukitoka tufanyeje arguements za maana tunafanya, ukileta matusi nakurudishia matusi. Simple, every one is handled accodingly!

Nikusaidie kitu, ukiwa ww ndio muanzisha mada, na ukaona una hoja ya msingi, hakikisha unazuia hisia zako ili kuitendea haki hoja yako. Ukitaka kujibu kwa jazba subiri hoja ambayo ww sio muhusika. Hapa ni sawa ww ndio bwana harusi, kisha unatoka meza kuu kwenda kuanzisha ugomvi na wageni! Hoja yako ni ya msingi sana, ila unataka kuichafua kwa kuweka vionjo vinavyoweza kuepukika.
 
Tulikuwa na mwendelezo walau wenye kuridhisha wa kuijenga demokrasia yetu licha ya mapungufu mengi tu yaliyokuwepo. Zaidi ya miaka 25 ya mfumo wa vyama vingi watu wamekufa, watu wamepotezwa, watu wamepoteza ajira zao n.k katika mapambano ya demokrasia ya nchi yetu...kwa hiyo basi hakuna sababu ya kuendelea kuitetea CCM katika uharamia huu uliofanyika eti taasisi imara.
Yes ni kweli, lakini mfumo wa Kidemokrasia una njia zake. Hebu nitajie Chama kimoja ukiicha CCM na ambacho shughuli zake zinaendeshwa Kidemokrasia. Tunaweza kufanikiwa Kama tunajenga vyama Taasisisi, siyo hizo Saccos za watu, Saccos ambazo mtu mmoja akichuja na zenyewe zinakufa. Hivi ukiwa na akili zako timamu hapa Tanzania ukiitoa CCM Kuna Chama kingine unaweza ukasimama na ukasema na moyo ukiwa na amani kabisa kuwa kinaweza kabidhiwa Dora na watu mioyo ikaka sehemu yake kuwa mambo yataenda vizuri!
 
Tulikuwa na mwendelezo walau wenye kuridhisha wa kuijenga demokrasia yetu licha ya mapungufu mengi tu yaliyokuwepo. Zaidi ya miaka 25 ya mfumo wa vyama vingi watu wamekufa, watu wamepotezwa, watu wamepoteza ajira zao n.k katika mapambano ya demokrasia ya nchi yetu...kwa hiyo basi hakuna sababu ya kuendelea kuitetea CCM katika uharamia huu uliofanyika eti taasisi imara.

Ccm sio taasisi imara, na huwa nawashangaa watu wanaosema kuwa ccm ni taasisi imara. Ukweli ni kuwa ccm sio chama cha siasa, bali ni kikundi cha dola kulichojivika koti la chama cha siasa. Na ccm imejibanza kwenye Muhimili wa serikali. Kwa sasa chini ya Magufuli ccm ndio imedhihirika kuwa sio taasisi imara, bali inatembelea jeuri ya madaraka ya urais yanayotumika vibaya. Ni ukweli usioacha shaka kuwa Magufuli ni rais mwenye jeuri na kiburi cha madaraka, kutokana na katiba mbovu anaibeba ccm kwa njia haramu na sahihi ili kuifanya ccm ionekane ni imara. Ila wananchi walio wengi wameshalijua hilo, ndio maana watanzania 2/3 wamepuuza uchaguzi huu kwani hawaamini anachoshurutisha watu waamini.
 
Nikusaidie kitu, ukiwa ww ndio muanzisha mada, na ukaona una hoja ya msingi, hakikisha unazuia hisia zako ili kuitendea haki hoja yako. Ukitaka kujibu kwa jazba subiri hoja ambayo ww sio muhusika. Hapa ni sawa ww ndio bwana harusi, kisha unatoka meza kuu kwenda kuanzisha ugomvi na wageni! Hoja yako ni ya msingi sana, ila unataka kuichafua kwa kuweka vionjo vinavyoweza kuepukika.
Huwa siandiki kwa ajiri ya kila mtu Bosi. Humu ndani wapo watu ambao kwa makusudi kazi yao ni kutukana nankuandika vitu visivyotiliwa na kichwa Wala miguu hata Kama umeandika hoja inayoeleweka. So napenda niwape kile wanataka. Full stop. Ukitakuna, natukana, ukijibu ugoro nakurudishia ugoro wako. Unapata unachostahili!
 
Yes ni kweli, lakini mfumo wa Kidemokrasia una njia zake. Hebu nitajie Chama kimoja ukiicha CCM na ambacho shughuli zake zinaendeshwa Kidemokrasia. Tunaweza kufanikiwa Kama tunajenga vyama Taasisisi, siyo hizo Saccos za watu, Saccos ambazo mtu mmoja akichuja na zenyewe zinakufa. Hivi ukiwa na akili zako timamu hapa Tanzania ukiitoa CCM Kuna Chama kingine unaweza ukasimama na ukasema na moyo ukiwa na amani kabisa kuwa kinaweza kabidhiwa Dora na watu mioyo ikaka sehemu yake kuwa mambo yataenda vizuri!
Chadema ni chama mbadala kabisa kwa sera za chama cha Mapinduzi, Kama nchi ni ya kidemokrasia basi maamuzi lazima yabaki kwa wananchi na sio kwa mitizamo ya watu wachache kama wewe.

Sasa labda hebu nisaidie hizo njia za kidemokrasia za kuijenga demokrasia ni zipi.
 
Ccm sio taasisi imara, na huwa nawashangaa watu wanaosema kuwa ccm ni taasisi imara. Ukweli ni kuwa ccm sio chama cha siasa, bali ni kikundi cha dola kulichojivika koti la chama cha siasa. Na ccm imejibanza kwenye Muhimili wa serikali. Kwa sasa chini ya Magufuli ccm ndio imedhihirika kuwa sio taasisi imara, bali inatembelea jeuri ya madaraka ya urais yanayotumika vibaya. Ni ukweli usioacha shaka kuwa Magufuli ni rais mwenye jeuri na kiburi cha madaraka, kutokana na katiba mbovu anaibeba ccm kwa njia haramu na sahihi ili kuifanya ccm ionekane ni imara. Ila wananchi walio wengi wameshalijua hilo, ndio maana watanzania 2/3 wamepuuza uchaguzi huu kwani hawaamini anachoshurutisha watu waamini.
Hakuna Uchaguzi ambao watu wote wanajitokeza Buda. Lakini Kama Kati ya watu M 29 ambao hata hivyo nyie mlikuwa mkipinga kuwa sio takwimu sahihi 12.5 wamemchagu Magufuli, hapa unadhani tatizo nini!? Kati ya vyama 15 ni Chama kimoja tu kimepata kura angau nusu ya wapiga kura wote. Kwa akili yako unadhani nani hakubaliki hapa!?

Magufuli na CCM waliopata kura 12.5M Kati ya 29 au nyie vyama 15 ambao mmeshindwa kufikisha hata kura milioni 3 kwa pamoja!? Kama Chama kimoja kimefanya was kushawishi watu 12.5 wakipigie kura, halafu nyie 15 mmeshindwa kushawishi hata watu 5M kuwapigia kura, unaandamana kusema hapa tuna vyama.

Unaanzaje kubisha kuwa CCM ndicho Chama Taasisisi pekee. Mtaendelea kushindwa hadi hapo mtako kwanza kubali kuwa CCM kimewazidi mbali,.pili mtakapoanza kujenga vyama vyenu kuwa Taasisisi! Hakunaga miujiza, Siasa ni Sayansi Buda
 
Yes ni kweli, lakini mfumo wa Kidemokrasia una njia zake. Hebu nitajie Chama kimoja ukiicha CCM na ambacho shughuli zake zinaendeshwa Kidemokrasia. Tunaweza kufanikiwa Kama tunajenga vyama Taasisisi, siyo hizo Saccos za watu, Saccos ambazo mtu mmoja akichuja na zenyewe zinakufa. Hivi ukiwa na akili zako timamu hapa Tanzania ukiitoa CCM Kuna Chama kingine unaweza ukasimama na ukasema na moyo ukiwa na amani kabisa kuwa kinaweza kabidhiwa Dora na watu mioyo ikaka sehemu yake kuwa mambo yataenda vizuri!

Mtu akitazama hoja yako kwa haraka anaweza kuamini usemacho. Ngoja nitembee kwenye hiyo hoja yako, kwa taarifa yako taasisi yoyote inapata nguvu kutokana na mtu, nikupe mfano mrahisi wa ccm yenyewe. Ccm ilisemekana ni imara wakati wa Nyerere kwa sababu tabia binafsi za Nyerere. Ccm ya Msingi, Mkapa, JK na sasa Magufuli zote zinaendana na hulka na tabia zao binafsi. Kama sio ubovu wa katiba hii inayompa rais mamlaka ya kimungu, basi ccm isingekuwa madarakani kama ilivyo KANU leo. Ccm nchi hii inabebwa na madaraka ya mwenyekiti wake ambaye huwa rais wa nchi.

Hapo Kenya enzi za KANU kuna watu walikuwa wanahadaa wananchi hivi hivi eti kuwa KANU ni imara, na hakuna chama kingine kinaweza kuendesha Kenya. Leo hii KANU ni historia, na Kenya ina uchumi mzuri kuliko sisi tunaoshurutishwa kuongozwa na ccm inayopora uchaguzi na kumwaga damu ya wananchi wake. Kwa mifano hiyo inaonyesha ww ni mmoja ya watu mlio ndani ya box la propaganda za ccm, ndio maana unachoambiwa unadhani ndio. Mtu au chama chochote kinaweza kuongoza nchi, na ikasonga mbele. Zaidi ya asilimia 60 ya watanzania hawana imani, wala hawaitaki ccm, ila matumizi ya vyombo vya dola ndio bado vinaiweka ccm madarakani.
 
Chadema ni chama mbadala kabisa kwa sera za chama cha Mapinduzi, Kama nchi ni ya kidemokrasia basi maamuzi lazima yabaki kwa wananchi na sio kwa mitizamo ya watu wachache kama wewe.
Sasa labda hebu nisaidie hizo njia za kidemokrasia za kuijenga demokrasia ni zipi.
CDM siyo Chama Buda. Nimekutumiss CC yake hapo juu, rudia kuangalia hiyo CDM unayosema ni Chama na utafakari Mara mbili mbili
 
Huwa siandiki kwa ajiri ya kila mtu Bosi. Humu ndani wapo watu ambao kwa makusudi kazi yao ni kutukana nankuandika vitu visivyotiliwa na kichwa Wala miguu hata Kama umeandika hoja inayoeleweka. So napenda niwape kile wanataka. Full stop. Ukitakuna, natukana, ukijibu ugoro nakurudishia ugoro wako. Unapata unachostahili!

Ukiona unajibu kwa jazba kwenye mada iliyoanzishwa kuna mawili, aidha hoja sio yako umepewa uilete, au ni ya kwako lakini una majibu yako mfukoni. Kibinadamu nakuelewa kuwa una haki ya kukasirika, ila sikubaliani na ww kutokana na weledi niliouna kwenye uandishi wako kwenye post namba moja, hata kama post yako naichallange.
 
Mtu akitazama hoja yako kwa haraka anaweza kuamini usemacho. Ngoja nitembee kwenye hiyo hoja yako, kwa taarifa yako taasisi yoyote inapata nguvu kutokana na mtu, nikupe mfano mrahisi wa ccm yenyewe. Ccm ilisemekana ni imara wakati wa Nyerere kwa sababu tabia binafsi za Nyerere. Ccm ya Msingi, Mkapa, JK na sasa Magufuli zote zinaendana na hulka na tabia zao binafsi. Kama sio ubovu wa katiba hii inayompa rais mamlaka ya kimungu, basi ccm isingekuwa madarakani kama ilivyo KANU leo. Ccm nchi hii inabebwa na madaraka ya mwenyekiti wake ambaye huwa rais wa nchi.

Hapo Kenya enzi za KANU kuna watu walikuwa wanahadaa wananchi hivi hivi eti kuwa KANU ni imara, na hakuna chama kingine kinaweza kuendesha Kenya. Leo hii KANU ni historia, na Kenya ina uchumi mzuri kuliko sisi tunaoshurutishwa kuongozwa na ccm inayopora uchaguzi na kumwaga damu ya wananchi wake. Kwa mifano hiyo inaonyesha ww ni mmoja ya watu mlio ndani ya box la propaganda za ccm, ndio maana unachoambiwa unadhani ndio. Mtu au chama chochote kinaweza kuongoza nchi, na ikasonga mbele. Zaidi ya asilimia 60 ya watanzania hawana imani, wala hawaitaki ccm, ila matumizi ya vyombo vya dola ndio bado vinaiweka ccm madarakani.
Ha ha ha unakosea sana unapomzungumzia mfumo wa vyama vingi na kuutolea mfano Kenya. Hivi hujui matatizo ya Kisiasa waliyo Ayo Kenya Tangu hiyo Kanu ianguke. Hivi unajua maana ya Demokrasia!? Au unatania, Kenya nako Kuna Demokrasia Buda. Yaani watu wanaochaguana kwa missingi ya Kabila unaweza ukaa na kusema Kuna Demokrasia teh teh teh, unajua nini hutokea Uchaguzi wa Kenya.

Huo uchumi wa Kenya unaoauzungumzia unajua Nani ameushikiria, hujui Kama Wakenya na Manamba katika Nchi yao.
Ni kweli CCM Mwenyekiti wa Chama ana nguvu na nguvu hiyo inatokana na Chama na Wala siyo mtu. Ndio maana leo JK na Kinana si lolote ndani ya Chama na ilikuwa hivo hivo kwa Mkapa na Mangula badass ya mda wao kuisha.

Magufuli naye baada ya kumaliza mda wake hiyo hali itamkuta, kwanini!? Kwa sababu nguvu yao hutokana na Taasisisi CCM na si haiba yao. Angalia muundo wa CCM na aina ya watu halafu linganisha na CHADEMA.

Mtoe Mbowe na Mtei CHADEMA uone Kama kuna chama hapo, Mtoe Zitto na Maalim kwa Sasa uone unatakiwa na Nini!? mtoe Mbatia NCCR uone Kama halibaki chuma chakavu. Bado hujaelewa ninachomanisha!?

USA nadhani ndilo Taifa ambalo Lina Demokrasia iliyopevuka zaidi juu ya Sayaru hii, pamoja na kuwa na nafasi ya Mgombea binasfi lakini bado wanaamini katika vyama, yes! Wanaamini Rais lazima atokane na Taasisisi Imara na inayoeleweka. Endeleeni kujidanyanga, eti ipo siku atapatikana mtu aishinde CCM. CCM inaweza kushindwa na Taasisisi iliyo Imara pekee!
 
Mtapata taabu sana kutetea uharamia niliofanya!

No more CCM, limebaki genge la watu linaloitisha uchaguzi ili liteke na kuua watu ili kulinda vyeo .

Vyama vya upinzani vingekuwa dhaifu kama unavyojiaminisha, Jiwe wako asingekuwa anatembea na feni kila mahali na alivyo na kiburi asingepiga magoti kulaghai watu kuwa anaomba kura kumbe tayari alishapika matokeo.

Uimara wa vyama upinzani unaoutaka labda na wao watafute magobore ili kujitetea dhidi ya dhuluma za genge la kiharamia linalojiita chama cha siasa (CCM).

Kuteka na kufukuza mawakala wa vyama upinzani nchi nzima na kuelekeza wasimamizi wa vituo vya kupigia kura wajaze matokeo bila kujali kura zilizopigwa bado mnapata ujasiri kuleta propaganda za kijinga namna hii! Hakika nyie ni mashetani afadhali ya Lucifer!

Bado mpaka sasa internet imefungwa mnataka wananchi wasijue mliyotenda na mnayoenda gizani!

Dunia inatoka kwenye ujinga nyie mnataka watu wabaki kuwa wajinga! How come CCM ikawa genge la primitive creatures kwa kiwango cha kutisha hivyo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom