Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,618
- 9,609
Uhuru si zawadi tunayopewa na watawala bali ni haki ya asili ya kila mtu kwa sababu tuliumbwa nayo. NI HAKI YA ASILI!!!
Kiuhalisia tawala za kidunia mara nyingi hulenga katika kupora uhuru huo ili wawatawale watu kama wapendavyo. Lakini hivyo si sawa. Hata Mungu alipowaumba Adamu na Hawa aliwapa uhuru wa kutosha wa kufanya maamuzi na uchaguzi (Mwanzo mlango wa 1 na wa 2).
Ni ubaya na uovu pale tu uhuru huo unapotumika vibaya kwa lengo la kuingilia, kukandamiza na kuhatarisha uhuru na maisha ya wengine. Hii ndio sababu zipo katiba na sheria za nchi huru pamoja na maazimio ya kimataifa vinavyotungwa ili kulinda uhuru huo.
Uhuru wetu ni haki na kipawa cha asili tulichopewa na muumba wetu.
Ni wajibu wako kupambana na yeyote anayejaribu kukunyang'anya uhuru wako ambao ni haki yako ya asili.
Kiuhalisia tawala za kidunia mara nyingi hulenga katika kupora uhuru huo ili wawatawale watu kama wapendavyo. Lakini hivyo si sawa. Hata Mungu alipowaumba Adamu na Hawa aliwapa uhuru wa kutosha wa kufanya maamuzi na uchaguzi (Mwanzo mlango wa 1 na wa 2).
Ni ubaya na uovu pale tu uhuru huo unapotumika vibaya kwa lengo la kuingilia, kukandamiza na kuhatarisha uhuru na maisha ya wengine. Hii ndio sababu zipo katiba na sheria za nchi huru pamoja na maazimio ya kimataifa vinavyotungwa ili kulinda uhuru huo.
Uhuru wetu ni haki na kipawa cha asili tulichopewa na muumba wetu.
Ni wajibu wako kupambana na yeyote anayejaribu kukunyang'anya uhuru wako ambao ni haki yako ya asili.