Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
Wapendwa Mapadri, Mashemasi, Watawa na taifa lote la Mungu, Kristo.
Kwa masikitiko makubwa napenda kuwataarifu juu ya kifo cha Padri wetu mpendwa Ernest Donald Boyo wa Jimbo Kuu la DSM, aliyekuwa Paroko Msaidizi wa Parokia ya Chang'ombe.
Padri Boyo amefariki leo tarehe 10 Februari 2021 saa 1:30 usiku katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa akitibiwa. Taarifa zaidi juu ya taratibu za Mazishi zinapangwa na tutawataarifu. Tumuombee Pumziko la Milele Mbinguni.
ASANTENI.
+ Jude THADDAEUS Ruwa'ichi
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la DSM