SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, amesema kuwa hoja ya Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), kwamba fedha za ujenzi wa barabara ya Chalinze, Segera hadi Tanga, zilianza kutumika kabla ya kuidhinishwa na Bunge, ni ya msingi kutokana na utata wa takwimu uliojitokeza : Selelii, alipopitia kitabu cha miradi ya maendeleoeo kwa mwaka huu wa fedha 2009/2010, ukurasa wa 189, item 4189, inaonyesha kuwa kwa miaka ya nyuma, hakuna fedha zilizotengwa, jambo lililomfanya aamini kuwa matengenezo yanayoendelea hivi sasa yanatokana na fedha zinazoombwa kwa mwaka huu wa fedha na ambazo hazijaidhinishwa na Bunge hili.
Ufafanuzi wa Spika ni kwamba mchakato wa kutengeneza barabara hiyo, ulianza mwaka 2006 na fedha zake jumla ya shilingi bilioni 10.4 ziliidhinishwa na Bunge mwaka 2006/2007, kwa matarajio ya kukamilisha usanifu na kuanza ukarabati wa barabara hiyo. Na kwamba kazi ya ukarabati inayoendelea sasa ,fedha zake ziliidhinishwa na Bunge katika mkutano wa 12 na fedha zilioombwa katika mwaka ujao wa fedha 2009/2010 shilingi 22,844,500,000 ni kwa ajili ya kufanyia ukarabati mkubwa wa barabara hii kwa fedha za DANIDA ambazo ni sh bilioni 17.6 na sh milioni 50 fedha za ndani; na kwamba ukitazama ukurasa husika wa 189, alioutaja Selelii,mradi wa ukarabati wa barabara Chalinze-Segera-Tanga kwa mwaka wa fedha 2007/2008 na 2008/2009, hakuna fedha ziizotengwa ila mwaka huu wafedha 2009/2010, inaonyesha kiasa cha fedha kilichotengwa ni sh 22,844,500,000.
Kwa maelezo ya Spika, utata huu unatokana na mabadiliko ya miundo katika Wizara. Miundo inabadilika ndani ya wizara bila Bunge kutaarifiwa! Na Mheshimiwa Spika, analiona hilo ni jambo la kawaida; analiona si jambo la kuwajibishana, analiona si jambo la kuiambia Serikali imekosea! Na bado anataka aonekane ni Spika wa kasi na viwango!
Kwa uangalifu mkubwa, ili isionekane anaikosoa serikali, Spika alitoa ushauri: Kwa kuwa utata huo unatokana na mabadiliko ya miundo, ni ushauri wangu kuwa ili kuondokana na matatizo kama haya kunapotokea na mabadiliko ya miundo ndani ya wizara, hasa mabadiliko yale yanayohusiana na miradi mikubwa, ni vyema fedha zinazotengwa katika miradi ya aina hiyo, zikabainishwa kwa uwazi zaidi katika vitabu vya bajeti.
Spika, anaogopa nini kuiambia serikali kwamba imekosea? Ni wazi serikali yenyewe inaongozwa na chama chake cha CCM, lakini Spika si wa CCM, hata kama yeye ni Mbunge wa CCM, lakini baada ya kukalia kiti cha spika, yeye ni mali ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; ni wajibu wake kulitendea haki taifa maana yeye anasimamia sauti ya uwakilishi ya taifa zima. Kati ya kazi za Bunge, ni kuisahihisha serikali; kama spika anaogopa kufanya kazi hiyo ni dalili tosha kwamba kazi hiyo iko juu ya uwezo wake!
Kuna maswali mengi ya kuuliza juu ya mwongozo wa Spika: Je kama Selelii, angekuwa ni Mbunge wa upinzani, uamuzi wake ungekuwa kama huu alioutoa? Endapo Selelii angethibitika kusema uongo, alikuwa akikabiliwa na adhabu ya kusimamishwa kuhudhuria mkutano mmoja wa Bunge, kama ilivyotokea mwaka 2007 kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), aliyesimamishwa kuhudhuria mkutano mmoja wa Bunge baada ya Bunge kubaini kuwa alisema uongo kuhusu kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa madini wa Buzwagi nje ya nchi katika mazingira ya rushwa.
Kama Zitto, angekuwa CCM, hapana shaka ujanja ungetumia kusudi Zitto asionekane ana kosa la kulidanganya Bunge na Buzwagi ingeshagiliwa! Kumekuwa na mwelekeo wa Spika Sitta, kuwalinda kwa gharama kubwa wabunge wa CCM na kuikingia kifua serikali. Tuna mifano mingi: Juzi Zitto, aliposema Naibu waziri Sumari, alijibu hovyo hovyo, Spika alimlazimisha kufuta usemi, maana kanuni za Bunge zinazuia lugha ya kuudhi;
lugha hiyo ikitumiwa na wabunge wa CCM hakuna mwongozo wa Spika.
Badala ya kuweka mbele maslahi ya Taifa, Spika anashughulika na Chama chake; anaweka mbele maslahi yake binafsi badala ya kuyatanguliza ya taifa. Ukweli ni kwamba akikilinda Chama chake, na chama chake kitamlinda wakati wa uteuzi kugombea tena kiti cha ubunge na labda kama ana matumaini ya kupanda zaidi, kuwa mwenyekiti wa Chama chake au kugombea urais. Hivyo kwa mtizamo wa kina, msimamo wake wa kukilinda chama na serikali una manufaa zaidi kwake kuliko kitu kingine kile. Spika wa namna hii si bora kwa Bunge la wananchi!
Swali jingine ni je kwanini imechukua siku nyingi Serikali kutoa jibu. Mbunge Selelii, aliuliza swali tarehe 15.6.2009 jibu limepatikana tarehe 30.6.2009, kama tatizo lilikuwa ni kukosea takwimu kwanini ichukue siku zote hizo? Takwimu zote zinakuwa kwenye kompyuta, ni kiasi cha kubofya na kufanya masahihisho.
Inawezeka Serikali imechelewa katika harakati za kujipanga kuandaa jibu? Kama barabara hii bado ina masalio ya fedha, ambazo tunaaminishwa kwamba ndo zinatumika hivi sasa kabla Bunge halijabariki matumizi ya mwaka 2009/2010; kwanini zitengwe tena fedha kwa barabara hii? Nafikiri hili ndilo swali la mheshimiwa Selelii na ndilo swali la Watanzania. Bila kuwa makini kwenye bajeti ni kuliangamiza taifa letu. Fedha zitatengwa na kuishia kwenye mifuko ya watu au kuelekezwa kwenye uchaguzi wa 2010.
Na je kama kweli kulikuwa na kosa la takwimu, kwanini alione Selelii, peke yake? Alipata taarifa mapema? Inawezekana kwenye wizara hiyo kuna vijana wanaochukia ufisadi na kuamua kuvujisha habari hizo kwa Mbunge anayeweza kusimama na kupinga ufisadi? Selelii, ni kati ya wabunge watano wa CCM, wanaoaminika kusema bila kuogopa, jimbo lake ni kati ya yale yaliyotangazwa kuwa wazi na gazeti mojawapo hapa nchini hadi Mheshimiwa Anna Kilango Malecela, akapiga kelele.
Au Selelii ndiye mbunge makini peke yake ndani ya bunge? Yeye, alikuwa na maslahi gani kufuatilia takwimu za barabara. Inawezekana wabunge wengine waliziona kasoro hizo wakamezea au hawakuwa na muda wa kupekuwa bajeti ukurasa hadi mwingine? Inawezekana hata takwimu za wizara nyingine zina makosa, kwa vile wabunge hawazichunguzi kwa makini zinapita hivyo hivyo?
Je, kama si Mheshimiwa Selelii, takwimu hizi zingesahihishwa lini? Au kosa hili halina athari kwenye bajeti na utendaji mzima wa kujenga Barabara, si ya Chalinze peke yake, bali hata na barabara nyingine? Kwa vyovyote vile, kama Mheshimiwa Selelii, yuko sahihi, basi serikali ina makosa. Haiwezekani serikali kuandaa bajeti yenye makosa: Hata kama makosa hayo yameandaliwa kwa makusidi mazima, kwa lengo la kuingiza kwenye bajeti fedha zinazoelea tu bila kuwa na lengo maalum ili zichotwe kiulaini, bado ni kosa kubwa maana huo ni udanganyifu na uhujumu uchumi.
CHANZO: kwanzajamii.com
Ufafanuzi wa Spika ni kwamba mchakato wa kutengeneza barabara hiyo, ulianza mwaka 2006 na fedha zake jumla ya shilingi bilioni 10.4 ziliidhinishwa na Bunge mwaka 2006/2007, kwa matarajio ya kukamilisha usanifu na kuanza ukarabati wa barabara hiyo. Na kwamba kazi ya ukarabati inayoendelea sasa ,fedha zake ziliidhinishwa na Bunge katika mkutano wa 12 na fedha zilioombwa katika mwaka ujao wa fedha 2009/2010 shilingi 22,844,500,000 ni kwa ajili ya kufanyia ukarabati mkubwa wa barabara hii kwa fedha za DANIDA ambazo ni sh bilioni 17.6 na sh milioni 50 fedha za ndani; na kwamba ukitazama ukurasa husika wa 189, alioutaja Selelii,mradi wa ukarabati wa barabara Chalinze-Segera-Tanga kwa mwaka wa fedha 2007/2008 na 2008/2009, hakuna fedha ziizotengwa ila mwaka huu wafedha 2009/2010, inaonyesha kiasa cha fedha kilichotengwa ni sh 22,844,500,000.
Kwa maelezo ya Spika, utata huu unatokana na mabadiliko ya miundo katika Wizara. Miundo inabadilika ndani ya wizara bila Bunge kutaarifiwa! Na Mheshimiwa Spika, analiona hilo ni jambo la kawaida; analiona si jambo la kuwajibishana, analiona si jambo la kuiambia Serikali imekosea! Na bado anataka aonekane ni Spika wa kasi na viwango!
Kwa uangalifu mkubwa, ili isionekane anaikosoa serikali, Spika alitoa ushauri: Kwa kuwa utata huo unatokana na mabadiliko ya miundo, ni ushauri wangu kuwa ili kuondokana na matatizo kama haya kunapotokea na mabadiliko ya miundo ndani ya wizara, hasa mabadiliko yale yanayohusiana na miradi mikubwa, ni vyema fedha zinazotengwa katika miradi ya aina hiyo, zikabainishwa kwa uwazi zaidi katika vitabu vya bajeti.
Spika, anaogopa nini kuiambia serikali kwamba imekosea? Ni wazi serikali yenyewe inaongozwa na chama chake cha CCM, lakini Spika si wa CCM, hata kama yeye ni Mbunge wa CCM, lakini baada ya kukalia kiti cha spika, yeye ni mali ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; ni wajibu wake kulitendea haki taifa maana yeye anasimamia sauti ya uwakilishi ya taifa zima. Kati ya kazi za Bunge, ni kuisahihisha serikali; kama spika anaogopa kufanya kazi hiyo ni dalili tosha kwamba kazi hiyo iko juu ya uwezo wake!
Kuna maswali mengi ya kuuliza juu ya mwongozo wa Spika: Je kama Selelii, angekuwa ni Mbunge wa upinzani, uamuzi wake ungekuwa kama huu alioutoa? Endapo Selelii angethibitika kusema uongo, alikuwa akikabiliwa na adhabu ya kusimamishwa kuhudhuria mkutano mmoja wa Bunge, kama ilivyotokea mwaka 2007 kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), aliyesimamishwa kuhudhuria mkutano mmoja wa Bunge baada ya Bunge kubaini kuwa alisema uongo kuhusu kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa madini wa Buzwagi nje ya nchi katika mazingira ya rushwa.
Kama Zitto, angekuwa CCM, hapana shaka ujanja ungetumia kusudi Zitto asionekane ana kosa la kulidanganya Bunge na Buzwagi ingeshagiliwa! Kumekuwa na mwelekeo wa Spika Sitta, kuwalinda kwa gharama kubwa wabunge wa CCM na kuikingia kifua serikali. Tuna mifano mingi: Juzi Zitto, aliposema Naibu waziri Sumari, alijibu hovyo hovyo, Spika alimlazimisha kufuta usemi, maana kanuni za Bunge zinazuia lugha ya kuudhi;
lugha hiyo ikitumiwa na wabunge wa CCM hakuna mwongozo wa Spika.
Badala ya kuweka mbele maslahi ya Taifa, Spika anashughulika na Chama chake; anaweka mbele maslahi yake binafsi badala ya kuyatanguliza ya taifa. Ukweli ni kwamba akikilinda Chama chake, na chama chake kitamlinda wakati wa uteuzi kugombea tena kiti cha ubunge na labda kama ana matumaini ya kupanda zaidi, kuwa mwenyekiti wa Chama chake au kugombea urais. Hivyo kwa mtizamo wa kina, msimamo wake wa kukilinda chama na serikali una manufaa zaidi kwake kuliko kitu kingine kile. Spika wa namna hii si bora kwa Bunge la wananchi!
Swali jingine ni je kwanini imechukua siku nyingi Serikali kutoa jibu. Mbunge Selelii, aliuliza swali tarehe 15.6.2009 jibu limepatikana tarehe 30.6.2009, kama tatizo lilikuwa ni kukosea takwimu kwanini ichukue siku zote hizo? Takwimu zote zinakuwa kwenye kompyuta, ni kiasi cha kubofya na kufanya masahihisho.
Inawezeka Serikali imechelewa katika harakati za kujipanga kuandaa jibu? Kama barabara hii bado ina masalio ya fedha, ambazo tunaaminishwa kwamba ndo zinatumika hivi sasa kabla Bunge halijabariki matumizi ya mwaka 2009/2010; kwanini zitengwe tena fedha kwa barabara hii? Nafikiri hili ndilo swali la mheshimiwa Selelii na ndilo swali la Watanzania. Bila kuwa makini kwenye bajeti ni kuliangamiza taifa letu. Fedha zitatengwa na kuishia kwenye mifuko ya watu au kuelekezwa kwenye uchaguzi wa 2010.
Na je kama kweli kulikuwa na kosa la takwimu, kwanini alione Selelii, peke yake? Alipata taarifa mapema? Inawezekana kwenye wizara hiyo kuna vijana wanaochukia ufisadi na kuamua kuvujisha habari hizo kwa Mbunge anayeweza kusimama na kupinga ufisadi? Selelii, ni kati ya wabunge watano wa CCM, wanaoaminika kusema bila kuogopa, jimbo lake ni kati ya yale yaliyotangazwa kuwa wazi na gazeti mojawapo hapa nchini hadi Mheshimiwa Anna Kilango Malecela, akapiga kelele.
Au Selelii ndiye mbunge makini peke yake ndani ya bunge? Yeye, alikuwa na maslahi gani kufuatilia takwimu za barabara. Inawezekana wabunge wengine waliziona kasoro hizo wakamezea au hawakuwa na muda wa kupekuwa bajeti ukurasa hadi mwingine? Inawezekana hata takwimu za wizara nyingine zina makosa, kwa vile wabunge hawazichunguzi kwa makini zinapita hivyo hivyo?
Je, kama si Mheshimiwa Selelii, takwimu hizi zingesahihishwa lini? Au kosa hili halina athari kwenye bajeti na utendaji mzima wa kujenga Barabara, si ya Chalinze peke yake, bali hata na barabara nyingine? Kwa vyovyote vile, kama Mheshimiwa Selelii, yuko sahihi, basi serikali ina makosa. Haiwezekani serikali kuandaa bajeti yenye makosa: Hata kama makosa hayo yameandaliwa kwa makusidi mazima, kwa lengo la kuingiza kwenye bajeti fedha zinazoelea tu bila kuwa na lengo maalum ili zichotwe kiulaini, bado ni kosa kubwa maana huo ni udanganyifu na uhujumu uchumi.
CHANZO: kwanzajamii.com