Oyaa!! - Usionyeshe Salary Slip Yako!

Kama kweli umeoa mke wa kukaa naye na siyo kwamba mna mkataba wa muda ni muhimu sana yeye kujua vyanzo vya mapato yako. Kumbukeni uwazi na mwasiliano mazuri ndani ya nyumba ni mojawapo ya mambo muhimu yanayofanya nyumba kusimama.

Ninamshukuru Mungu katika hili ametuponya mimi na mke wangu. Nina faili nyumbani ambalo lina nakala zote za mikataba yangu ya ajira toka nilipoanza kuajiriwa na humo ndani ndimo tunaweka salary slips. Kila mmoja wetu ana acess na faili hilo kwa hiyo mimi najua mshahara wake na yeye anajua mshahara wangu.

Kwa wale wenye kuhofu kuwa akijua mshahara wako atazipangia bajeti mpaka ziishe nadhani siyo , kama kweli mnakaa na kukubaliana matumizi yaweje. Ni ninyi wawili mnaopaswa kukaa na kukubaliana bajeti ya mwaka, mwezi, wiki na ikiwezekana hata siku iweje.

Wanaume naomba msiwafiche wake zenu mishahara yenu kwa hofu kuwa watamaliza fedha, amua kumshirikisha na uone ana hekima ya namna gani katika kushauri suala zima la bajeti na matumizi. Ukiona hekima yake ni ndogo unachoweza kufanya ni kusimamia wewe bajeti nzima na kumuacha yeye ni mtekelezaji lakini akiwa anajua unapata kiasi gani. Naamini hii itasaidia kuifanya ndoa yenu isimame vizuri.
 
Kama kweli unampenda mwenzi wako kwa dhati, na hukulazimishwa na mtu yeyote kumpenda; BASI una kila sababu ya kumwonyesha salary-slip yako na marupurupu mengine pia.......

UTAKE USITAKE, HABARI NDO HIYOOOO!!!!!!!

Sio slip tu; mie hata deal zangu nyingine anazijua! mie nikijua kuna deal naifuatilia huwa nashare na wife na hata tunapeana ushauri!

Hivi kwanini umfiche? kumficha ni kutomwamini na kutomwamini kwako maana yake wewe mwenyewe hujiamini na simsafi!

Kuna kuugua ghafla na hata kufa; sasa mwenzio asipojua utakuwa umepata faida gani na hebu utueleze hapa kama una mke na mnafamilia unahangaika kutafuta kwa ajili ya nani ikiwa utamficha mkeo?
 
Binafsi si mwajiriwa, hivyo sina salary slip. Lakini mwisho wa mwezi tunakaa na wife ambaye ndiye mshauri wangu mkubwa, tunaangalia makadirio yalivyokuwa na faida tuliyopata. Pamoja na hilo, si kazi zote nazofanya lazima niripoti kwa mke wangu pamoja na pesa iliyokuwa involved pamoja na faida, ananifahamu vizuri, kazi zingine huwa anajua ni "kazi" tu, hana haja ya kuuliza, na wala huwa haulizi.Matumizi yote lazima nijue ulazima wake, nikiona vp namwambia "nimefulia mammii"
 
Binamu nikajua hiyo Heading ..unatuandikia masela wako tetetetetehh
Nikirudi kwenye mada ..ukiamua kuoa na kuolewa mambo ya siri hayatakiwi kuwa siri tena mmeshakuwa mwili mmoja .
Kwa nini ufanye mambo yako kwa kificho????
 
Haya mambo ya usiri ndo yanayoharibu ndoa haya, mtabaki daily mnalalamika oooh sijui wife kafanya hivi, kumbe vitu vingine humshirikishi anajiona km outsiders, mshirikishe mwenza wako atajiona yeye ni mhusika halisi kwenye family na sio kila kitu unafanya wewe tu. Mwonyeshe kipato chako ajue ukomo wa matumizi/demand zake, tena mwanamke akishajua hivyo ni rahisi sana ku control bajeti ya nyumba yenu.
 
Inategemea mazingira mlio jenga kati ya wewe na mkee wako kama niya kukomoana basi matatizo kama hayo itakiwa ni ya kawaida kwenu. Unatakiwa uwe mkweli kwenye mambo kama hayo ndiyo mapenzi yenu yata dumu..
 
Sioni sababu ya kufichana salary, mi na hubby wangu kila mtu anajua mwenzie anapata nn! ni vyema mwenzi wako akajua unapata nn lakini sizungumzii vimada only wife na husband.kujua mapato yenu inasaidia pia kuweza kupanga mipango ya kimaendeleo, na inaleta kuelewana pia.
 
Kama kweli unampenda mwenzi wako kwa dhati, na hukulazimishwa na mtu yeyote kumpenda; BASI una kila sababu ya kumwonyesha salary-slip yako na marupurupu mengine pia.......

UTAKE USITAKE, HABARI NDO HIYOOOO!!!!!!!

Bado hayajakukuta.. Wewe ndio utakuwa wa kwanza kuficha na kuwashauri wengine wasioneshe...
 
hivi shori wako akijua salary yako tatizo liko wapi? mie shori akiwa ananikamua mijihela ndio nasikia raha......

Hata mimi aisee,yaani kama shori ananipiga mizinga najiona very secure na mali zangu kuliko yule anaejitia kila kitu anafanya mwenyewe.
 
Mi sioni umuhimu wa kuficha, pia si mume tu, bali yeyote yule, sioni point ya kumficha mtu yeyopte yule anayetaka kujua napata ngapi.
 
Mi sioni umuhimu wa kuficha, pia si mume tu, bali yeyote yule, sioni point ya kumficha mtu yeyopte yule anayetaka kujua napata ngapi.

wapata ngapi carmel?......(hapa sidhani kama nitapata jibu)
 
Kwani kosa liko wapi? kama katika kuapa katika siku ya ndoa yenu kuwa UTAMPENDA WAKATI WA SHIDA NA RAHA. Sasa kama mtu alidiriki kusema maneno hayo mbele ya kiongozi wa dini yake, kwanini leo hii asimwonyeshe 'salary slip?'Ambao hawawaonyeshi wake zao salary slip jua hao ni hawana upendo wa dhati ndani ya mioyo yao. juu ya mke wake.
 
Bado hayajakukuta.. Wewe ndio utakuwa wa kwanza kuficha na kuwashauri wengine wasioneshe...


Well utatusidia ukitusimulia yaliyokukuta! Na kama yamekukuta kwa sababu hii basi hiyo ni tabia mbaya tu ya mtu! Kimsingi ndio maana anitwa mwenzi wako!
 
Back
Top Bottom