Entrepreneur
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 1,087
- 620
Ndugu zangu,
Wakati wa kampeni za uchaguzi ni wakati muhimu sana katika jamii yoyote. Ni wakati muhimu kwa sababu jamii husika hujiandaa kuchagua viongozi wao wa kuwaweka mstari wa mbele (frontline) katika kukabiliana na changamoto za kimaisha iwe kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Ni wakati muhimu kwa wananchi kusikiliza sera za wagombea na kupembua mchele katikati ya pumba, ni wakati wa kutafuta dhahabu katikati vipande vya chupa. Je haya ndio yanayoendelea huko ARUMERU?
Tunashuhudia tambo za kila aina! matusi ya kila aina! (hata mbele za watoto) badala ya Sera, Sera zitakazomkomboa mwana wa Arumeru Mashariki. Ndugu zangu, Taifa hili limejengwa katika misingi ya kuheshimu UTU WA MWANADAMU, (Dignity of Man). Je ni nani kati ya hawa wanasiasa waliopo huko ARUMERU anaweza akasimama na kusema anafanya siasa zinazoheshimu UTU? Kwa siasa hizi tutafika wapi?
Inasemekana kuwa SIASA ni UCHUMI, na uchumi wetu ndio huo tena unazidi kuporomoka, hivyo basi ni vyema hawa wanasiasa walio mstari wa mbele watupatie HOJA zao na si VIOJA vyao, watupe SERA zao na si SIRI zao, ili wananchi wajue dhahabu ni ipi na chupa ni zipi, wajue Mchele ni Upi na makapi ni yapi. Sasa kama leo wanafanya SIASA za namna hii (visasi,kuchafuana,chuki,udanganyifu,matusi, ..) tena kwenye ngazi ya Jimbo tu, je kesho watafanya siasa za namna gani?
Ewe mwanaJF, mpenda mabadiliko, tena usiyevutiwa na mtindo huu wa siasa za kupakana matope ungana nami kuwataka wanasiasa wetu wafanye siasa safi.
Ewe mwananchi unajua nguvu ulizonazo? Tusikubali kikundi cha wanasiasa wachache na wafuasi wao watuharibie mfumo wetu wa maisha
Wakati wa kampeni za uchaguzi ni wakati muhimu sana katika jamii yoyote. Ni wakati muhimu kwa sababu jamii husika hujiandaa kuchagua viongozi wao wa kuwaweka mstari wa mbele (frontline) katika kukabiliana na changamoto za kimaisha iwe kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Ni wakati muhimu kwa wananchi kusikiliza sera za wagombea na kupembua mchele katikati ya pumba, ni wakati wa kutafuta dhahabu katikati vipande vya chupa. Je haya ndio yanayoendelea huko ARUMERU?
Tunashuhudia tambo za kila aina! matusi ya kila aina! (hata mbele za watoto) badala ya Sera, Sera zitakazomkomboa mwana wa Arumeru Mashariki. Ndugu zangu, Taifa hili limejengwa katika misingi ya kuheshimu UTU WA MWANADAMU, (Dignity of Man). Je ni nani kati ya hawa wanasiasa waliopo huko ARUMERU anaweza akasimama na kusema anafanya siasa zinazoheshimu UTU? Kwa siasa hizi tutafika wapi?
Inasemekana kuwa SIASA ni UCHUMI, na uchumi wetu ndio huo tena unazidi kuporomoka, hivyo basi ni vyema hawa wanasiasa walio mstari wa mbele watupatie HOJA zao na si VIOJA vyao, watupe SERA zao na si SIRI zao, ili wananchi wajue dhahabu ni ipi na chupa ni zipi, wajue Mchele ni Upi na makapi ni yapi. Sasa kama leo wanafanya SIASA za namna hii (visasi,kuchafuana,chuki,udanganyifu,matusi, ..) tena kwenye ngazi ya Jimbo tu, je kesho watafanya siasa za namna gani?
Ewe mwanaJF, mpenda mabadiliko, tena usiyevutiwa na mtindo huu wa siasa za kupakana matope ungana nami kuwataka wanasiasa wetu wafanye siasa safi.
Ewe mwananchi unajua nguvu ulizonazo? Tusikubali kikundi cha wanasiasa wachache na wafuasi wao watuharibie mfumo wetu wa maisha