Our eternal ambassadors

..Balozi Elly Mtango alikuwa balozi Geneva, halafu akarudishwa nyumbani na Mzee Mwinyi kuwa PS wizara ya habari. Mzee Mkapa akamteua kuwa PS Mambo ya Nje. Baada ya hapo akateuliwa tena kuwa Balozi Japan.

..Balozi Hassani Kibelloh ndiye aliyempokea Elly Mtango U-PS pale Mambo ya Nje. Wakati Mtango anakwenda Japan, Raisi Mkapa alimteua Dr.Ben Moses na Charles Sanga kuwa Ubalozi.Siyo kweli kwamba Balozi Mtango amekaa Japani miaka 16!

..Mabalozi waliokaa nje muda mrefu ni wa aina ya Gen.Sarakikya, Lt.Gen.Mwakalindile na Lt.Gen.Silas Mayunga "mti mkavu." Hawa ukiwarudisha nyumbani bila kuwastaafisha Jeshi watawasumbua watu kama Waitara,Mwamunyange,na Shimbo.

..Mabalozi wanabadilika siku hizi. Mkapa alipoingia madarakani aliteua Mabalozi kama watano kama wakuu wa idara wizarani. Kituo kama Harare wali-serve Muganda na baadaye Mbita. UN alimbadilisha Mwakawago na Mahiga. India alikwenda Capt.Kiwanuka, halafu baadaye Mama Nzaro. London alipelekwa Prof.Abdul-Kadiri badala ya Col.Mchumo. Hata itifaki alianza na Mwawado, akaja Opanga, akamaliza na Cisco Mtiro.

..Hiyo ni mifano michache tu...Lusekelo amekosea kuzungumzia kiujumla-jumla, bila data, suala kama hili.

Nafikiri swala siyo kwa mabalozi wenyewe ila wale wanaoitwa maofisa wa ubalozi; hawa ndio wanaokaa muda mrefu sana.
 
..kama sikosei mtango amekuwa balozi japan toka 2000 au 2001

- mabalozi wengi aliowachagua mkapa ni kwenda kuchukua nafasi za waliostaafu. mwishoni mwa kipindi chake ndio aliwachagua baadhi ya mabalozi wakurugenzi makao makuu nadhani ni timu ya akina cisco, mombo, kallage

- mabalozi waliotoka jeshini nadhani wengi wao waliteuliwa toka awamu ya kwanza. jokakuu amewataja, pia kanali (mstaafu) mchumo alichaguliwa kipindi hichohicho.

- mwakawago ni baadhi tu ya mabalozi waliobadilishwa mwishoni mwa kipindi cha mkapa

- kama sikosei prof. abdukadir aliteuliwa na mzee mwinyi na sio mkapa

nadhani lusekelo angesaidia sana kama angesema ni kipindi gani anazungumzia.

wizara/idara nyingi tu za serikali, wizara ya mambo ya nje ni moja wapo, zina watendaji ambao sio waadilifu lakini sidhani ni vyema kuzihukumu wizara/idara hizo kijumla jumla.

kweli ni jukumu la serikali kuwakwamua raia wake wanapokwama nje ya nchi lakini kukwama huko inabidi kuelezeka na kwa bahati mbaya kutokana na hali ya kiuchumi balozi hazina fungu maalum kwa ajili ya huduma hiyo. hivyo mtu akikwama ubalozi unaweza msaidia kwa kuwasiliana na ndugu zake wamtumie pesa au kuomba pesa makao makuu kwa ajili ya kumkwamua raia huyo. swali wakati msaada huo unangojewa huyo raia anaishije? hapo ndo wanajitokeza raia wema kama fmes au maafisa wa ubalozi na kutoa msaada lakini utakuta raia aliyesaidiwa anaona ni haki yake kusaidiwa na wala hao waliomsaidia hawajatenda utu. hata akikopeshwa pesa harudishi sasa kwa kufanya hivyo ndo anakuwa kishawapaka shombo wengine watakao kwama
 
..by the way yuko Balozi.Maj.General Martin Mwakalindile. Nina imani ame-serve zaidi ya miaka 10. Huyu alikuwa Chief of Staff mara baada ya vita vya Kagera. Kama hajastaafu jeshi basi inakuwa vigumu sana kumrudisha nyumbani.

Mkuu Jokakuu ni Kweli Mzee Mwakalindile alikaa Ubalozi wetu Msumbiji kama Balozi kwa muda wa Miaka 15,aliteuliwa kuwa Balozi huko mara baada ya kuacha kazi ya Army Chief of Staff mwaka 1988 ambayo alikaa kwa miaka 6 (1982 - 1988).Major General Martin Mwakalindile alikuwa Balozi Msumbiji toka mwaka 1988 -2003 alipohamishiwa Rwanda ambako amekaa mpaka 2006 alipostaafu Utumishi serikalini/ Jeshini na kurudi kwao Mwakaleli- Rungwe.

Kabla ya kuwa Balozi huko Msumbiji,Maj Mwakalindile aliwahi kuwepo Msumbiji kabla ya Uhuru kwa maombi rasmi ya Hayati Machel,alikuwa ni mmoja wa Askari wetu waliofundisha viongozi wa jeshi la Frelimo,Baada ya uhuru wa Msumbiji 1975,Maj Mwakalindile alikuwa mmoja wa walioanzisha Ubalozi wetu huko Maputo akiwa kama Muambata wa kijeshi chini ya Balozi Marehemu Katikaza.
 
mwawado, asante kwa historia hiyo.. na pia jokakuu nashukuru.. maana kuna mambo mnayomwaga hapa hayamo vitabuni! kudos
 
Kumbe kuna aliyekaaa miaka 15. Adam kakosea wapi? kuna tofauti ya miaka 15 na 16 kweli jamani?, YES ipo, lakini ina worth kusema habari nzima haina maana?
 
I used to be a regular on Adam's column "With a light touch" in late 70s up to late 80s; other popular columnists of the time included Freddy Macha with his "Cultural Images" and Agoro Anduru with his "A Short Story with Agoro Anduru." I understood Adam as a person who identifies problems in the system and generically writes about them to raise public awareness. In his writing he uses a vulgar language without providing specifics of his subject. Despite this lack of specifics, readres would easily get the message. I took this as a writing syle and I had no problem with it. I guess this sytle may have its roots in Professor Penina Mrama's Drama Group to which Lusekelo was a member.

The article copied above still reflects his "trade mark" writing style, and I clearly get his message: there is no time limit for our diplomats. Their tenure in a foreign country depends on the boss at the Ministry and at State House.
All I see as Lusekelo's mistake is in his choice of the journal. Such article should have appeared in a regular newspaper instead of this investigative newspaper.

U have said it all!

Asante sana, mengine ni uongo dhidi ya Adam.

Asante tena Mwalimu, ndio maana ukawa mwalimu. Hivi mwanafunzi wako NUNGWI amepotelea wapi?
 
I use to Trust Lusekelo sana na kwangu ni mmoja wa watu ambao nilikuwa napenda kusoma makala zao.
But i think on this one, Mr Lusekelo alitakiwa ku control Temper yake!!! Naona aliandika kwa ghadhabu either kuna kilichomtokea au kuna namna. Binafsi nashawishiki hata kudhani labda hii makala ilikuwa imemlenga mtu, unaposema....

"...As I said embassies are places for friends, embarrassing buddies, girlfriends and other unqualified guys...."

Umewakosea Waheshimiwa Mabalozi kwa kiasi fulani, any way sijui kila mmoja ana njia yake ya kuelewa jambo!!
 
Pope,

Kama unasoma makala zake, ndio njia yake ya kuwakilisha jambo. Ana jumuisha, hawi specific hata kidogo. Halengi mtu analenga watu. Kama mtu akitukana ma GAY wote wakati wewe umesimama ndani ya kundi la ma GAY, akasema nyinyi Ma GAY mnafanywa hivi au vile... UNAKASIRIKIA NINI WAKATI WEWE SIO Gay?
 
lakini mzuri kuliko wote kati ya mabalozi wetu wanawake ni bi Mwanaidi Mjaar, aliopo London..duh!
 
I have always admired Adam since my boyhood and even now I never miss his three times weekly articles in the Daily News(Weds),Sunday News and ThisDay.To understand his articles you must be aware that he tries to make it sound like a joke but there is seriousness underlying in the message.What he wanted to convey here was that the ambassadors stays just too long in their work stations unlike other countries.You can mirror this with ambassadors sent to TZ by other countries.They hardly stay more than 4 years.Trying yto judge his style of writting may not be appropriate unless you are the type of ambassador reffered here(no hard feeling)
 
Just like Muhidini Issa Michuzi, Lusekelo is another mediocre journalist from "DAILY NEWS" . His opinions are crap, absive rude, nasty sick and twisted of the first order.

But then again this idiot is just exercising his freedom of speech

You remind me of my Investigative Reporting class. We hated mediocre journalists. This was meant to be an investigative story. So Interview some credible sources,check and cross check facts,dig,find out information. Lecturing aside, but armchair journalism has made this guy write such big bluff! Did he attend some journalism class somewhere during his career?
 
Man, this is a piece of crap. How many missions do we have around the world, ina maana hao jamaa wa "chuo Kikuu" wote wanaweza kuwa mabalozi? au kazi huko foreign ni kuwa balozi tu? What the Heck is this Adam thinking, labda alikuwa amechoka hakuna na story ya kuandika, alngekaa kidogo na kuzungusha ubongo wake angeandika makala nzuri sana. This is why Mkapa aliwadharau waandishi wa Tanzania!

He was also once a journalist.... remember!!!
 
Back
Top Bottom