Orodha ya vitabu nilivyosoma 2018



Simulizi za mrengo mmoja.

Vitabu vya Wamarekani tupu havinisaidii kukabili kuzibua mitaro ya maji taka yaliyonizunguka hapa Yombo Kilakala na msongo wa mawazo wa kikokotoo cha mfuko wa kiinua mgongo.
 
Simulizi za mrengo mmoja.

Vitabu vya Wamarekani tupu havinisaidii kukabili kuzibua mitaro ya maji taka yaliyonizunguka hapa Yombo Kilakala na msongo wa mawazo wa kikokotoo cha mfuko wa kiinua mgongo.
Nafikiri hujajua nguvu ya fasihi mkuu,Fasihi ni silaha moja kali sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inategemea akili yako inatafsir vipi maana ya utajiri au mafanikio! Yapo mafanikio ya maarifa n uelewa,yapo mafanikio ya kipato ambayo ndio unaongelea hapa,yapo mafanikio ya Amani ya nafsi nk! Ukipewa nguvu na akili za kutafuta pesa then ukapewa akili ya kutafuta pesa ambayo ni endelevu na bila kutumia nvuvu kubwa hii ni akili ya juu kabisa,Sijawahi fikiria mtu ambaye yupo busy masa Kumi na mbili au zaidi anatafuta pesa,haijulikani hata anaoga saa ngapi,hyo pesa ana spend vipi,ana mwaka wa Kumi hata mazoezi anafanyaga saa ngapi,hajui hata jinsi gani ya kuifanya pesa iwe endelevu pesa ipo Kwa kuwa yupo asipokiwepo na pesa haipo na ndio matajiri wengi wa kariakoo!
Na anaye Linda vitabu mara nyingi huwa anajiliwaza tuu maana hata kushika kitabu kimoja hajawahi,
"Usipo weza kuitafuta pesa ukiwa umelela,utafanya kazi mpaka siku unakufa" Warren Buffet

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona Vichache sana, Inaelekea una michezo sana. Yani mwaka mzima vitabu hata kiganja cha mkono hakijai?! Inabidi uongeze bidii kujisomea.
Hapo nimejitahidi sana, nilipanga nisome kimoja kwa mwezi.
 
Huamini kuwa knowledge inahitajika kwenye kufanya kazi? Na moja ya njia ya kupata knowledge ni kusoma vitabu....
 
Kwa kasumba hizi za kulishwa na wazungu lazima ufe masikini.
Kitakacho kuuwa zaidi ni msongo wa mawazo maana umesoma mavitabu bwalo zima umeambulia kufahamu kingereza tu mfukoni huna hata mia.

Ndio maana maprofesa na ma doctor wengi wa vyuo vikuu vya Afrika ni masikini.
Mwisho wa siku wanakimbilia kwenye siasa.

Wenye muda wa kusoma mavitabu ni watu masikini na wavivu kutafuta shilingi.

Watu wenye mawazo tegemezi. Huwezi fahamu tafuta shilingi afu ushindwe kuilinda labda uwe lofa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona wewe husomi vitabu,unasaka shilingi na bado sio Tu masikini wa mfukoni Bali rofa wa akili na pesa pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona wewe husomi vitabu,unasaka shilingi na bado sio Tu masikini wa mfukoni Bali rofa wa akili na pesa pia

Sent using Jamii Forums mobile app
Lofa na masikini ni mtu kama wewe usiyeamini akili yako ya kuzaliwa.

Unadhani umaskini wako utaondolewa na mtu mwingine ati kwa kusoma makaratasi aliyoandika.

Huu ni ufukara wa hali ya juu kutegemea mawazo ya wamarekani hata kwa vitu vidogovidogo personal.

Mwisho wa haya mnaambiwa muwe mashoga ili mpate utajiri kwa sababu wanaandika hivyo kwenye mavitabu mnayokimbilia kuchota mawazo yao.


Kwani wewe huna maarifa ya kuandika na wewe ukauza kwa hao wazungu?

Kwa mwendo huu kwa nin msiwe mashoga?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huamini kuwa knowledge inahitajika kwenye kufanya kazi? Na moja ya njia ya kupata knowledge ni kusoma vitabu....
Ni kweli. Ila mimi nazungumzia namna watu wengi wanavyovichukulia hivi vitabu. Wanaona kama kusoma ni magic bullet ya kufanikiwa. Kumbe hata baada ya kukisoma bado anakuwa amebakiwa na kazi kubwa zaidi ya ku-apply kile alichokisoma.
 
Knowledge is power mzee, wengine tunasoma kuongeza ujuzi na harakati za kuukacha umaskini tunafanya zaidi so relax hatuezi fanana wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka huu nimesoma hivi vifuatavyo:-
1. Biblia
2. Biblia
3. Biblia
 
Nimefanikiwa kusoma vitabu vifuatavyo kwa mwaka 2018.

1. Soccernomics - Simon Kuper & Stefan Szymanski

2.Tax Compliance in Tanzania ( Analysis of law & policy affecting voluntary Tax payer compliance) - Kibuta Ongwamuhana

3. Tax Dispute Resolution - Kibuta Ongwamuhana

4. The East Africa Tax system - Rup Khadka

5. Tanzania in the Age of Change and Transformation - Ambassador Juma Mwapachu

6. Kichwamaji - Prof. Euphrase Kezilahabi

7. Dunia uwanja wa fujo -Prof. Euphrase Kezilahabi

8. Rose Mistika- Prof. Euphrase Kezilahabi

9. Kaptula la Max - Prof. Euphrase Kezilahabi

10. Gamba la nyoka-Prof. Euphrase Kezilahabi

11. Joka la mdimu- Prof Abdallah Safari

12. Harusi -Prof Abdallah Safari

13. Pepo ya mabwege- Dr Harrison Mwakyembe

14. Kielezo cha fasili- Shaaban Robert

15. Msimu wa vipepeo- K. W. Wamitila

16. Almasi za bandia -C. S. L. Chachage.

17. Mstahiki Meya -Timothy Arege

18. Mtoto wa mama- Adam Shaffi

19. Hofu - E. Musiba
 
Mkuu, bila shaka wewe ni mhasibu, but your choice of reading is very wide!!!



 
Kumbe we Kwa akili yako kusoma kitabu unachukua akili ya mzungu! Alafu kisaikolojia hauko Sawa! Kuna kitu kinakusumbua maana inaonyesha una mengi yanayokusibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu namba 2, 3 & 4 unazo softcopy??
Kama unazo utafanya vyema kuweka hapa jukwaani
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…