Mbogela
JF-Expert Member
- Jan 28, 2008
- 1,384
- 257
Wana JF nimeona uchambuzi umefanyika huko GP.
Nilipoangalia orodha ya hayo maamuzi yaliyowekwa sidhani kama yamewekwa kwa usahihi. Naona kama maamuzi muhimu makubwa yanayolitia hasara taifa hili au kulifanya liwe kama lilivyo hayajasemwa au hajapewa umuhimu na kipaumbele. Kwa vile hapa ndipo jamvi la great thinkers of the time wanakutana nikaona niazime hii hoja na kuileta hapa.
Je unadhani ni nani lini alitoa uamuzi (Utaje) ambao unaweza kusemwa ni uamuzi mbovu (wa hovyo hovyo) ambao uliingiza taifa letu na watu wake matatani wakati huo, au ni uamuzi ambao umetuletea au unatuleta hasara mpaka leo. Je kwenda vita na Idd Amin ulikuwa uamuzi mzuri? Azimio la Arusha? Kuipa TICTs container terminal? Kujenga Uwanja wa Mpira mkubwa wa kisasa? Kutanua njia? Kupiga marufuku mabasi kusafiri usiku? Ebu tufikirie kwa mapana zaidi, ningependa kutoa list ya maamuzi 100 mabaya yaliyowahi kufanywa aidha na kiongozi kama yeye au serikali, Bunge mahakama au chombo chochote cha dola ambayo yameitia nchi hii hasara. Tusaidiane kutengeneza list
Nilipoangalia orodha ya hayo maamuzi yaliyowekwa sidhani kama yamewekwa kwa usahihi. Naona kama maamuzi muhimu makubwa yanayolitia hasara taifa hili au kulifanya liwe kama lilivyo hayajasemwa au hajapewa umuhimu na kipaumbele. Kwa vile hapa ndipo jamvi la great thinkers of the time wanakutana nikaona niazime hii hoja na kuileta hapa.
Je unadhani ni nani lini alitoa uamuzi (Utaje) ambao unaweza kusemwa ni uamuzi mbovu (wa hovyo hovyo) ambao uliingiza taifa letu na watu wake matatani wakati huo, au ni uamuzi ambao umetuletea au unatuleta hasara mpaka leo. Je kwenda vita na Idd Amin ulikuwa uamuzi mzuri? Azimio la Arusha? Kuipa TICTs container terminal? Kujenga Uwanja wa Mpira mkubwa wa kisasa? Kutanua njia? Kupiga marufuku mabasi kusafiri usiku? Ebu tufikirie kwa mapana zaidi, ningependa kutoa list ya maamuzi 100 mabaya yaliyowahi kufanywa aidha na kiongozi kama yeye au serikali, Bunge mahakama au chombo chochote cha dola ambayo yameitia nchi hii hasara. Tusaidiane kutengeneza list