Operesheni ya Magufuli yatikisa Dar

Operesheni ya Magufuli yatikisa Dar

si kweli huyu ni mpenda sifa hafanyi kazi kwa sababu anajua, kinachonishangaza tunamchekea tutaingia nae chooni, Jerry Slaa you are my hero uko wapi please put this insane where he belongs,
ujinga mzigo!
 
anafuata sheria..., hamuonei mtu, sisi wananchi tungekua na utamaduni wa kufuata sheria bila kushurutishwa tungekua mbali sana,,
 
Mi namuunga mkono Magufuli....

Pale Tegeta tunataabika sana!

Masaa mawili foleni kisa watu wanafanyia biashara barabarani. Wakiambiwa wahamie soko la Nyuki hawataki. Bomoa baba! Bomoa!
 
Mi namuunga mkono Magufuli....

Pale Tegeta tunataabika sana!

Masaa mawili foleni kisa watu wanafanyia biashara barabarani. Wakiambiwa wahamie soko la Nyuki hawataki. Bomoa baba! Bomoa!

kaka

siasa ndio inayotuumiza nchi hii,tumeweka sheria kama mapambo tuu,kwani wakati PM anamzuia Magufuri asibomoe alikuwa ana tumia sheria zipi
 
Msimamo wangu katika hili ni kwamba Sheria za nchi lazima zifuatwe. Watu wengine hawafuati sheria na akiambiwa anasema viongozi hawafuati haki za binadamu. Ili tupate maendeleo ni lazima sheria zifuatwe...Magufuli ni mtekelezaji mzuri wa maamuzi ya serikali katika wizara yake. Tumpe ushirikiano na viongozi wengine waige mfano...waache unafiki wa kujifanya wanatetea wanyonge wasio fuata sheria.
 
Mwacheni magufuli afanye kazi zake. Kigamboni tulilalama alipopandisha nauli na wengine wakamdifia na kutubeza ! sasa zamu yenu mwahceni afanye kazi yake ! ili mji upate barabara nzuri tuweze kuwahi makazini ! go go go magufuli
 
NA wewe Ambrose kwa sababu ndugu yako mnatoka maeneo ya huko juu ndio unamtetea! hujambo lakini?
 
kaka

siasa ndio inayotuumiza nchi hii,tumeweka sheria kama mapambo tuu,kwani wakati PM anamzuia Magufuri asibomoe alikuwa ana tumia sheria zipi


Hizi sheria huwa zinafuatwa kipindi kama hiki. Thubutu afanye hivi mwaka 2015. Hata chama chake kitampiga BAN!!!!!!

Tatizo Sheria zimewekwa na wenyewe na kisha wenyewe wanapindisha kwa masilahi binafsi ya either kulinda kura au mshiko wako watendaji wa Serikali waliopewa madaraka.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
si kweli huyu ni mpenda sifa hafanyi kazi kwa sababu anajua, kinachonishangaza tunamchekea tutaingia nae chooni, Jerry Slaa you are my hero uko wapi please put this insane where he belongs,
Kapimwe wewe!!
 
Hizi sheria huwa zinafuatwa kipindi kama hiki. Thubutu afanye hivi mwaka 2015. Hata chama chake kitampiga BAN!!!!!!

Tatizo Sheria zimewekwa na wenyewe na kisha wenyewe wanapindisha kwa masilahi binafsi ya either kulinda kura au mshiko wako watendaji wa Serikali waliopewa madaraka.[/B]


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

MIZAMBWA
Hata mimi inaniuma sana
kufuata sheria kwa kipindi furani tu
 
NA wewe Ambrose kwa sababu ndugu yako mnatoka maeneo ya huko juu ndio unamtetea! hujambo lakini?

Ndugu yangu Magufuli ni kiongozi wa Kitaifa, na anayoyafanya tunafaidika wote...as long as anatekeleza maamuzi halali, tupo pamoja naye. Akighafilika pia tutasema.
 
tatizo la pinda ni nidham ya woga yaan anatoa amri haamini kama itatekelezeka...wakati magufuli anauhakika na anachokiongea akitoa amri inasikilizwa.!!
 
kama tunataka barabara hizi ni lazima tumwache Magufuri afanye kazi yake.

ChinaRoads.jpg

Wewe na mimi na watoto wetu hatutaziona hizo hapa Tz - hata huyo makufuli akiachiwa kuvunja kila kitu. Labda wajukuu wetu.
 
kama tunataka barabara hizi ni lazima tumwache Magufuri afanye kazi yake.

ChinaRoads.jpg


Hii kitu ilitakiwa unaikopi kama ilivyo afu unaipaste pale ubungo mataa weeeeee!ukitoka tauni unanyoosha moja kwa moja kimara-mbezi huyooo, kama unaenda mwenge unavuka unashuka zako kulia hapo huyoooo

Hii kitu inawezekana kabisa! Ni kuacha siasa na kuweka kipaumbele tu !
 
Watanzania wengi hadi Rais wameleta huu usemi kwa wakti tofauti kuwa mlikuwa wapi mpaka mtu/watu wanamaliza kufanya kitendo fulani kibaya kama kujenga sehemu isiyoruhusiwa. Yaani tunataka kugeuza mamlaka zake kama City, Tanroads, etc. kuwa za kupita mitaani kutafuta nani anafanya kosa badala ya kufanya kazi zao husika? Hawa si wavunjaji sheria tu? Mbunge wa Ubungo naye alisema watu wanaofanya biashara barabarani watafutiwe kwanza mahali pakwenda halafu ndiyo watolewe. Kazi ya kuatafuta sehemu kama hizo zipo ndani ya uwezo wake. Amefanya hivyo?

Serikali ni lazima isimamie sheria zake. Rais wa zamani wa Botswana, Festus Mogae aliamuru karibu kijiji kizima kilichojengwa kwa kuvamia ardhi ya serikali kivurugwe. Waliovamia walikuwa ni watu wazito na majengo yaliyojengwa pale yalikuwa ni ya gharama kwelikweli. Tingatinga zilivuruga majengo yote. Wahanga walilalama kuwa wathamasisha asihaguliwe tena kuwa Rais. Aliwajibu kuwa wafanye hivyo tu lakini yeye asingependa kuwa rais wa wavunja sheria. Alichaguliwa kuwa rais tena.
Kumbuka kuwa huyu ndiye aliyepata tuzo la Mo Ibrahim baada ya urais wake.

mkuu last year novemba hapo Kenya kuna wananchi tena wenye fedha makazi yao yalibomolewa baada ya kuvamia eneo la uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta...kimsingi huu ndio utawala wa sheria,kama unaona sheria inakushinda piga mbizi
 
Noamba kujua kwa maeneo ya Kimara na Mbezi hifadhi ya barabara ni umbali gani? najua siyo tena 22.5m
 
Hapa umeongea kweli. kwani huyo anayekwenda kufanya biashara barabarani yeye hajui hiyo ni barabara? Hivi ni mpaka mtu aje akuambie kwamba hii ni barabara huruhusiwi kufanya biashara? Tatizo ni kwamba kila mtu katika nchi hii anataka afanye anachotaka kila mahali na wakati wowote bila kuulizwa na mtu hata akifanya biashara mlangoni kwako ukimwuliza atataka kufanya fujo kwamba unamtendea kinyume na haki za binadamu. Hivi haki za binadamu zinaangalia upande mmoja tu wa shilingi? Viongozi waache kuwa vipofu wa kisiasa wasimamie sheria kila jambo lifanyike kwa utaratibu na sheria zilizopo. Mbona tunafurahia kuona miji ya wenzetu ilkiwa katika mpango mzuri na usafi? Nakusapoti Mpita Njia na nampongeza sana Mh. Magufuli songa mbele hata wasipokupa kura heshima yako italiinua jina lako na kukuweka katika kumbukumbu za wapenda maendeleo katika nchi hii. Mungu akubariki na kukulinda.:lock1:
 
Kwa nini wafanyie biashara barabarani? Licha ya kuvunja sheria pia ajali inaweza kutokea na ikateketeza watu wengi.
 
Hii kitu ilitakiwa unaikopi kama ilivyo afu unaipaste pale ubungo mataa weeeeee!ukitoka tauni unanyoosha moja kwa moja kimara-mbezi huyooo, kama unaenda mwenge unavuka unashuka zako kulia hapo huyoooo

Hii kitu inawezekana kabisa! Ni kuacha siasa na kuweka kipaumbele tu !

mkuu hii kitu inawezekana,tatizo ni kwamba viongozi wetu wa bongo wazuri wa kupanga wabovu ktk utekelezaji,kwa mfano hii barabara sio kwamba ni photoshop kitu kipo China-西安

sielewi ni kwanini kenya wanakimbia sisi hatuoni mifano na wala hatuna tamaa kwa mambo wayafanyayo tena wenzetu wanawatumia haohao wachina kujenga flying over zao

na kama walikuwa hawataki Magufuri asitekeleze kazi zake kwanini walimpa wizara hiyo?
 
Mzee Magufuli Chapa Mwendo!! Mimi na wengine wengi Tuko Nyuma Yako!! Kujenga Jamii yenye Kujali ustaarabu ni Gharama!! Na Unayoyafanya Ndio yenyewe!! Dar Ustaarabu Umepotea Hadi Kero!! Endelea baba Tupo Bega kwa Bega na wewe!!
 
Back
Top Bottom