Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

Hivi sasa naendelea vyema ndugu Ahsanteni kwa maombi yenu

Pole sana mkuu, kuna jamaa yetu mmoja alikuwa anaitwa Ibra(R.I.P) alikuwa anatuletea hadithi ya NITAKUPATA TU, naye aligua kama wewe na baadae akatutoka. Nakuombea kwa Mungu akuponye haraka uweze endelea na shughuli zako pamoja na kutupa burudani. Uwe na jumapili njema
 
Pole sana mkuu, kuna jamaa yetu mmoja alikuwa anaitwa Ibra(R.I.P) alikuwa anatuletea hadithi ya NITAKUPATA TU, naye aligua kama wewe na baadae akatutoka. Nakuombea kwa Mungu akuponye haraka uweze endelea na shughuli zako pamoja na kutupa burudani. Uwe na jumapili njema
Aisee! Umenikumbusha kifo cha Ibra (RIP). Huyu jamaa alikuwa hana longolongo kwenye hadithi. Natamani watunzi wengine wawe kama yeye.

Anyway pole sana mkuu Mwenyezi Mungu akuponye haraka ili uzidi kushusha vitu vitamu kama hivi.
 
Aisee! Umenikumbusha kifo cha Ibra (RIP). Huyu jamaa alikuwa hana longolongo kwenye hadithi. Natamani watunzi wengine wawe kama yeye.

Anyway pole sana mkuu Mwenyezi Mungu akuponye haraka ili uzidi kushusha vitu vitamu kama hivi.
Nashukuni ndugu zanguni hivi sasa naendelea vyema msiwe na shaka mungu ni mwema tu
 
Sehemu ya kumi na mbili


“nakuuliza tena ziko wapi ama uliambiwa nini na Luteni Haji Makame ambae ni rafiki yako?!”safari hii alizungumza huku akivua fulana yake na kuitupa chini

Luteni kanali Mwinyi kisoda hakuwa na cha kujibu na hata angelikuwa nacho bado asingeliweza kutoa jibu.

Kukaa kimya kwa Mwinyi kisoda kukazidi kumpandisha gadhabu Mangazeni nkunda na akaamua kuagiza zana za kazi ambazo zingelimsaidia kumbana Komando yule ili aseme ukweli.

“makomando kama nyinyi huwa tunadawa yenu ya mateso yalioboreshwa na utautapika ukweli”akasema Mangazeni huku akipokea kitorori kidogo kilichokuwa na vifaa mbali mbali na akachagua kitaulo kidogo na kwenda nacho hadi karibu na alipofungwa Luteni kanali Mwinyi kisoda na kisha akamziba nacho usoni na ili kumnyima hewa kisha mtu mwingine akaja na kuanza kumwaga maji juu yake na hivyo kumfanya Luteni Kanali Mwinyi Kisoda atapetape kwa kukosa hewa.

Zoezi lile lilidumu kwa zaidi ya nusu saa kwa kujirudia rudia lakini hakuna alichokisema Mwinyi kisoda kwa kiongozi yule wa waasi.

Mangazeni Nkunda akaamua kubadili mbinu ya kumwadhibu Mwinyi,akachukua waya mfupi wenye unene sawa na mdenge wa tairi ya baiskeli aina ya sport na ulikuwa umewekwa ndani ya moto hivyo kuufanya uwe mwekundu kutazama.

Akautazama kwa madaha kisha akamsogelea Luteni kanali Mwinyi na bila huruma akaudidimiza upande wa kulia wa kifua kipana cha komando Mwinyi kisoda.

Komando Mwinyi kisoda akapiga kelele za uchungu hasa alipohisi waya ule wa moto ukizama na kutoka kifuani kwake na kisha kurudishwa tena na Mangazeni aliposikia kilio cha Mwinyi akazidisha ukatili kwa kuchezesha waya ule uliokuwa umezama kifuani mwa komando Mwinyi ..

Mateso mengi aliokuwa amepatiwa na waasi wale yakamfanya komando azimie hivyo kufanya Mangazeni Nkunda aamuru wapambe wake wampeleke kwenye bwawa la tope.

Bwawa la tope lilikuwa ni bwawa lenye tope zito lililochanganyikana na maji yenye kutoa harufu kali ya uvundo wa mizoga ya watu hasa wale walioteswa na kufia hapo.

Katika bwawa hilo kulikuwa na miti miwili iliokuwa imechimbiwa chini katika pande mbili na kisha kupitisha mti mmoja juu na kufanya kuwe na unganiko katika miti ile.

Mwinyi kisoda aliletwa eneo lile huku kamba zikiwa zimefungwa vyema mikononi mwake na walipomfikisha katika bwawa lile wakamning’iniza kwenye miti ile miwili na kumfanya awe kama anabembea juu ya bwawa lile lenye tope zito.

Kamba imara zilzokuwa zimemfunga zilikuwa zimeshikiliwa na watu wawili wenye ujazo wa nyama mwilini mwao kama mcheza mieleka maarufu wa miguvu bila akili Brown strawman.

Mangazeni Nkunda alifika katika bwawa lile akiwa na bakora iliotengenezwa kwa ngozi ya mnyama Kiboko.

Mangazeni akaamuuru wale washika kamba waachie kamba na walipoachia kamba mwili wa komando Mwinyi Kisoda ambao haukuwa na fahamu ukazama katikati ya tope zito na kumwacha kama dakika tatu hivi kisha wale washika kamba wakavuta kamba kuja juu kwa lengo la kumuibua .

Mwinyi kisoda alipoibuliwa juu tayari alikuwa amepata fahamu na tayari alikutana na mateso mengine tena na bakora kadhaa zilikuwa zimeshapigwa na Mangazeni Nkunda kisha akarudishwa tena kwenye tope lile na hapo akapata tabu mana pumzi hakuipata kabisa na pia alipata adha nyingine ya kugusana miili kadhaa ya watu waliofia ndani ya bwawa lile.

Washika kamba walipompandisha tena,wakazisikia pumzi zake kwa shida,lakini hiyo haikuzuia bosi wao asiendelee kumpiga Komando yule ambae hakuwa amesema lolote hadi wakati huo zaidi ya kulia tu kwa maumivu na adha ya wadudu walikuwa wanaishi ndani ya tope lile.

Wadudu walizidi kumtesa Mwinyi na kumfanya sasa asisikie adha ya bakora alizopigwa zaidi ya wadudu wale ambao walianza kumtoboa mwili wake na pia walitafuta sehemu zenye uwazi na kuanza kujinyonga kuingia ndani ya mwili wake.

Wadudu hawa aliwatambua kwa jina la Migori,wadudu hawa ukibahatika kuwaona mchana wapo kama ngozi ya uume ambao haujafanyiwa tohara,na midomo yao imekaa kama duara,ni wadudu ambao wamekaa bila mfumo wa kuwa na mifupa yani wapo hole na ngozi yao ni ngumu sana hadi utumie ncha kali ndo unaweza kuwaua na waingiapo au wapatapo kidonda kwenye mwili huingia kwa kufyonza damu,midomo yao ni tepetevu lakini inanguvu sana za kutoboa ngozi ya mtu.

Wadudu hawa walikuwa wameanza kwa kuingia sehemu za masikio na na sehemu zenye majeraha ya risasi na michubuko kadhaa,lakini mdudu mmoja akawa anajilazimisha kupita kwenye tundu la uume na hivyo kufanya Mwinyi Kisoda apate maumivu makali na mwili ulianza kuwa kama unamagamba kwa kuwa wadudu hawa migori walikuwa wamemwingia kwa wingi na sifa kuu ya wadudu hawa ni kuwa wanauwezo wa kunywa kiwango kikubwa cha damu mana hawana utumbo na mwili wao unasinyaa na kutanuka.

Mwinyi alijua hatari ya wadudu hawa na hata wale ambao hawajui hata sura yao tazama filamu ya Rambo3.

Wakati Mwinyi akipambana na walau kujitikisa mana alikuwa amefungwa ndivyo alizidi kupata maumivu ya kuongiliwa na wadudu wale na aliumia zaidi sehemu za uume .

Mangazeni alirejea eneo lile baada ya kuwa ametoka kuongea na simu na aliporudi akaamuru atolewe eneo lile na walipomtoa wakatumia maji yenye nguvu kumsafisha na hapo wadudu wale wakatoka huku mana walishindwa kuhimili nguvu ya maji .

Komando Mwinyi akiwa hoi akivalishwa nguo zake kisha wakamfunga pingu miguuni na na mikononi kisha Safari ikawadia na hakujua anapelekwa wapi wakati huo zaidi aliwekewa ulinzi mkali na msafara wa magari matatu,moja mbele na lingine lilikuwa nyuma hivyo kufanya yeye awe katikati ya magari yale.

*****

Jenaral Tasi Kinoga alipokea simu akiwa ofisi kwake na simu hii ilitoka kwa waziri wa ulinzi.

Simu hii haikuwa nzuri kwake, simu hii ilifanya atokwe na jasho licha ya kuwa na kiyoyozi ndani humo.

Alinyanyua simu yake na kumpigia rais .

“Ghost Recon alpha yote imelala chini Mheshimiwa!!”alisema kwa kitetemeshi Jeneral na kwa mbali akazisikia pumzi zikishushwa kwa mkupuo na hiyo ikampa taarifa ya kuwa Rais amechoka kwa taarifa ile.

“Makomando kumi na nne kufa ni hatari na hasara kwa taifa letu Jeneral lakini pia wamekufa katikati ya uwanja wa vita,lakini mateka na ndege havijapatikana”hatimae rais alisema.

“taarifa toka serikali ya Uganda zinasema yaezekena hata mateka wameuwawa usiku wa jana mana tayari vikosi vya waasi vimevuka mpaka na kuingia Burundi.”alisema Jeneral.

Kauli ya Jeneral ikampa kigugumizi rais ambae hakujua aseme nini wakati huo na kubwa hakuwa anaona mwisho mwema katika madaraka yake.

“Hakuna namna lazima tupate ukweli mateka wamekufa au bado wapo mikononi mwa magazeni”akasema rais na kukata simu huku akimwacha Jeneral akitafakari mambo mawili matatu kuhusu taarifa hizo.

Jeneral Tasi Kinoga akaamua kutafuta simu mbili tatu ambazo kiongozi wa waasi alikuwa akizitumia kuwasiliana nao wakati wa mazungumzo,lakini hakupata simu hata moja na jambo hilo likazidi kumuumiza akili na akaona anazidiwa ujanja na waasi tu ambao hawana nguvu ya kushindana na jeshi lake.

Jeneral akapiga tena simu kwa rais

“Nipe ruhusa yako nimtie adabu Mangazeni Nkunda na waasi wote wa LRA”alisema Jeneral

“Ni mapema sana Jeneral kuchukua hatua hiyo na pia najua wajua ya kuwa mpango huu umesukwa kuanzia hapa kwetu,hivyo tunapoamua tumue kisomi zaidi…Nakuomba ofisini Kwangu”alimaliza kwa kuhitaji kuonana na Jeneral kisha akakata simu.

****

Wakati Rais akikutana na Jeneral kwa mara nyingine,huko Zanzibar nako kulikuwa na kikao ambacho hakikuwa rasimi na kikao hiki kiliongozwa na waziri wa mambo ya ndani Zanzibar na kilihusisha watu sita tu akiwamo mzungu mmoja.

“Rais hataki kukubaliana na matakwa yetu na ni kama amesahau mkataba wetu wa 97 na tulitoa watu kama kafara ili mpango wa Zanzibar kujitawala yenyewe utimie lakini naona yeye kabadili gia angani.”alisema Makoye ambae ndie alikuwa mwenyekiti wa kikao kile.

“hakuna makubaliano zaidi ya haya na yale ya mwaka 97,sisi ndio tulimweka pale kwenye kiti,tumepigana ili awe madarakani na lengo aachie Zanzibar ijitenge na iwe ni nchi yenye katiba yake”alisema mjumbe mwingine tena.

“Akikataa kwa maneno inabidi,tufanye mkakati wa machafuko na watu wa waiombe nchi yao,na uzuri mwenyekiti wa SOTE HUB yuko hapa na ndio waliomdhamini Mwenda Mpya na kukataa kwake bila kutii makubaliano inamaana yuko kinyume na mkataba na hatutakuwa na lingine la kufanya zaidi ya kuanza mipango ya kuichukua nchi wenyewe na mpango wa kwanza ndio huu”alisema mjumbe mwingine.

Ulipita ukimya wa dakika kadhaa na kisha bwana makoye akasema

“mkakati wa kwanza umefanywa na ndio huu,tayari tumeirudisha operesheni jicho la paka na hii lazima ijae kwenye bongo za wazanzibar wote na tunaanza kuipanda chuki miongoni mwao kisha miaka kadhaa mbele hakuna mtanganyika atakae kanyaga Zanzibar”.

“Yuko wapi Habibu.B.Anga?”akauliza Mzungu ambae alikuwa kimya muda wote

Mjumbe mmoja akataka kujibu lakini muito wa simu ya Makoye ukamkatisha na bwana makoye akapokea simu ile.

Zilikuwa ni dadika tatu za mazungumzo kati Makoye na mpiga simu ile na kisha Makoye akawapasha wajumbe wa kikao kile dhumuni la mpiga simu.

“Habibu kapiga simu na kasema ubalozini wamempa taarifa ya kuwa kuna mwanajeshi mmoja amekombolewa kutoka kwa waasi wa LRA na taarifa hii amepewa na Mangazeni Mwenyewe”

“mh kama kuna aliebaki inaeza kuwa tatizo”akadakia mjumbe mwingine ambae alikuwa kimya muda mwingi.

“Na aliebaki ni kiongozi wa Gost recon Alpha,na alibakizwa kwa sababu ya kutaka kujua iko wapi nyaraka namba 08 ya mwaka 97 ile ya makubaliano ya kikao chetu cha kuigawa nchi lakini kwa taarifa alionipa Habibu B Anga ni kuwa kuna mtu mwingine tena katokea na kufanya wokozi hivyo kumfanya Luteni kanali Mwinyi Kisoda awe huru hadi tuongeavyo”Alifafanua Makoye na kufanya kikao kizima kiwe kimya bila hata kusikika sauti ya pumzi zao,na ukimya ule ukavunjwa na mzungu.

“kwa kawaida hawawezi kumwamini yeyote zaidi ya ubalozi hivyo wekeni macho huko kisha hakikisheni taarifa haitoki nje ya ubalozi kisha mtunzeni huyo Komando anaeza kuja kutufaa badae”

Alipomaliza kusema wajumbe wote wakapiga makofi huku makoye akinyanyuka na kupiga simu kwa Habibu alieko Uganda na kumpa maelekezo ya nini cha kufanya.

****

Msafara wa magari matatu yaliokuwa yamembeba Luteni kanali Mwinyi Kisoda yalikuwa yanakata kona kuingia mzunguko wa sanamu ya Chief wa baganda,mzunguko huu ulikuwa upo umbali katikati ya mji wa Entebe.

Wakati wanaanza kuikamata barabara ya uzalendo,ndipo dereva wa gari lililokuwa limetangulia alipoona kuna pikipiki inakuja kwa kasi upande wao huku kukiwa na mtu alievalia mavazi ya kijeshi bila kofia ngumu kichwani.

Itaendelea
Riwaya nyingine zipo tayari unaeza wasiliana nami kwa 0758573660 na ukapta riwaya moja mwanzo mwisho na Nyongeza ya riwaya moja kwa bei ya Tsh 3000/=karibuni
 
Niseme tuuu pole na Mungu akufanyie wepesi katika mapitio hayo magumu

Maombi yetu akuponye haraka ili uwe huru kukuza kipaji chako cha kutumia wono na maandiko kutoa burudani
 
Pole sana mkuu, kuna jamaa yetu mmoja alikuwa anaitwa Ibra(R.I.P) alikuwa anatuletea hadithi ya NITAKUPATA TU, naye aligua kama wewe na baadae akatutoka. Nakuombea kwa Mungu akuponye haraka uweze endelea na shughuli zako pamoja na kutupa burudani. Uwe na jumapili njema
Mkuu hapana


Naomba mfano huo usiwe thabiti na Mungu aepushie mbali aaseeee
 
Nashukuni ndugu zanguni hivi sasa naendelea vyema msiwe na shaka mungu ni mwema tu
Tukushukuru tuu kwa kukutia moyo kwa maendeleo mazuri ya afya yako


Mungu akufanyie wepesi mpendwa.

Nisisahau
R.I.P IBRAH

Huyu ni mtanzania miongoni mwa watanzania wachache sana
 
Sehemu ya kumi na tatu

Wakati wanaanza kuikamata barabara ya uzalendo,ndipo dereva wa gari lililokuwa limetangulia alipoona kuna pikipiki inakuja kwa kasi upande wao huku kukiwa na mtu alievalia mavazi ya kijeshi bila kofia ngumu kichwani.

Mtu yule alizidi kikaribia gari lile na alipofikia karibu kwa wepesi wa aina yake akaipisha kidogo ile gari,na niyeye tu aliejua aliekifanya kwenye gari lile na kwa kuwa alikuwa kasi haikuchukua walau sekunde akalipita gari la pili na kwenda kufanya kile alichokifanya kwenye gari la kwanza na kisha akaruka juu na kutua chini kwa mtindo wa aina yake na hakuumia hata kidogo na aliiacha pikipiki yake ikienda kugonga magari mengine yaliokuwa nyuma kisha yeye akaepa na kutua upande wa pili wa barabara na haikupoita hata dakika moja gari la kwanza na la tatu yakalipuka kwa kishindo na dereva wa gari la pili akayumba kukwepesha gari lake na akajikuta anagonga kingo ya barabara na gari likapaa na kuanguka huku tairi zikiwa juu zinazunguka.

Dereva wa pikipiki hakutaka watu ama polisi wamkute pale,haraka akachomoa bastola yake na kukimbia kwa kasi ya na kulifikia gari lile na akaenda upande wa dereva akaachia risasi mbili zikatua kichwani kwa dereva na kumwacha maiti kisha akapita upande wa pili akakutana na mtu akijaribu kutoka ndani ya gari lile nae akamchapa risasi ya mgongo kisha akinama na kuchomoa funguo kutoka kwa mtu yule ambae alimpiga risasi na haraka akapita upande wa nyuma na akapiga risasi moja ilioenda kuvunja kufuli na kufungua mlango,risasi zake tatu zikaenda na uhai wa watu ambao hakuwahitaji na aliwakuta huko nyuma wakiwa wamweka mtu aliemhitaji katikati yao.

Alipohakikisha kaua wote akamsaidia kutoka mtu aliemhitaji kisha akamfungua na pingu za miguu na mikono na alipotaka kumkokota watoke,kagundua mwenzie hana nguvu kabisa,akachomeka bastola yake kiunoni na akamweka begani kisha akakimbia nae kuelekea barabarani na punde ikaja range nyeusi ikasimama na haraka akashuka mwanamke aliekuwa amevaa mavazi ya jeshi la Uganda na akamsaidia kufungua milango na kumwingiza waliemwokoa kisha yule mwanamke akaukamata usukani na kuondoa gari kwa kasi sana huku nyuma wakiacha kelele za magari ya polisi na zimamoto yakifika pale.

****

Unajisikiaje kamanda”aliuliza mtu aliekuwa amekaa karibu na Mwinyi Kisoda.

“Haji nipo hovyo sana,na wamenitesa sana wajinga hawa”alijibu Mwinyi.


Gari walilokuwamo likaenda kuegesha kwenye maegesho ndani ya nyumba ya kawaida iliokuwa imezungushiwa ukuta.

Mwanamke aliekuwa dereva,akawa wa kwanza kushuka na kuja kuwafungulia mlango na akatoka Luteni Haji Makame,na kisha akafuatia Luteni Kanali Mwinyi Kisoda.

Licha ya kuonekana hana nguvu sana,lakini alikataa kusaidiwa kutembea na akatembea mwenyewe kwa tabu na akaingia ndani na yule mwanamke akamwomba aongoze moja kwa moja hadi kwenye chumba kingine ambacho kilikuwa na vifaa tiba na alipofika huko Luteni Haji na yule mwanamke wakaanza kumpa tiba kwenye majeraha mbali mbali mwilini.

“Huyu mwanamke ni nani Haji”aliuliza Mwinyi.

Haji na yule mwanamke wakaangaliana kisha Haji akajibu.

“Afisa wa Jeshi la Uganda anaitwa Cathy ni tabibu kambi ya Enungu,tulikutana miaka kadhaa nyuma huko Sudani”

“ok sawa ndo mana mmeanza kufanana sasa”akatania Mwinyi na kufanya wote waangue kicheko pale ndani.

Baada ya saa tatu kupita tayari Mwinyi Kisoda alianza kurudiwa na nguvu zake na akanyanyuka na kwenda kukaa sebuleni ambako aliwakuta Haji na Cathy wakitizama runinga.

“Vipi kamanda ungelipumzika kwanza…”alisema Haji Makame baada ya kumuona Mwinyi akikaa kwenye sofa.

“mapumziko yanatosha Haji ngoja niungane nanyi hapa mana naona nikilala nitamuota yule mshenzi Nkunda”alijibu huku akitoa sonyo la hasira.

“Yule kafanya kazi yake,tatizo lipo tulikotoka Kamanda na si mimi ama wewe aliegundua hilo”alisema Haji Makame.

“Kwani wewe uliwezaje kutoka kule”aliuliza Mwinyi.

“wakati nikiwa nimeshusha Chopa, nikawa nimetulia nikisubiri amri yako,hapo ndipo nikaamua kutazama kushoto kwangu na nikakutana na mawani moja ikiwa kmesalia mle na nilipoishika nikakutana na chip ndogo na hapo nikajua kuna kitu hakipo sawa nikashuka nayo chini ili niiharibu lakini wakati nafika chini tu nikakutana na watu watatu,sikutaka kuwa mzembe nikapambana na kukimbia,sikufika mbali nikaona chopa ikiwaka moto ndipo nikakutaarifu kisha mikavua bulg na kuzitupa mana sikuziamini tena,na nikaanza kuja uelekeo mliokuwako na nilifika hadi kwenye yale majengo mawili na huko nikafanikiwa kukuona ukifukuzwa na waleywapiganaji,nikataka kukusaidia ila ukawakimbia na ukarudi nilikotoka nami nikarudi na nikafanikiwa kuona ukitekwa nami nikafanya jitihada nikateka mmoja ndie akanambia wanakuleta entebe kwenye nyumba zao,nikachomoka na kuja hadi huku nikampata Cathy na tukafanikiwa kukuokoa”alimaliza kusema Haji Makame.

Luteni Kanali Mwinyi Kisoda akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akasema.

“sasa tunarudije nyumbani mana kuendelea kukaa hapa nikujirudisha tena mikononi mwa LRA ambao naamini hadi sasa wanatutafuta”

“ni kweli na hakuna njia nyingine,lazima twende ubalozi kama raia wema tu kisha tutarudishwa nyumbani na huko tutajua cha kufanya ila mimi sintorudi jeshini tena”alisema Haji Makame huku akimwomba Cathy awapishe wazungumze faragha wao wawili.

Baada ya Kubaki wenyewe Mwinyi akasema

“afu wale wajinga walikuwa wanaulizia nyaraka namba 08 ya 97,sijui wajua lolote”

Haji Makame akakaa kimya kisha akajibu

“wakati nipo kitengo niliwahi kuiona na niliihifadhi mimi chini ya usimamizi wa Kanali Zwange ila nyaraka ile ni janga kama ikiwafikia watu”

“basi inapaswa tutoke hapa Uganda,mwite Cathy atupeleke ubalozi sasa hivi”akasema Mwinyi huku akisimama na kwenda maliwatoni kubadilisha mavazi nae Haji alifanya hivyo.


Dakika kumi baadae walikuwa nje ya uzio wa nyumba ya Cathy wakielekea Kampala huku wote wakiwa kimya kabisa.

***

Bada ya mwendo wa saa mbili na nusu hivi,tayari walikuwa wanaingia Kampala na ndipo Mwinyi akauvunja ukimya.

“Luteni,naona tusiende pamoja wewe baki huku utakuja kwa njia zako,wacha mimi nitangulie,mana kama tulisetiwa nyumbani,hadi sasa wananijua mimi si wewe hivyo baki hapa Uganda”

“Umenena vyema kamanda”kwa mara ya kwanza Cathy aliingilia maongezi yao kisha akaendelea.

“japo sijajua kwa kina ilikuwaje,ila inavyoonekana ni mkondo mkubwa mnauingia hivyo kwenda pamoja ni kama kujimaliza wenyewe”alisema tena.

“hapana shaka we tangulia,mi nafanya niwezalo kesho ama leo hii nitafika Tanzania”alisema Haji Makame.

“ukifika nenda nyumbani kwangu,ukikuta geti limefungwa kwa kufuli jipya ujue nipo na usalama upo ila ukikuta kufuli la kale,jua kabisa sipo na sipo salama,fanya jitihada za kunitafuta”alisema Mwinyi kisoda huku akionekana dhahiri kuingiwa na woga moyoni mwake.

• * *

Gari yao ilisimama hatua kadhaa kutoka kwenye lango la kuingilia ubalozini na Mwinyi Kisoda akashuka kisha lile gari likaondoka kwa kasi kurudi lilikotoka.

Luteni kanali Mwinyi Kisoda akapiga hatua hadi mapokezi,akaeleza shida yake kisha akapelekwa kwenye ofisi ya kushugulikia dharura na huko akakaribishwa na kijana nadhifu,ambae hakuwa mnene wala mwembaba na hakuwa mrefu wala mfupi ila alikuwa na urefu wa kawaida sana na kwa haraka Mwinyi akatupia jicho mezani kwake na akaliona jina Habibu B Anga,kibao kilisoma hivyo.

Habibu akaomba atoke nje na atarudi kumsikiliza alikaa huko nje kwa dakika kama tano kisha akarudi na kuendelea kumsikiliza mgeni wake,kisha akamwambia atamsaidia mana kuna ndege inaenda dar jioni hiyo.

****

Baada ya nusu saa Luteni kanali alikuwa juu ya anga,wakielekea dar es laam kwa ndege ya shirika la Afya duniani.

Tofauti na alivyotegemea ndege ile kutua JNIA,yenyewe ikaenda kutua uwanja wa Karume Zanzibar na kisha wakaja wanajeshi kama kumi hivi wakamweka chini ya ulinzi na kutoka nae na kuelekea asikokujua.

Nb:nunua moja upate moja bure kwa Tsh 3000/= wasiliana nami 0758573660
 
Back
Top Bottom