Wadau Hali zenu:
Napenda kuwazindua kwamba msizuzuke na uwingi wa watu majukwaani. Hii ni kwasababu Watanzania hawana kazi za kufanya, wengi wao hutumia mikusanyiko kama sehemu ya kujifariji na kujichanganya. Sio kama wanaokuja kwenye mikutano ya siasa kwamba ni wapigakura au washabiki wa mgombea fulani, la hasha, kuna kundi kubwa ambalo halina msimamo wowote ule. Akisikia Magufuli atakuja, akija Zitto atakuja, akija Slaa atakuja, na wengineo.
Kama ukitaka kujua, wewe toka nje ya nyumba yako na mke wako anzeni ugomvi fake tu, au wakemee watoto wako live watajaa Wabongo kibao.
Natamani Watanzania tungekuwa na aina ya tafiti ambazo zitatoa tathmini ya watu hawa ambao huenda ni wengi kuliko wanasiasa. Kuna watu Bongo wanapiga kura kimaslahi. Mfano anajua kama CCM itaendelea kuwepo basi baba yake ambaye ni mteuliwa sehemu fulani ataendelea kuleta riziki nyumbani. Hawa watu hawana sera. Pia wapo ambao dili zimeshindikana kwa kuwa CCM wanambania. Hawa hata Magufuli nani aseme nini lazima watapigia against.
So please tunapopiga kampeni, tusisahau or kutosheka kwakuwa watu wanafurika. Mrema alisukumwa mara kadhaa akaishia chaka...
Msijesema sijawatahadharisha!!
Mandokwa me.