Jasusi Mbobezi
Senior Member
- May 17, 2020
- 195
- 851
Kwanza nakupongeza kwa namna unavyojituma kuitumikia nchi kwa moyo wa dhati na nakupa pole kwa matusi unayolipwa na baadhi ya Watanzania. Hata Yesu alijitoa kwaajili ya wanadamu na hawakusita kumsulubisha kwa aibu, ndivyo tulivyo mzee wangu ila we fanya kazi, Mungu atakulipa.
Nirudi kwenye mada, ninapendekeza ikikupendeza, mkuu wa mkoa wa Mtwara pamoja na wakuu wa wilaya watoke kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, sina maana kuwa waliopo hawafai, ila napendekeza ikiwezekana wahamishiwe sehemu nyingine.
Pia, napendekeza mkoa mzima wa Mtwara iwe ni lazima kila anayepokea mgeni kwenda naye kwa mjumbe na kumtambulisha na yeyote atakayekiuka achukuliwe hatua kali za kisheria.
Pia, napendekeza uwachunguze viongozi wote kuanzia ngazi ya serikali za mitaa mpaka juu kabisa mkoani Mtwara, naamini hakuna mgeni anayeweza kuja na kutekeleza uhalifu bila kuongozwa na mwenyeji.
Mwisho nasikitika sana kuona baadhi ya watu hapa JamiiForums wanafurahia vitendo hivi wakishabikia kuwa haviwezi kukomeshwa, nakusihi hata usijibishane nao, Mungu alietusaidia katika kipindi cha CORONA atusaidie katika hili, aviongoze vikosi vya askari wetu kushinda kwa kishindo kama alivyo washindia watu wake katika nyakati zote.
Mungu akubariki sana mzee wangu, watakusaliti wote ila kamwe Mungu hatakusaliti. Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe juu yako, sasa na hata milele Amen.
Nirudi kwenye mada, ninapendekeza ikikupendeza, mkuu wa mkoa wa Mtwara pamoja na wakuu wa wilaya watoke kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, sina maana kuwa waliopo hawafai, ila napendekeza ikiwezekana wahamishiwe sehemu nyingine.
Pia, napendekeza mkoa mzima wa Mtwara iwe ni lazima kila anayepokea mgeni kwenda naye kwa mjumbe na kumtambulisha na yeyote atakayekiuka achukuliwe hatua kali za kisheria.
Pia, napendekeza uwachunguze viongozi wote kuanzia ngazi ya serikali za mitaa mpaka juu kabisa mkoani Mtwara, naamini hakuna mgeni anayeweza kuja na kutekeleza uhalifu bila kuongozwa na mwenyeji.
Mwisho nasikitika sana kuona baadhi ya watu hapa JamiiForums wanafurahia vitendo hivi wakishabikia kuwa haviwezi kukomeshwa, nakusihi hata usijibishane nao, Mungu alietusaidia katika kipindi cha CORONA atusaidie katika hili, aviongoze vikosi vya askari wetu kushinda kwa kishindo kama alivyo washindia watu wake katika nyakati zote.
Mungu akubariki sana mzee wangu, watakusaliti wote ila kamwe Mungu hatakusaliti. Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe juu yako, sasa na hata milele Amen.