Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwa nafasi ya Mwenyekiti Kamati ya Ulinzi na Usalama anaweza akaathirika na kauli ya Mhe. Rais kuhusu mauaji ya Polisi Mtwara?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Taarifa ya kutoonekana kwa mfanyabishara aliyekuja kubainika kuwa ameuawa ilichukua muda mrefu Sana. Ndugu kwa maelezo Yao walifuatilia suala la ndugu yao ngazi tofauti. Zipo kamati mbili ambazo ni muhimu sana kuwa na updates za matukio yanayotokea. Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya Mtwara Mjini ambayo ipo chini ya Mkuu wa Wilaya na Mmoja na Mmoja wa watuhumiwa ambaye ni OCD ni mjumbe Kwenye hiyo kamati. Je kamati DC na wajumbe wake walipata Lini taarifa ya tukio hili? Waliwajibika au walipuuza? Kama awakufanya kazi Yao kamati ya Mhe. Waziri Mkuu itawaacha salama?

Kamati ya pili ni kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa ambayo RPC ni mjumbe na Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti. Je hapa mkuu wa mkoa anawezaje kuchomoka mahojiano? Kama kamati yake haikuwa na taarifa aiwezi kutoa doa ufanisi wa kamati Hii? Je, zipo athari zinazoweza kumpata RC Kwa sakata hili?

Nauliza haya maswali Kwa maana uzoefu wa tume za kijaji Huwa na wigo mpana sana Kwenye uchunguzi. Tungekuwa na Tum ya kijaji maana yake kila aliyepaswa kuchukua hatau angewajibika.

Mwisho, kamati anaweza kuwahoji watuhumiwa ambao tayari wamefikishwa Mahakamani? Ushahidi wa tume una nafasi Gani kisheria Mahakamani au umejikita Kwenye madhaifu ya Watumishi wa Umma pekee?Tukumbuke tume inatumwa wakati timu ya wapelelezi imeshapita Kila Kona na hata askari aliyejinyonga tayari Polisi wameshaconclude Kwamba amejiua na hivyo kwao hakuna Cha Zaidi Cha kufanya.

Je, fedha zilizoporwa Kwa marehemu zimerejeshwa au ndizo zinatumiwa na watuhumiwa kugharamia mawakili wao? Kama zimerejeshwa means watuhumiwa walikiri?

Tuishi ndugu zangu, tuache kutoa nafsi za watu Kwa lengo la fedha au madaraka. Tusifike mahali tukasimama kutetea wauaji maana ipo siku watanogewa na kuamua kuondoa nafsi za watu wa karibu
 
Pascal

Unasema kwamba anatoa tuhuma kwa vyombo nyeti vya usalama,

Je kwako ni mara ya kwanza kusikia tuhuma kama hizi achilia mbali kutoka kwa Lissu?

Au unataka kujifanya haukusikia malalamiko tena makali kutoka ndani ya mhimili mkubwa wa dola (bunge) juu ya utesaji na mauaji yanayo fanywa na hao tiss ? Rejea kauli za wabunge Bashe, Nape, nk ndani ya bunge, Je uliwahi kuwaonya hao wabunge?

Kama wao (vyombo nyeti vya usalama) wamekuwa wakisikia tuhuma hizi kutoka kwa Wananchi mbona hawajawahi kuzitolea ufafanuzi wa maana ili jamii iachane na lawama dhidi yao?
Mkuu Mbogi, kila siku humu if, wanaingia madogo wapya, hivyo hawawezi kujua nani aliwahi kusema nini kuhusu wasiojulikana TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Na ufafanuzi pekee wa kuondoa lawama hizi ni fanya uchunguzi wa kile kinacholalamikiwa ikiwa ni pamoja na mauaji/ majaribio ya mauaji ya watu yaliyotokea.

Wewe Pascal, lisaidie taifa letu kwa kusema ukweli.
Kwenye hili la wasiojulikana, nimejitolea hata kufanya uchunguzi





Mabandiko hayo ni uthibitisho wangu kulisaidia taifa kwenye hii issue ya wasiojulikana.

P
 
Back
Top Bottom