Ombi langu kwa vijana ni kusitisha harakati zote za maandamano.
Maandamano yalishafanyika tena makubwa sana. Ujumbe ulishatumwa. Watawala wameshafahamu kuwa wananchi wameshachoka na uhuni uliokuwa ukifanyika wa mazingaombwe ya kura, ufisadi, uminywaji wa haki, utekaji na mauaji.
Watawala wameshafahamu kuwa kile walichokuwa wakipigania Chadema ndiyo matakwa ya wananchi. Watawala wameshafahamu kuwa huwezi itisha uchaguzi ukaitenga Chadema.
Watawala wameshafahamu kuwa wananchi wanahitaji katiba mpya na bora pamoja na tume huru ya kweli ya uchaguzi.
Watawala wameshafahamu kuwa hawana kibali cha wananchi katika utawala wao hawamu hii na ndiyo maana kete mbaya ya udini inaanza kutumika kugawa watanzania.
Uchumi wa nchi umeshaathirika sana, dola imepotea, mapato yanapungua, watalii hakuna hivyo watawala wapo katika wakati mgumu pia wa kutekeleza yale waliyoyaahidi.
Sasa tuwape muda watekeleze madai ya wananchi badala ya kuendeleza harakati za maandamano, nchi ni yetu na tunapaswa kusonga mbtke kama taifa.
Maandamano yalishafanyika tena makubwa sana. Ujumbe ulishatumwa. Watawala wameshafahamu kuwa wananchi wameshachoka na uhuni uliokuwa ukifanyika wa mazingaombwe ya kura, ufisadi, uminywaji wa haki, utekaji na mauaji.
Watawala wameshafahamu kuwa kile walichokuwa wakipigania Chadema ndiyo matakwa ya wananchi. Watawala wameshafahamu kuwa huwezi itisha uchaguzi ukaitenga Chadema.
Watawala wameshafahamu kuwa wananchi wanahitaji katiba mpya na bora pamoja na tume huru ya kweli ya uchaguzi.
Watawala wameshafahamu kuwa hawana kibali cha wananchi katika utawala wao hawamu hii na ndiyo maana kete mbaya ya udini inaanza kutumika kugawa watanzania.
Uchumi wa nchi umeshaathirika sana, dola imepotea, mapato yanapungua, watalii hakuna hivyo watawala wapo katika wakati mgumu pia wa kutekeleza yale waliyoyaahidi.
Sasa tuwape muda watekeleze madai ya wananchi badala ya kuendeleza harakati za maandamano, nchi ni yetu na tunapaswa kusonga mbtke kama taifa.