Omba omba ya Chadema ni haramu; tulaani utapeli huo!

Omba omba ya Chadema ni haramu; tulaani utapeli huo!

Status
Not open for further replies.

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,830
WanaJF!

Dhana ya kuchangia chama cha siasa kwa kujitolea si vibaya kwa baadhi ya matukio yenye uhitaji wa kuchangiwa kwa hali na mali ikiwemo chaguzi.

Dhana hii imekuwa ikitumiwa kimakosa na viongozi wa CHADEMA kwani wao wameigeuza dhana hii na kuifanya tabia, kwani kila mahali wakikutana na wananchi wao ni kutembeza bakuli tu.

Hali hiyo ya kupitisha maboksi kwa walala hoi na kushawishi kuchangiwa imekuwa ni kama utapeli, kwani ni wazi kuwa CHADEMA ina jitosheleza kimapato ya kuendesha mikutano na ina wadhamini wakubwa tena wafanyabiashara.

Aidha, katika kufanikisha azma yao hiyo ya kutapeli wananchi kwa mwamvuli wa kuchangia mabadiliko, wamebuni mbinu ya kuweka watu wao mbele ili watakapo changia wao kwa wingi iwe chachu ya kuhamasisha na walala hoi nao kuchangia, huu ni usanii wa CHADEMA.

Ikumbukwe kuwa kwa sasa vyama vya siasa vina ruzuku kutoka serikali na kazi mojawapo ya ruzuku kwa vyama vya siasa ni kuwezesha vyama kufanya shughuli za siasa ikiwemo mikutano, sasa kwanini CHADEMA ipitishe kapu kwa walala hoi?

Kwa sasa viongozi wa CHADEMA wapo mikoani kuelimisha wananchi kuhusu suala la katiba mpya, lakini jambo la kusikitisha ni kuona viongozi hao wa CHADEMA wakipitisha maboksi kwa ajili ya kuchangiwa pindi wanapo maliza kutoa elimu hiyo kwa wananchi. Je, hivi ndivyo jinsi elimu kuhusu katiba inavyo tolewa?

USHAURI KWA CHADEMA;

Kwa kutambua kuwa siasa sio uadui, nichukue fursa hii kushauri viongozi wa CHADEMA kuwa wabunifu wa miradi mbalimbali ya chama yenye tija ili kuweza kuingizia chama mapato ya ziada kwa ajili ya chama, badala ya huu utaratibu wa kuwakamua walala hoi unao ongozwa na kamanda Mbowe.

.facebook_-1879148922.jpg Mbowe akipitisha boksi kwa walala hoi kwa ajili ya kuchangiwa hela baada ya mkutano.
 
wanajf!

Dhana ya kuchangia chama cha siasa kwa kujitolea si vibaya kwa baadhi ya matukio yenye uhitaji wa kuchangiwa kwa hali na mali ikiwemo chaguzi.

Dhana hii imekuwa ikitumiwa kimakosa na viongozi wa chadema kwani wao wameigeuza dhana hii na kuifanya tabia, kwani kila mahali wakikutana na wananchi wao ni kutembeza bakuli tu.

Hali hiyo ya kupitisha maboksi kwa walala hoi na kushawishi kuchangiwa imekuwa ni kama utapeli, kwani ni wazi kuwa chadema ina jitosheleza kimapato ya kuendesha mikutano na ina wadhamini wakubwa tena wafanyabiashara.

Aidha, katika kufanikisha azma yao hiyo ya kutapeli wananchi kwa mwamvuli wa kuchangia mabadiliko, wamebuni mbinu ya kuweka watu wao mbele ili watakapo changia wao kwa wingi iwe chachu ya kuhamasisha na walala hoi nao kuchangia, huu ni usanii wa chadema.

Ikumbukwe kuwa kwa sasa vyama vya siasa vina ruzuku kutoka serikali na kazi mojawapo ya ruzuku kwa vyama vya siasa ni kuweza vyama kufanya shughuli za siasa ikiwemo mikutano, sasa kwanini chadema ipitishe kapu kwa walala hoi?

Ushauri kwa chadema;

kwa kutambua kuwa siasa sio uadui, nichukue fursa hii kushauri viongozi wa chadema kuwa wabunifu wa miradi mbalimbali ya chama yenye tija ili kuweza kuingizia chama mapato ya ziada kwa ajili ya chama, badala ya huu utaratibu wa kuwakamua walala hoi unao ongozwa na kamanda mbowe.

wacha unafiki wewe! Waambie ccm warudishe viwanja vyote vya mpira serikalini ili vitumike kwa manufaa ya umma. Waambie ccm warudishe majengo ya serikali yaliyojengwa wakati wa mfumo wa chama kimoja ili yatumike kwa manufaa ya umma. Kuna viwanja vingi vya wazi wanasema vyakwao lakini ukifatilia ni vya umma!!!!!!!!!!!!
 
Kumbuka kwamba ata TANU WALIKUA WANAOMBA MICHANGO YA WANANCHI ILI KUENDELEZA HARAKATI ZA UKOMBOZI, CDM NI KAMA TANU .IMEDHAMILIA KUWAKOMBOA WANANCHI KUTOKA KWA MKOLONI CCM.
 
njaa bana kitu mbaya sana gazeti lenu la uhuru limekishindwanchadema sasa wewe unakesha humu pole sana mpaka 2015 utakuwa unaokota makopa
 
Naomba CHADEMA waitishe kongamano la changizo kwa ajili ya ukombozi wa taifa letu toka kwa mkolono mweusi!.
 
Kumbuka kwamba ata TANU WALIKUA WANAOMBA MICHANGO YA WANANCHI ILI KUENDELEZA HARAKATI ZA UKOMBOZI, CDM NI KAMA TANU .IMEDHAMILIA KUWAKOMBOA WANANCHI KUTOKA KWA MKOLONI CCM.

Kuwa muelewa wewe, kwani TANU ilikuwa ikipewa ruzuku na nani?, kwa sasa CHADEMA inakula milioni 240 kwa mwezi pesa za kitanzania,bado tu wanatembeza maboksi kwa walala hoi?, kwako wewe ni sawa kweli?, mbona kwa wakazi wa Dar huu utapeli hawafanyi?
 

Naona vijana wanakenua meno baada ya kushawishi walala hoi kuchangia, huu ni utapeli wa mchana kweupe. Halafu mlala hoi akitoka hapo kwenye mkutano anaanza kukuna kichwa jinsi ya kupata hela, CHADEMA wawe na huruma kwa watanzania wenye kipato cha chini jamani.
 
Nimesema "tulaani utapeli huo",hivyo hata wewe unaweza kuwa mmoja wa watakao shirikiana nami kulaani huo utapeli wa CHADEMA.
 
Uwe na moyo huo huo DJ wangu Hamy-D, nakukubali sana baba. Big up DJ wangu Hamy-D.
 
wacha unafiki wewe! Waambie ccm warudishe viwanja vyote vya mpira serikalini ili vitumike kwa manufaa ya umma. Waambie ccm warudishe majengo ya serikali yaliyojengwa wakati wa mfumo wa chama kimoja ili yatumike kwa manufaa ya umma. Kuna viwanja vingi vya wazi wanasema vyakwao lakini ukifatilia ni vya umma!!!!!!!!!!!!
Yaani hiyo inauma sana. mimi nakumbuka mzee wangu alivyo changishwa miaka ya 70 fedha ya kujengea uwanja wa SAMORA MACHEL IRINGA halafu leo mtu anajifanya ni wa CCM.uzuri risiti aliyo changia mpaka leo ipo na yeye hajawahi kuwa mwanachama wa TANU/ CCM.SIKU SUALA HILI LIKIPELEKWA MAHAKAMANI MIMI NITAKUWA SHAHIDI NA 1 viwanja vyote vya mpira virudishwe mikononi mwa serikali.
 
Naona vijana wanakenua meno baada ya kushawishi walala hoi kuchangia, huu ni utapeli wa mchana kweupe. Halafu mlala hoi akitoka hapo kwenye mkutano anaanza kukuna kichwa jinsi ya kupata hela, CHADEMA wawe na huruma kwa watanzania wenye kipato cha chini jamani.
Hakuna kitu rahisi kama kuongoza chadema

kuongoza chadema ni kama kuendesha baiskeli tu, huwezi kushindwa.

Wafuasi wa chadema wameisha kuwa brainwashed na ni kazi ngumu sana kurudisha kwenye hali ya kawaida
 
Uwe na moyo huo huo DJ wangu Hamy-D, nakukubali sana baba. Big up DJ wangu Hamy-D.

Mkuu,

DJ ni Mbowe, mimi sikuwahi na sitokuja kufanya shughuli ya DJ, hivyo kuhusu DJ tafadhali mpe Mbowe hiyo status.
 
Nipe Single nyingine DJ wangu Hamy, Hamy, Hamy Hammmyyyy-DDDDD!!!!
Napenda sana unavyofuata nyayo za Mbowe baba, uko vizuri mtu wangu.
Single unazotoa hapa JF unafikiri nini, balaa tupu kaka.
 
Hakuna kitu rahisi kama kuongoza chadema

kuongoza chadema ni kama kuendesha baiskeli tu, huwezi kushindwa.

Wafuasi wa chadema wameisha kuwa brainwashed na ni kazi ngumu sana kurudisha kwenye hali ya kawaida

Mkuu,

Signature yangu ina sadiki maneno yako, kama Mbowe alishindwa kufaulu mitihani ya taifa hata kwa kupata alama D wakati alikuwa kwenye mazingira mazuri ya kusoma, ila Mbowe huyo leo ana akili ya kuiongoza CHADEMA, hii inaonyesha ni jinsi gani ilivyo rahisi kuiongoza CHADEMA.
 
Hamy D LEO UKO PEKE YAKO!! Team lumumba wamelala!!! !! NA KAGERA MSHAPOTEZA! Leo we huwez kulala..
 
Nimesema "tulaani utapeli huo",hivyo hata wewe unaweza kuwa mmoja wa watakao shirikiana nami kulaani huo utapeli wa CHADEMA.
Kila chama kina wafadhili,kuna shida gani kupata ufadhili wa wananchi wa kawaida?Hao wananchi wanachangia ili waweze kuwaondoa nyie magamba madarakani,hayo ni malengo ya chadema na wanayafahamu fika.Unachoongea kwao ni pointless!
 
Hamy-D unahitaji kufanya mrejesho wa harakati zako uone je unafanikiwa kwa style hii? Ni linganifu na muda unaoutumia, nguvu na mali zingine?

Kama ukiona unafanikiwa endelea kutumia mbinu hii hii, ukiona hufanikiwi anza kutumia mbinu ya kutangza sera za chama chako na utekelezaji wa sera hizo.

NOTE: Shetani ukimtaja sana na ubaya wake kila siku kuna watu wataanzakujiuliza kama kweli huyo shetani ni mbaya kiasi hicho anachotajwa, na wakija kujua unawadanganya hawarudi tena! Ila ukitaja ubora na uzuri wa Mungu, watu watauona na kuusadiki, hivyo hawatakuwa na shida ya kutafuta nini kiko kwa shetani kwa sababu wana neema huku wanakokuamini. Na pia ukumbuke kuwa inabidi kuwe na neema ya kweli ndio watu watabaki huko.
 
Dj hamy d mbona single zako huuzi?kesho njoo naya kumtykana dr slaa labda itauza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom