Elections 2010 Omary Kimbau, umeifanyia nini Kijitonyama?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,870
155,827
Barabara mbovu, maji ya shida maisha magumu.
Foleni inaanzia Moroko hadi Mwenge, eneo ambalo kata yake ipo.
Barabara mbadala zipo, haziwekwi lami wala kukwanguliwa.
Zuzumagic huyo tumemchoka na hatumtaki.
Akagombee udiwani hukohuko Masaki kwenye maslahi nako.
 
Kimbau!!
Oh! I know the guy, huwa hakosi kwenye shoo ya FM academia pale katika ukumbi wa kijiji cha Makumbusho.
Na ni kawaida yake kuwatunza(kuwapa pesa) akina Nyoshi El Saadat sauti ya Simba.
 
Ndio taabu ya kuwachagua mapedeshee.
Mwenge Kijijini maji si ya uhakika, kipindi cha mvua ni balaa,
mifereji hamna.
Madampo yanaibuka kila siku, sasa dampo limehamia kwenye Zahanati ya Mwenge.
Ukienda kupata tiba unarudi na mafua huku kifua kikuuma kutokana na harufu kali ya uchafu.
 
Kwani nyie wakazi wa Kijitonyama mlimchagua huyo kimbau kwa vigezo gani hasa?
Majuto mjukuu mnalo, limewaganda.
 
Msimpe kura tena huyu bitozi.
Tafuteni watu makini wenye kuelewa nini maana ya dhamana ya uongozi.
 
Back
Top Bottom