Oktoba tunatiki!!

Oktoba tunatiki!!

Kauli yako imenikumbusha kutiki maneno ya Paulo katika 2 Kor 5:13
Maana ikiwa tumerukwa na akili zetu, ni kwa ajili ya Mungu; au ikiwa tunazo akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.
Unachokiandika inaonekana una tatizo pahala halafu tunakushauri unatuona hatujui kitu, kuna member mwingine alikuja na kujifanya ni Rais wa baadae, simuoni siku hizi hata wewe upweke ndio unakufanya uonekane na tabia ambazo huziangalii kwa namna nyingine 😂
 
Nashauri watu wajitafutie maarifa wao wenyewe binafsi, usisubiri utafutiwe ndio ufuate...dunia ina rangi nyingi, hivyo hakikisha hugeuki kenge...
 
Kuwa makini na kila unachoposti, hasa kuhusianisha Yesu na siasa za hawa wezi na waporaji wa mali za umma na hususani kipindi hiki ambacho kuna fukuto kubwa sana la watu kutaka mabadiliko. Mwombe Roho Mtakatifu akujalie hekima na busara. Lengo linaweza kuwa zuri lakini uwasilishaji wake ndio ukawa na kasoro.
Tatizo lake anatafuta attention zisizo na maana, sifa zimezidi anaharibu sasa
 
Marko 12:17
"...Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu."

Mimi hata kabla ya Oktoba, yaliyo ya Mungu ninayatiki ✅
  1. Yesu Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu ✅
  2. Damu ya Yesu inasafisha dhambi zote ✅
  3. Wokovu haupatikani kwa matendo, bali kwa neema ✅
  4. Biblia ni Neno la Mungu, ni tamu kuliko asali ✅
  5. Msalaba ni msingi wa upatanisho kati yetu na Mungu ✅
  6. Roho Mtakatifu ni Msaidizi na Mwalimu wetu ✅
  7. Kanisa ni mwili wa Kristo duniani ✅
  8. Jina la Yesu lina nguvu ya kufukuza mapepo ✅
  9. Yesu atakuja tena kwa utukufu ✅
  10. Wanaomwamini Yesu wataurithi uzima wa milele ✅

wewe ni mtumishi wa Mungu unayebariki uovu, uliye kinyume na haki. Najiuliza ikiwa unamtumikia huyu Mungu wa haki., Mungu wa mbinguni. Andiko la ya mpeni kaisari halihalalishi udhalimu.
 
Phoenix20250905_091024.png
 
Asante. Umenikumbusha nitiki maneno ya Paulo katika 1 Tim 2:1-4
"Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote; kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu. Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu."
Ubarikiwe mtumishi
 
Back
Top Bottom