KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 3,117
- 5,321
Siku ya Jana tarehe 09.08.2025 ilikuwa ni mwanzo mpya wa mabadiliko makubwa yaliyo mbeleni kwa Taifa baada ya mgombea bora wa urais kwa tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu kuchukua fomu ya uteuzi.
Kilichofanya ubora wa mgombea huyu ni vipaumbele vyake vilivyobeba matarajio makubwa ya wapigakura na tumaini ya Tanzania iliyopo Bora kesho. Vipaumbele vyake ambavyo ni viwanda, kilimo ,ajira na afya vitajenga Tanzania Bora na kukamilisha Ile R ya Rebuilding kwenye falsafa ya 4R.
Kwa nini vipaumbele vya Rais Samia ni msingi wa Tanzania Bora? Tujadili kila kipaumbele:
1.Viwanda
CCM inaamini katika sera ya ujamaa na kujitegemea na katika kujitegemea ni lazima uzalishaji uwepo na hapo ndipo kutakuwa na uhitaji wa viwanda. Kipaumbele hiki kitasaidia kuongeza uzalishaji wa bidhaa, kupunguza mfumuko wa bei, kuimarisha thamani ya shilingi, uhakika wa masoko, uongezakaji wa thamani ya bidhaa zinazotoka nchini. Kwa kipaumbele hiki, Tanzania itakuwa ni moja ya nchi yenye uwezo wa kujiendesha bila mikopo wala misaada ya kigeni na kuingia kwenye moja ya nchi wazalishaji wakubwa.
Ufanikishaji wa kipaumbele hiki ni pamoja na kuwa na miundombinu Bora ya usafirishaji kama SGR, huduma Bora za usafiri wa anga na majini na uboreshaji na uongezekaji wa huduma za bandari.
2. Kilimo
Dkt.Samia hajasahau matumaini ya nchi yetu yapo kwenye kilimo. Kupitia kilimo maisha ya watanzania wengi yataboreshwa na matumaini ya wengi kurejeshwa. Kipaumbele hiki kitawahakikishia watanzania kilimo biashara, kukuza bei za mazao ya kilimo, nchi kuwa na uhakika wa chakula, kupunguza umasikini kwa asilimia kubwa.
3. Ajira
Tatizo la ajira ni bomu linalosubiri kuripuka na hapa Dkt. Samia kaliwahi kabla ya kuripuka. Kwa kuwa Kuna kipaumbele katika viwanda na kilimo basi tatizo la ajira litamalizwa kabisa. Viwanda vitaajiri na kilimo kitaajiri. Tatizo la ajira kwa vijana wa kitanzania litakwisha kwa Samia kupewa nafasi .
4.Afya
Matumaini ya Taifa Bora na imara ni kuwa na watu wenye afya Bora. Kipaumbele hiki kitapunguza kwa asilimia kubwa changamoto zitokananzo na huduma za afya kutofika kwa urahisi.
Vipaumbele vya Rais Samia vimegusa matarajio waliyonayo watanzania na kwa kiwango kikubwa yatapunguza kama si kumaliza kabisa maadui watatu waliosemwa na Baba wa Taifa letu Mwalimu Nyerere ambao ni Umasikini ,ujinga na maradhi.
Kipaumbele Cha viwanda, kilimo na ajira kitaenda kupunguza umasikini , kipaumbele cha afya kitapunguza maradhi na Taifa linaendelea kupambana na ujinga kwa kuendelea kutoa elimu Bora bila malipo, ujenzi wa madarasa na uimarishaji wa kisasa wa ujifunzaji kupitia TEHAMA
ndio maana nasema
OKTOBA TIKI KWA SAMIA KUJENGA TANZANIA ILIYO BORA
Kilichofanya ubora wa mgombea huyu ni vipaumbele vyake vilivyobeba matarajio makubwa ya wapigakura na tumaini ya Tanzania iliyopo Bora kesho. Vipaumbele vyake ambavyo ni viwanda, kilimo ,ajira na afya vitajenga Tanzania Bora na kukamilisha Ile R ya Rebuilding kwenye falsafa ya 4R.
Kwa nini vipaumbele vya Rais Samia ni msingi wa Tanzania Bora? Tujadili kila kipaumbele:
1.Viwanda
CCM inaamini katika sera ya ujamaa na kujitegemea na katika kujitegemea ni lazima uzalishaji uwepo na hapo ndipo kutakuwa na uhitaji wa viwanda. Kipaumbele hiki kitasaidia kuongeza uzalishaji wa bidhaa, kupunguza mfumuko wa bei, kuimarisha thamani ya shilingi, uhakika wa masoko, uongezakaji wa thamani ya bidhaa zinazotoka nchini. Kwa kipaumbele hiki, Tanzania itakuwa ni moja ya nchi yenye uwezo wa kujiendesha bila mikopo wala misaada ya kigeni na kuingia kwenye moja ya nchi wazalishaji wakubwa.
Ufanikishaji wa kipaumbele hiki ni pamoja na kuwa na miundombinu Bora ya usafirishaji kama SGR, huduma Bora za usafiri wa anga na majini na uboreshaji na uongezekaji wa huduma za bandari.
2. Kilimo
Dkt.Samia hajasahau matumaini ya nchi yetu yapo kwenye kilimo. Kupitia kilimo maisha ya watanzania wengi yataboreshwa na matumaini ya wengi kurejeshwa. Kipaumbele hiki kitawahakikishia watanzania kilimo biashara, kukuza bei za mazao ya kilimo, nchi kuwa na uhakika wa chakula, kupunguza umasikini kwa asilimia kubwa.
3. Ajira
Tatizo la ajira ni bomu linalosubiri kuripuka na hapa Dkt. Samia kaliwahi kabla ya kuripuka. Kwa kuwa Kuna kipaumbele katika viwanda na kilimo basi tatizo la ajira litamalizwa kabisa. Viwanda vitaajiri na kilimo kitaajiri. Tatizo la ajira kwa vijana wa kitanzania litakwisha kwa Samia kupewa nafasi .
4.Afya
Matumaini ya Taifa Bora na imara ni kuwa na watu wenye afya Bora. Kipaumbele hiki kitapunguza kwa asilimia kubwa changamoto zitokananzo na huduma za afya kutofika kwa urahisi.
Vipaumbele vya Rais Samia vimegusa matarajio waliyonayo watanzania na kwa kiwango kikubwa yatapunguza kama si kumaliza kabisa maadui watatu waliosemwa na Baba wa Taifa letu Mwalimu Nyerere ambao ni Umasikini ,ujinga na maradhi.
Kipaumbele Cha viwanda, kilimo na ajira kitaenda kupunguza umasikini , kipaumbele cha afya kitapunguza maradhi na Taifa linaendelea kupambana na ujinga kwa kuendelea kutoa elimu Bora bila malipo, ujenzi wa madarasa na uimarishaji wa kisasa wa ujifunzaji kupitia TEHAMA
ndio maana nasema
OKTOBA TIKI KWA SAMIA KUJENGA TANZANIA ILIYO BORA