VoiceOfReason
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,194
- 1,375
Yaani uko ok jamaa abandikwe zigo sio lake hapo kwenye red? I wish mtoto atokee chotara na huyo mume aje kujua yote then amtose tu huyo mke. Alichokifanya huyu mke ni dhambi kubwa sana. Ndio maana tunauana na HIV kijingaaaa, jamaa wa watu maskini anajichunga na vishawishi kumbe work done is equal to zero! Ndio maana ukimwona mgonjwa wa ukimwi usimcheke, anza kujihurumia mwenyewe kabla hujamhurumia. Ndoa za leo yaani hakuna morals kabisa.
Kwa upande wangu,kama kweli huyo mme kampenda mke wake,sioni kosa la kuto kuendelea kumpenda mkewe maana historia kama hiyo nimewai kuiona hapa ulaya (Canada). Mzungu aliyemuowa dada yetu fulani wa ki-Afrika (mweusi) alijikuta anamlea mtoto mweusi wala asiye mfanana babake,huku dada yetu huyo alikuwa akimuakikishia kuwa ni mwanaye du!!!Basi hapo hospitalini damu ilipopimwa,dadetu kajikuta ni uongo mtupu.Na mme huyo akaamua kuendelea na mpenzi wake licha ya uongo huo,mtoto huyo akawa wake tu pasipo shida wala tatizo.Aliendelea kumtimizia kila kitu,alimnunulia gari mpya ,nyumba mpya na kumpa chochote alichokipenda.Hadi leo hii wanaishi pamoja na mtoto yupo na miaka mine imepita sasa;wala hautasikia mzungu huyo anamletea ubaguzi wowote,isipokuwa tu wanapokuwa kwenye sikukuu za sisi wa-Afrika kila mtu hushangazwa na kutaka kufahamu ni nani dada huyo aliyemdanganya mzungu namna hiyo.Tusisahau kwamba hata sisi wanaume (hasa kwa wakati huu) tunafanya mambo makubwa zaidi ya hayo dhidi ya wake zetu ;na , tusidhani kuwa waliogerezani ni wabaya dhidi ya wasiofungwa...
Mwambie achague mume au mtoto wa kizungu. Hiyo tabia madada zetu mmeigeuza kama mchezo wa kawaida, yani umeolewa halafu unaendelea na mechi za mchangani? Ona sasa umevunjika mguu na huna bima!!!!!
Mkuu sikatai kwamba Muhusika amefanya kosa la Jinai; Sikatai kwamba inabidi asisamehewe.., lakini tunaangalia where do we go from here....
Labda Muhusika ana watoto na familia na huyo mume ambae kuondoka kwa mama kutaleta shida, na huyo mtoto ana kosa gani?, kama kweli anaweza kuzaliwa na kulelewa kwa mapenzi ya baba na mama, kwanini isiwe hivyo na apate tabu sababu ya kosa la mama au Just because the Guy is not a biological father
Mkuu Maji yameshamwagika hatuna budi kuzima matundu ili yasimwagike zaidi....
Probably na mimi ningefanya hivyo lakini hapa siongelei mume kumsamehe huyo Dada naongelea Mume kutokujua (yaani hapa ni the better of the two Evils)... Mume kujua na kumfukuza mke hence mtoto anakuwa kama Bastard au Mume kutokujua na kuendelea na mapenzi na mkewe kama zamani hence mtoto kupata malezi ya wazazi wawiliKila mume ana maamuzi yake anayoona yatamfaa kama akikutwa na drama kama hii. Kama ingalikuwa ni mimi ndie mume mhusika basi this marriage is over for I won't be able to live with someone I can't trust. I'll find another woman and start all over.
Hiyo ni element ya Umalaya. Alivyokuwa anajikumbushia kwa huyo chotara Zimbabwe nafsi ilikuwa haimsuti kwamba anamhujumu Mpenzi wake wa Ndoa? Akina dada acheni kutufanyia hivyo, kama unajua mme wako mtarajiwa ana mapungufu kwa nini ukubali kuolewa naye halafu unamsaliti kwenye ndoa? Mtachomwa kwenye jehanamu na mkisikia kiu mtanyweshwa lami inayochemka. Very dissapointing, limtu linakwenda kufanya ngono zembe, hata hali-negotiate kufanya ngono salama kwa kuhofia familia yake, leo limejaa kitoto ambacho si ajabu kinaumwa pamoja na yeye ndo anaomba ushauri. Hakuna ushauri hapa, hayo ndo matokeo ya dhambi na unasubiriwa kwenye hukumu ya milele ambayo ninaamini itakuwa kali sana kwako.
Kila kitu kina gharama. Hii ni gharama ya kutotumia condom. Asubiri matokeo tu hamna namna.Dada huyu ni mtoto wa mama wa kambo wa rafiki yangu niliyesoma nae shule ya msingi;huyu dada yetu ni mfanyakazi wa kampuni moja ya usafirishaji,ameolewa,tatizo ni kuwa ali wahi kuwa na uhusiano na chotara mmoja raia wa Afrika kusini ambae alikuwa nchini na kampuni moja ya ujenzi wa barabara,uhusiano wao ulifikia kikomo baada ya kampuni aliyokuwa anafanyia chotara huyo kumaliza kazi yake,baadae dada yetu akapata mpenzi mwingine na wakaoana,dada yetu akapata safari ya kikazi kwenda Zimbabwe ndipo akakutana na ex wake huko,wakakumbushia na dada yetu akapata ujauzito,lakini aliporudi hakumwambia mumewe,kule Zimbabwe alikaa wiki moja,ujauzito ukawa mkubwa na anakaribia kujifungua,mumewe anajua ni ujauzito wake,dada anaogopa iwapo mtoto atafanana na ex wake rangi na nywele kwani ex wake ana nywele lain kama za kiarabu na ni mweupe sana kutokana na kuchanganya mzungu na mwafrika na inaonekana ana uzungu zaidi,mume wa dada ni mweusi wa kutosha na familia yao haina historia ya weupe,dada kachanganyikiwa,kwani mumewe anampenda sana na alipogundua mkewe ni mjamzito alimnunulia gari mpya na alimtafutia daktari special ili kuhakikisha usalama wa mke wake na mwanae kipenzi!
Is it a real story? It looks unreal... anyyway, huyo dada ajiandae kwa chochote kitakacho tokea.
sometimes or almost always??????????????????Sometimes kina dada tuna dhambi
wapenzi wa zamani ni hatari sana katika mahusiano.
Ni kweli kabisa,kuna usemi uhawara haufagi
Natumaini condom zimbabwe hakuna ndio maana wakatumia kavukavu