Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,708
Dada huyu ni mtoto wa mama wa kambo wa rafiki yangu niliyesoma nae shule ya msingi;huyu dada yetu ni mfanyakazi wa kampuni moja ya usafirishaji,ameolewa,tatizo ni kuwa ali wahi kuwa na uhusiano na chotara mmoja raia wa Afrika kusini ambae alikuwa nchini na kampuni moja ya ujenzi wa barabara,uhusiano wao ulifikia kikomo baada ya kampuni aliyokuwa anafanyia chotara huyo kumaliza kazi yake,baadae dada yetu akapata mpenzi mwingine na wakaoana,dada yetu akapata safari ya kikazi kwenda Zimbabwe ndipo akakutana na ex wake huko,wakakumbushia na dada yetu akapata ujauzito,lakini aliporudi hakumwambia mumewe,kule Zimbabwe alikaa wiki moja,ujauzito ukawa mkubwa na anakaribia kujifungua,mumewe anajua ni ujauzito wake,dada anaogopa iwapo mtoto atafanana na ex wake rangi na nywele kwani ex wake ana nywele lain kama za kiarabu na ni mweupe sana kutokana na kuchanganya mzungu na mwafrika na inaonekana ana uzungu zaidi,mume wa dada ni mweusi wa kutosha na familia yao haina historia ya weupe,dada kachanganyikiwa,kwani mumewe anampenda sana na alipogundua mkewe ni mjamzito alimnunulia gari mpya na alimtafutia daktari special ili kuhakikisha usalama wa mke wake na mwanae kipenzi!