Ogopeni sana watu wanaosema wao hawana upande wowote katika siasa za nchi hii na wakati huo huo wanapiga kura

Kwa mtazamo wangu,licha ya haki yao ya kutokuwa na upande,hili ni kundi la watu "mzigo" maana ni watu wanaokuwa influenced na matukio yanayofanya na wanasiasa pasipokujali dhamira za wanasiasa hao na wanakuwa ni watu wa kuyumbishwa tu na bahati mbaya kura wanapiga kuchagua viongozi.

Watu wa aina hii,mwanasiasa leo akipata tuhuma za kuua, ufidadi au kudhuru, na kesho akajenga barabara,akawapa hela, n.k, wao watakuja hadharani na kumsifia wanasahau kuwa ni lazima mwanasiasa huyu afanye mazuri machache ili apate kuungwa mkono ili kesho tena aweze kudhuru, kuiba, n.k(anang'ata na kupuliza).

Watu wasio na upande ambao leo watamsifia na kesho watamlalamikia, wanashindwa kuelewa kuwa mwanasiasa wa aina hii lengo lake ni kuwa-fool watu ili aweze kupata kundi la watu wa kuumunga mkono, hata kama ni wache, licha ya madhambi ya makusudi anayoyafanya.

Kwa upande mwingine, watu wenye upande mara nyingi huangalia zaidi dhamira ya kiongozi na sio matendo au maamuzi anayoyafanya ambayo wakati mwingine ndani yake yanaweza kuwa yamejaa hadaa fulani ili kupumbaza watu.

Watu wanye upande wao huangali zaidi dhamira ya mtu na wakishagundua ni mtu wa aina gani, basi hufanya maamuzi ya ama kumuunga mkono au kumkataa (kuwa na upande mmoja) na watu wa aina hii ndio wanaweza kufanya maamuzi sahihi katika sanduku la kura tofauti na wale utakaowasikia wakisema mimi niko neutral ambao huyumbishwa na matukio au maamuzi ya wanasiasa pasipo kuwapma dhamira zao na matokeo yake hufanya maamuzi yasiyo sahihi katika kuchagua viongozi.

Kwahiyo, wale wote ambao leo utwasikia wanamlalamikia mwanasiasa fulani na kesho wanamfagilia,mjue tu watu wa aina hiyo teyari ni mateka wa fikra na hawana tofauti na mwanaume alielishwa "limbwata" na kuwa "zezeta" na hawa wanaponza hata wale walioamua kufanya maamuzi ya kumkataa mwanasiasa au kiongozi wa aina hiyo (mwenye tabia ya kung'ata na kupuliza).

Ni kweli binadamu wote tuna mapungufu lakini kufanya au kutenda mambo mabaya kwa makusudi,hii huwa ni dhamira ya mtu ambayo siku zote tunapaswa kuitumia katika kumpina mtu, kiongozi au mwanasiasa yoyote yule.

Kiongozi bora apimwe wa dhamira iliyo nyuma ya maamuzi au matendo yake na kamwe si kwa kutazama matendo au maamuzi anayoyafanya kwani mtapotea na kudanganyika.
Petro E. Mselewa huu uzi unamuhusu.
 
Watu wa aina hii huwa ni mzigo kwa nchi hasa katika sanduku la kura.
Salary Slip kwa kifupi mimi huwa nafuatila sana mada ama komenti zako,aisee wewe ni kichwa,tena kichwa makini sana,naamini familia yako ama famailia unayotoka imepata mtu makini kabisa,mada nyingi namaana zote unazoandikaga huwa ni mada zenye uzito wa hali ya juu sana kama hii .
 
Salary Slip kwa kifupi mimi huwa nafuatila sana mada ama komenti zako,aisee wewe ni kichwa,tena kichwa makini sana,naamini familia yako ama famailia unayotoka imepata mtu makini kabisa,mada nyingi namaana zote unazoandikaga huwa ni mada zenye uzito wa hali ya juu sana kama hii .
Asante mkuu.Pamoja sana!
 
Sina upande wowote wa siasa ukifanya upuuzi nakosoa uwe A au B.

Sijawahi kupiga kura katika maisha yangu na SITAKUJA KUPIGA KURA.
Kweli kabisa...yani hao jamaa wanakomaa na ma-vyama yao ni manyumbu kabisa...yani CCM ifanye ujinga mtu anasifia tu,upande mwingine CHADEMA inafanya ujinga mtu anasifia tu

Sasa huo ni ujinga...na muda mwingi watu kama nyie hamna maslahi ni nchi,mpo na maslahi ya chama zaidi,eti unakuta Rais anakosea kitu,watu flani wako busy kumsifia au mradi mzuri unazinduliwa,watu wako busy kuponda
 
Kwa mtazamo wangu,licha ya haki yao ya kutokuwa na upande,hili ni kundi la watu "mzigo" maana ni watu wanaokuwa influenced na matukio yanayofanya na wanasiasa pasipokujali dhamira za wanasiasa hao na wanakuwa ni watu wa kuyumbishwa tu na bahati mbaya kura wanapiga kuchagua viongozi.

Watu wa aina hii,mwanasiasa leo akipata tuhuma za kuua, ufidadi au kudhuru, na kesho akajenga barabara,akawapa hela, n.k, wao watakuja hadharani na kumsifia wanasahau kuwa ni lazima mwanasiasa huyu afanye mazuri machache ili apate kuungwa mkono ili kesho tena aweze kudhuru, kuiba, n.k(anang'ata na kupuliza).

Watu wasio na upande ambao leo watamsifia na kesho watamlalamikia, wanashindwa kuelewa kuwa mwanasiasa wa aina hii lengo lake ni kuwa-fool watu ili aweze kupata kundi la watu wa kuumunga mkono, hata kama ni wache, licha ya madhambi ya makusudi anayoyafanya.

Kwa upande mwingine, watu wenye upande mara nyingi huangalia zaidi dhamira ya kiongozi na sio matendo au maamuzi anayoyafanya ambayo wakati mwingine ndani yake yanaweza kuwa yamejaa hadaa fulani ili kupumbaza watu.

Watu wanye upande wao huangali zaidi dhamira ya mtu na wakishagundua ni mtu wa aina gani, basi hufanya maamuzi ya ama kumuunga mkono au kumkataa (kuwa na upande mmoja) na watu wa aina hii ndio wanaweza kufanya maamuzi sahihi katika sanduku la kura tofauti na wale utakaowasikia wakisema mimi niko neutral ambao huyumbishwa na matukio au maamuzi ya wanasiasa pasipo kuwapma dhamira zao na matokeo yake hufanya maamuzi yasiyo sahihi katika kuchagua viongozi.

Kwahiyo, wale wote ambao leo utwasikia wanamlalamikia mwanasiasa fulani na kesho wanamfagilia,mjue tu watu wa aina hiyo teyari ni mateka wa fikra na hawana tofauti na mwanaume alielishwa "limbwata" na kuwa "zezeta" na hawa wanaponza hata wale walioamua kufanya maamuzi ya kumkataa mwanasiasa au kiongozi wa aina hiyo (mwenye tabia ya kung'ata na kupuliza).

Ni kweli binadamu wote tuna mapungufu lakini kufanya au kutenda mambo mabaya kwa makusudi,hii huwa ni dhamira ya mtu ambayo siku zote tunapaswa kuitumia katika kumpina mtu, kiongozi au mwanasiasa yoyote yule.

Kiongozi bora apimwe wa dhamira iliyo nyuma ya maamuzi au matendo yake na kamwe si kwa kutazama matendo au maamuzi anayoyafanya kwani mtapotea na kudanganyika.
Ndio sababu akili kama hizi zako Mbowe akifanya madudu wewe nikupiga makofi tu,
Na ccm hata ifanye zuri gani wewe utaponda tu!

Akili zenu ni mfu.
 
Watu hao ni.

Maria Sarungi.
Fatuma Karume
Jebra Kambone
Carol Ndosi
 
Nimeongela wanasiasa zaidi na si vyama nadhani hukunielewa.

Lakini hivi unataka mpaka CCM ifanye jambo gani ndio uje hiki chama hakifai tena kuendelea kuongoza nchi hii?

Hata ukiwa mwanasiasa bora,ndani ya CCM hii unaweza ukafanya jambo gani bila kukwamisha?

Kikwete, licha ya mapungufu yake, issue ya katiba mpya aliiweza ndani ya CCM?


Mpe mfano mwingine wa hivi karibuni huko ndani ya ccm. Katibu mkuu wa sasa alizunguka nchi nzima kuchunguza mali za chama. Akapewa ukatibu mkuu ili atekeleze mapendekezo aliyotoa, akaishia kutoa mkwara kwamba akaingia ofisini wanaomiliki mali za chama wataipata. Saa hii yuko kimya anahubiri ujamaa uliopitwa na wakati.
 
Mpe mfano mwingine wa hivi karibuni huko ndani ya ccm. Katibu mkuu wa sasa alizunguka nchi nzima kuchunguza mali za chama. Akapewa ukatibu mkuu ili atekeleze mapendekezo aliyotoa, akaishia kutoa mkwara kwamba akaingia ofisini wanaomiliki mali za chama wataipata. Saa hii yuko kimya anahubiri ujamaa uliopitwa na wakati.
Wajinga walidanganyika na kitendo cha mtukufu kuunda tume/kamati wakasahau hakuwa na dhamira ya kufanyia kazi mapendekezo ya tume/kamati na huu ndio ugonjwa wa watanzania wengi na unaweza ukawa-fool kwa njia hii na kura wakakupigia /wakakuona unafaa kumbe sio hata kidogo.
 
Bahati mbaya sana kwako mleta mada ni kwamba wapiga kura wengi wa nchi hii si waumini wa vyama kihivyo.
Na bahati mbaya zaidi kwa watanzania ni kwamba vyama havisimamimii sana sera, itikadi au falsafa flani, ndio maana leo unaona chama kilichopinga ufisadi kwa miaka zaidi ya 8 kinawapokea watuhumiwa wao wakubwa na kuachana na sera zao za kupinga ufisadi.

Vivyo hivyo chama kingine kinachotawala wanasema sera yao ni ujamaa lakini kimeendeshwa kwa kibepari tangu 1985 hadi 2015, na sasa hakieleweki hasa nini itikadi yao.

Hawa wanaotung'ang'aniza kwenye vyama wanataka tutetee matumbo yao kimakundi kwa kufuata mkumbo kama nyumbu.
Utachaguaje chama kama vyama vyote havina itikadi na sera zinazoeleweka?
Unataka kusema hata kama chama kikiongozwa na watu ovyo na wakafanya misimamo ya ovyo basi tuwaunge mkono sababu tunatakiwa tuwe na vyama?
Makosa ya kuchagua chama ndio haya yaliyowapa jeuri viongozi wa chama kuweka viongozi wanaonunulika wanao saliti wapiga kura, huku viongozi hao waliokosea kuwapitisha kugombea wakiwa hawana hofu ya kuwajibishwa sababu wanajua watatumia mbinu ya kusema chama kilihamua hivyo wao si wa kulaumiwa na yeyote atakayekosoa maahamuzi hayo anakipinga na kukisaliti chama.

Hapa ndio umeonesha hakuna tofauti kati ya CCM na hao wapinzani ila inategemea nani kashika dola, ni kwamba hata tukiichagua CUF au CHADEMA basi suala la mgombea binafsi tusahau.

Sisi ulio tutukana hapa tunachagua sera safi na kiongozi safi bila kujali chama chake cha ulaji. Aaah, samahani nilikusudia kusema chama chake cha siasa.
 
Sasa niwape majibu ya kwanini kura zimepungua ktk chaguzi ndogo, na CCM wanashinda chaguzi hizo zaidi kuliko vyama vingine ingawa kuna mbinu tata zinzotumiwa na CCM.
Ukweli ni kwamba sisi tusiokuwa na vyama ndio wapiga kura wengi wa chaguzi kuu. Ukija na sera safi na mgombea safi watu watamchagua mgombea wa chama chako.
Sasa kutokana na mambo ya ajabu na ya kukatisha tamaa wanayo tenda watu wenu tuliowapa kura, na matendao yasiyofurahisha ya viongozi wenu wa vyama yamepelekea sisi tusio na vyama kuchukizwa na kukatishwa tamaa na wanasiasa toka vyama vya siasa, na ndio tumehamua kutopiga kura.

Kutokana na ukweli kwamba CCM ina wanachama wengi basi inawalazimisha hao wakapige kura kutetea chama chao hata kama hawaridhiki na mgombea wao au mambo ya chama chao ila wao lazima wakitumikie chama. Kama vile mtoto amteteavyo mzazi wake muovu, mhalifu au pia kinyume chake kwa mzazi amteteavyo mwanawe muovu.

Na kwa hoja hii hii utaona vyama vya upinzani haviwezi kuishinda CCM bila kuwa na wanachama wengi kuliko CCM au kuwashawishi wasiokuwa na vyama kuwapa kura wagombea wao. Sasa wewe badala ya kuwashawishi wasiokuwa na chama kwa lugha nzuri, sera na hoja maridhawa tena kwa busara unakuja kuwavuruga hao watu na kuwatukana, kuwakejeli na mengineyo ya kuwaudhi.

Subiria majibu 2020 kama utaendelea na siasa hizi za kutukana wasiokuwa waumini wa siasa za vyama na ukada.
 
Sasa niwape majibu ya kwanini kura zimepungua ktk chaguzi ndogo, na CCM wanashinda chaguzi hizo zaidi kuliko vyama vingine ingawa kuna mbinu tata zinzotumiwa na CCM.
Ukweli ni kwamba sisi tusiokuwa na vyama ndio wapiga kura wengi wa chaguzi kuu. Ukija na sera safi na mgombea safi watu watamchagua mgombea wa chama chako.
Sasa kutokana na mambo ya ajabu na ya kukatisha tamaa wanayo tenda watu wenu tuliowapa kura, na matendao yasiyofurahisha ya viongozi wenu wa vyama yamepelekea sisi tusio na vyama kuchukizwa na kuktishwa tamaa na wanasiasa toka vyama vya siasa, na ndio tumehamua kutopiga kura.

Kutokana na ukweli kwamba CCM ina wanachama wengi basi inawalazimisha hao wakapige kura kutetea chama chao hata kama hawaridhiki na mgombea wao au mambo ya chama chao ila wao lazima wakitumikie chama. Kama vile mtoto amteteavyo mzazi wake muovu, mhalifu au pia kinyume chake kwa mzazi amteteavyo mwanawe muovu.

Na kwa hoja hii hii utaona vyama vya upinzani haviwezi kushishinda CCM bila kuwa na wanachama wengi kuliko CCM au kuwashawishi wasiokuwa na vyama kuwapa kura wagombea wao. Sasa wewe badala ya kuwashawishi wasiokuwa na chama kwa lugha nzuri, sera na hoja maridhawa tena kwa busara unakuja kuwavuruga hao watu na kuwatukana, kuwakejeli na mengineyo ya kuwaudhi.

Subiria majibu 2020 kama utaendelea na siasa hizi za kutukana wasiokuwa waumini wa siasa za vyama na ukada.
Wewe ni mwana-CCM ila unaeogopa au unaeona aibu kukiri kuwa ni mwana-CCM kutokana na matendo ya CCM hii ya sasa hivyo unabaki kuzungukazunguka tu.
 
Nimeongela wanasiasa zaidi na si vyama nadhani hukunielewa.

Lakini hivi unataka mpaka CCM ifanye jambo gani ndio uje hiki chama hakifai tena kuendelea kuongoza nchi hii?

Hata ukiwa mwanasiasa bora,ndani ya CCM hii unaweza ukafanya jambo gani bila kukwamisha?

Kikwete, licha ya mapungufu yake, issue ya katiba mpya aliiweza ndani ya CCM?
Mimi sijaongelea vyama bali nimeongelea wapigakura ambao si lazima wawe wanasiasa kama post yako inavyosema, waogopwe wanaodai hawana vyama halafu wanakwenda kupiga kura.
 
Kwa sasa ni nadra sana viongozi kuchaguliwa na wapiga kura kwny sanduku la kura.

Wapiga kura wanachagua A, nec inateua B kama alivyofanya jecha
 
Wewe ni mwana-CCM ila unaeogopa au unaeona aibu kukiri kuwa ni mwana-CCM kutokana na matendo ya CCM hii ya sasa hivyo unabaki kuzungukazunguka tu.
Unaweza kusema lolote na kuwaza chochote lakini mimi si mwana CCM na wala hakuna anae nijua huko CCM.
Mwaka 2005 sikupiga kura kabisa niliamini hakuna chama kilicho simamisha mgombea sahihi. Nilivutiwa na CHADEMA lakini sikumkukubali Mbowe hata kidogo.
Mwaka 2010 nilivutiwa sana na CHADEMA na nilikuwa mmojawapo wa waliotia saini petition ya kumuomba Dr. Slaa agombee kupitia CHADEMA.
Mwaka 2015 nilikatishwa tamaa ghafla na ile sarakasi ya mshenga na gia angani upande wa chama nilichokuwa nimevutiwa na wanasiasa wake na itikadi yao (CHADEMA) nikampigia kura Magufuli na namtetea inapostahili hadi sasa ndio maana unadhani mimi ni mwana CCM.
 
Kuna watu tunashindwa kuvumilia ushabiki na kutuweka huko hututakii mema kabisa.

Naona wanasiasa wengi kipaumbele ni maslahi yao na sisi wengine wanataka tusherekee maslahi yao. Wakianza kugusa maslahi yetu au tukiwa ni nguvu ya umma tutahusika. Kwa sasa endeleeni na drama.

Tukihitaji kutafuta pia pesa kwa siasa tutakuwa wote.
 
Unaweza kusema lolote na kuwaza chochote lakini mimi si mwana CCM na wala hakuna anae nijua huko CCM.
Mwaka 2005 sikupiga kura kabisa niliamini hakuna chama kilicho simamisha mgombea sahihi. Nilivutiwa na CHADEMA lakini sikumkukubali Mbowe hata kidogo.
Mwaka 2010 nilivutiwa sana na CHADEMA na nilikuwa mmojawapo wa waliotia saini petition ya kumuomba Dr. Slaa agombee kupitia CHADEMA.
Mwaka 2015 nilikatishwa tamaa ghafla na ile sarakasi ya mshenga na gia angani upande wa chama nilichokuwa nimevutiwa na wanasiasa wake na itikadi yao (CHADEMA) nikampigia kura Magufuli na namtetea inapostahili hadi sasa ndio maana unadhani mimi ni mwana CCM.
CHADEMA walishajua watanzania ni watu wa aina gani na wakaingiza sokoni bidhaa inayokubalika na matokeo yake mliyaona.

Watanzania wangekuwa wanajali sana ufisadi, Kikwete mwaka 2010 asingepata hata asilimia 30 ya kura na watu kama kina Chenge mwaka 2015 wasingerudi Bungeni.

CHADEMA wamehubiri sana ufisadi lakini kila uchaguzi CCM inapata wabunge wengi na hata leo hii tunarudia uchaguzi kwasababu za kipuuzi kabisa ambazo chanzo chake ni CCM lakini bado watu wanawapigia kura wagombea wa CCM waliojiuzulu na kugombea tena.

Tatizo sio CHADEMA bali tatizo ni watanzania wenyewe na ushahidi ni kura alizopata Lowassa ambazo hakuna mgombea wa uraisi kutoka CHADEMA aliewahi kuzipata.

CHADEMA waliangalia watanzania wanapenda bidhaa gani na wao wakaiingiza sokoni na hakika iliuzika tena sana.

Cha muhimu ilikuwa ni kuitoa CCM madarakani kwa kutumia silaha yoyote ile then mambo mengine yangefuata baadae.
 
Back
Top Bottom