Kwanini viongozi wakatili upenda sana kuhubiri kulogwa, kuuawa, kudhurika na kumtaja sana Mungu?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,105
Watu wengi wasiotenda haki ni wepesi sana kuamini katika kulogwa na kudhurika. Upenda sana kuifanya jamii ionekane kama ina kizazi cha watu wakatili na ambao wasingependa wenzao wafanikiwe.

Kwa upande wa pili viongozi hawa upenda sana simpathy na perfection huku walio chini yao wakitakiwa kuwa wajinga na wasio fikiri sawa sawa.

Ni kundi la watu lisilopenda kujiridhisha kwa chochote badala yake kila kinachoingia ndani ya masikio yao ukurupuka na kukifanyia kazi bila kujali kinadhuru wangapi.

Kwao wao familia ni yeye na familia yake na siyo jamii au Taifa. Upenda kuambatana na binadamu ambao uwafanya kama watumwa. Upendelea sana kujikweza na kuambatana na binadamu wakumlinda bila kumtegemea Mungu.

Viongozi hawa ni wepesi sana kuondoa uhai wa mtu kwa kigezo cha maendeleo. Kwao wao maendeleo ni elimination; kwao wao hakuna checks and balance na anayeheshimika japo kinafiki ni yule aliyewazidi cheo.

Kundi la watu wa aina hii limeanza kuongezeka nchini na watawala wamekuwa wakiwatumia kutimiza malengo yao. Mwanasiasa anaamini kuwa na kiongozi asiyeheshimu sheria na katiba ya nchi ni sahihi as long as familia yake na yeye mwenyewe awahesabiki kuwawakosefu katika macho ya binadamu.

Tanzania inaanza kuacha misingi ya utu na kwenda kwenye misingi ya vitu. Viongozi wa sasa kwao watu ni silaha ya kuangamiza wenzao na siyo silaha yakuunganisha watu.

Kinachofanywa kwa ubaya kwa viongozi wa sasa hakitachukuliwa hatua endapo aliyetenda anaweza kuwafikia na wanakunywa nakula naye. Mafisadi Tanzania ndio watoa maamuzi kuhusu siasa na wananchi wanyonge. Magereza yanajazwa maskini huku matajiri wakiishi kwa kuamua wafanye uhalifu gani kwa wakati gani.

Lini utatambua kwamba tunakosa?
 
Je, haikupata kuandikwa waovu hukimbia wasipofuatwa na mtu bali wenye haki ni jasiri kama simba? Tafakari!
 
Ulipaswa kuanzisha hii mada hapo kabla ili likitokea kama lililokufanya kuanzisha mada ionekane kweli ila kwa sababu ya huyu jamaa ndipo umeanzisha naona siyo kweli!.
 
Bashite kwenye sakata la kughushi vyeti alipitia makanisa mengi na kwa Mufti wa Bakwata kutafuta kuombewa.
Hata majambazi kwenye kazi zao ama huomba Mungu au kutegemea uchawi kaa Bashite tuu
 
Ni ngumu kutambua kama tunakosea, sababu magugu na ngano vimeachwa vistawi pamoja.

Unajua hii nchi ina watu washenzi kwelikweli hasa hawa wenye nafasi nzuri.

Kiongozi wa juu kabisa anapaswa kuwa makini kweli.
Utam wa ngoma ni mpaka uicheze

Ukianza kupambana na ukatili usioonekana kwa kufanya ukatili unaoonekana ni wewe ndio utaonekana katili.
 
Umeandika ujinga ujinga tu,

Wee unamwamini Mungu halafu unaogopa kufa? Utaenda vipi sasa huko peponi bila ya kufa?
 
Kundi la watu wa aina hii limeanza kuongezeka nchini na watawala wamekuwa wakiwatumia kutimiza malengo yao. Mwanasiasa anaamini kuwa na kiongozi asiyeheshimu sheria na katiba ya nchi ni sahihi as long as familia yake na yeye mwenyewe awahesabiki kuwawakosefu katika macho ya binadamu.
Kurasa nyingi za Vitabu vya Historia, vya Historia za Wazungu na Waarabu walivyokuja Kuiba, kutufanya watumwa, kutubaka, na kujaribu kubadilisha mifumo yetu ya Kiasili ya Kisiasa, Kijamii, na Kiuchumi, vinaonyesha ni jinsi gani walifanya hivyo kufikia malengo yao, kwa kile walichokiita "Ukombozi" na "Kufundisha" Ustaa.

Walifanya "Ukombozi" huo na "Mafundisho" hayo wakiwa na Fimbo upande mmoja na Biblia upande mmoja, au Jambia upande mmoja na Quran upande mwingine.

Na wote hawa, Waarabu na Wazungu walikuwa wakitumia jina la Mungu.

Mmoja alisema 'In the name of God' huku akikuchapa na mwingine alisema 'Alahu akbaru' huku akikuchinja.


Wanashangaa nini kuona tume staarabika?



Tunashangaa nini na haya yanayofanyika?

Sasa najua wapo wale watasema,

'oh mnawasingizia wazungu na waarabu na hiyo ilikuwa ni miaka hiyo ishapita'

Kwa hiyo tuache kuangalia Historia?

Na hao wanaosema haya mara nyingi, ndio wale wale wanaosema

'oh mnahitaji elimu ya Mzungu au Mwarabu' mbona hamkatai madawa yao, Biblia yao au hela na Quran yao'?

Sasa mnashangaa nini?

Haya Viongozi wamekubali madawa yao, elimu yao, hela yao, na sasa tunaelekea kukubali, kama sio kujitweka, utamaduni wao ambao umeambatanishwa na matendo(maukatili) yao.

Tunalalamika nini?


'He who doesn't know history is doomed to repeat it.'

Tumesahau Historia ya kwetu. Tumesahahu UTU.
 
Back
Top Bottom