Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mali za Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Jimbo la Same zimetolewa nje katika iliyokuwa ofisi ya chama ya jimbo hilo kwa kile kilichoelezwa ni kutokulipwa kwa kodi kwa miezi sita.
Leo Julai 17, 2025 wameonekana mafundi wakipaka rangi na kufuta majina pamoja na rangi za CHADEMA ili ibadilishwa kuwa ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA)
Jambo TV imemtafuta Katibu wa CHADEMA jimbo la Same Magharibi, Mohamedi Mnandi akatueleza kuwa wamekuwa na mazungumzo na CHAUMMA na wakaamua kuwaachia ofisi hizo.
Hata hivyo amesema mwanzo miongoni mwa waliokuwa wanachama wa CHADEMA aliyehamia CHAUMMA alitaka kubadilisha jina la ofisi hiyo kuwa ofisi ya CHAUMMA kwa siri.
“ofisi tumeamua kuwasamehe tumetafuta sehemu nyingine sisi watu wa CHADEMA jana tulikuwa Polisi tumeandikishana polisi kwamba huyu katibu wa zamani tumuachie tunawadai viti 20 watupe viti vyetu tuwaachie” amesema Mnandi
Aidha Jambo TV imemtafuta Mwenyekiti wa CHAUMMA Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni mtia nia wa Ubunge kwa jimbo la Same Magharibi bwana Gervas Mgonja akatueleza kuwa ofisi hiyo alikuwa akiilipia kodi kwa miaka 12 na mwaka huu alipoamua kuhama kutoka CHADEMA aliacha kulipa kodi hiyo.
“mwenye nyumba alisema anataka alipwe kodi nikamwambia Katibu wangu wa jimbo wa CHAUMMA kama ni kulipa nilipe kama ofisi ya CHAUMMA na asaini mkataba wa CHAUMMA”
Mgonja amesema mmiliki wa nyumba ambayo wamepanga ofisi alimfuata akimuuliza kuhusu deni la miezi sita ambalo anadaiwa (kuanzia novemba 2024 mpaka April 2025) huku akimuuliza kama ana mpango wa kuongeza mkataba akakubali mkataba ukaandikwa lakini ofisi ikipangwa kwa matumizi ya CHAUMMA.
“Leo amekuja na mkataba wa CHAUMMA tukawaita vijana wa CHADEMA kuchukua vitu vyao ambavyo ni makaratasi kwa sababu samani(furniture) zote ni mimi niliweka” ameongeza Mgonja
Leo Julai 17, 2025 wameonekana mafundi wakipaka rangi na kufuta majina pamoja na rangi za CHADEMA ili ibadilishwa kuwa ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA)
Jambo TV imemtafuta Katibu wa CHADEMA jimbo la Same Magharibi, Mohamedi Mnandi akatueleza kuwa wamekuwa na mazungumzo na CHAUMMA na wakaamua kuwaachia ofisi hizo.
Hata hivyo amesema mwanzo miongoni mwa waliokuwa wanachama wa CHADEMA aliyehamia CHAUMMA alitaka kubadilisha jina la ofisi hiyo kuwa ofisi ya CHAUMMA kwa siri.
“ofisi tumeamua kuwasamehe tumetafuta sehemu nyingine sisi watu wa CHADEMA jana tulikuwa Polisi tumeandikishana polisi kwamba huyu katibu wa zamani tumuachie tunawadai viti 20 watupe viti vyetu tuwaachie” amesema Mnandi
Aidha Jambo TV imemtafuta Mwenyekiti wa CHAUMMA Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni mtia nia wa Ubunge kwa jimbo la Same Magharibi bwana Gervas Mgonja akatueleza kuwa ofisi hiyo alikuwa akiilipia kodi kwa miaka 12 na mwaka huu alipoamua kuhama kutoka CHADEMA aliacha kulipa kodi hiyo.
“mwenye nyumba alisema anataka alipwe kodi nikamwambia Katibu wangu wa jimbo wa CHAUMMA kama ni kulipa nilipe kama ofisi ya CHAUMMA na asaini mkataba wa CHAUMMA”
Mgonja amesema mmiliki wa nyumba ambayo wamepanga ofisi alimfuata akimuuliza kuhusu deni la miezi sita ambalo anadaiwa (kuanzia novemba 2024 mpaka April 2025) huku akimuuliza kama ana mpango wa kuongeza mkataba akakubali mkataba ukaandikwa lakini ofisi ikipangwa kwa matumizi ya CHAUMMA.
“Leo amekuja na mkataba wa CHAUMMA tukawaita vijana wa CHADEMA kuchukua vitu vyao ambavyo ni makaratasi kwa sababu samani(furniture) zote ni mimi niliweka” ameongeza Mgonja