Ofisi ya CCM yafungwa na kugeuzwa ya CHADEMA:CCM yapoteza Mali na wanachama

Katika tukio ambalo halikutarajiwa na la kushangaza vijana zaidi ya 50 waliokuwa wanachama wa CCM Tawi la Cairo mjini Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara wameishusha bendera ya Tawi hilo na kuipandisha ya CHADEMA huku kila kitu ikiwemo ofisi,samani na wanachama wote kuhamia CHADEMA.

Wanachama hao wamesema wameamua kufanya tukio hilo la kushangaza kutokana na kudai kwamba CCm imepoteza dira na mwelekeo hadi kusababisha maisha kuzidi kuwa magumu na mfumuko wa bei.Pia wamesema wameamua kumuunga mkono aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha James Ole Millya aliyejiondoa CCM na kujiunga na CHADEMA mwezi uliopita.

Akizungumzia tukio hilo kiongozi wa CCM kata hiyo Sifael Saitore mbali ya kushtushwa na tukio hilo aliahidi kutafuta kiwanja sehemu nyingine kwa ajili ya kujenga ofisi mpya ya Tawi kwani awali Tawi hilo lililojiunga na CHADEMA halikuwa katika eneo linalomilikiwa na CCM.

Source:Mwananchi Ijumaa Uk.10

Heeee! Heeeeee! Kibelaaaaaaaa! Nyavu zangu zimecheuaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kama naenda Sokonyi,nakuta ile kaniki amepanda bei! Ameacha ile skolio yangu nyumbani bila kitu ya kufaa! Kake mada ena CCM,! Kanyo doi! Nausa mbusi mbili,lakini mbado haitoshi kununulia ile watoto yangu shakula. Kake,etwaa ena CCM! Engarai duo!

Very interesting Msafiri kwani hawa ccm wameshindwa hata kukidhi hata yale mahitaji madogo madogo ya wananchi. THIS IS OUR RIGHT TIME FOR CHANGE.
 
Haba na haba.................... . Bado magogoni na Lumumba. peoplesssssssssssssssssssssss*3
 
Vijana wameamua kuanza kurudisha mali za wananchi zilizotekwa na CCM. Mbio hazijashika kasi bado, kasi itakapoongezeka zaidi CCM watachanganyikiwa zaidi kuliko inavyotokea sasa kwani wanashikwa na kigugumizi cha kujibu mapigo hayo.

tumeanza kurudisha samani, majengo then viwanja vyote vya michezo vinavyomilikiwa na magamba lzm siku 1 vitarudi mikononi mwa wananchi. wananchi wote walichangia bila kujali itikadi miaka ileee. so navyo lzm virudi.
 
You have a good point. Hawa kama kweli wamekuja kwa kumfuata Milya, sioni kama ni wakushangiliwa sana. Kesho Milya akienda NCCR wanaondoka naye tena? Mrema alikuwa akiimba kuwa na mtaji allioondoka nao NCCR kwenda TLP na hiyo (umimi) ni moja ya sababu zilizommzlliza kisiasa. Tunahitaji mitaji ya chama, si ya baadhi ya wanachama.


Kuchoka akili kuna ji manifest kwa namna hii!!!!!
 
Rebranding ya richard kasesela imekuwa worse kuliko ccm aliyoiacha mzee makamba
 
Tunahitaji kurejeshwa kwa umma viwanja vyote tulivyojenga mikoani na vikamilikiwa na C.I.C.I.E.M
 
Interesting.... isije wakaja kubadili tena kabla ya uchaguzi

CDM inabidi iwastadi hawa watu kwa makini na ku-pre-empty motive yao kama ni hiyo!! Maana kwa magamba lolote linawezekana japo siamini hivyo ukizingatia CCM wanavyopokea matukio haya ya wanachama wao kuhama! Hata hivyo, kinga ni bora kuliko tiba!!!
 
Ulianza upepo, yakafuatia mawimbi, baadae dhoruba ikaja, kutahamaki manyunyu yakashuka. Wakasubiri kupisha hali ya hewa. Wakati huo mvua ikaanza ya masika. Naona sasa hii ni mvua ya mawe iliyochanganyika na dhoruba kali isiyo na maelezo.
 
Safari ya maelfu ya miles huwa inaanza kwa hatua moja moja mpaka ikamilike. Huu si upepo mdogo na wa kuudharau. Kama mtu akizembea kuuzima moto mdogo anaweza kujikuta msitu mzima unateketea. CCM lazima ikubali kuwatumikia wananchi na kuacha kujidanganya eti ni chama tawala. Hakuna chama kinatawala salama bila ridhaa ya wananchi walio wengi....not now maana Dunia imebadilika sana.
ajira ilivyo ngumu mtu ukiomba kazi ya ajira ccm si unaweza kupata siku hiyohiyo;;;;;ukatibu wa wilaya, mkoa,nk si wamekosa ubunifu mi cv yangu imejaa ubunifu,,nataka hai moshi karatu mbulu,nk,,,wanalipa ngapi manake yataka moyo na phd ya uvumilivu,,ninavyo,,,,,,naomba ushauri,,,
 
People's!!!!!!!!!!!!!!!!power............................,ndo kwanzaaaaaaaaaaaa kumekuchaaaaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom