Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,287
- 9,719
Ndugu zangu Watanzania,
Kuna malalamiko na manung'uniko makubwa sana yanaendelea miongoni mwa wanachama wa CHADEMA juu ya michango yao ambayo walichangia chama chao maarufu kama join the chain.mpaka sasa haieleweki ni kiasi gani cha pesa kilikusanywa na kupatikana,kipo wapi,kimefanya nini na kwa utaratibu upi.jambo ambalo limewakatisha sana tamaa na kuwavunja moyo wanachadema.
Lissu akiwa Marekani baada ya kuhojiwa juu ya fedha hizo yeye ameruka kama mwewe aliyenyakua kifaranga kwa kusema kuwa yeye siyo katibu mkuu wala mhasibu wala mtia saini wa fedha ndani ya chama chake.jambo ambalo limeendelea kuzua sintofahamu na mkanganyiko ndani ya chama juu ya fedha hizo,huku wengi wakiwa na hisia kuwa itakuwa zimetafunwa na viongozi wa juu kama ambavyo Ruzuku za chama zimekuwa zikitafunwa kwa miaka mingi sana mpaka kufikia hatua chama kushindwa kujenga hata ofisi zake.
Kwa uchungu mkubwa sana huku wakibubujikwa na machozi wanachama wameeleza kukatishwa Tamaa na uaminifu mdogo ambao umekuwa ukionyeshwa na viongozi wao linapokuja suala la fedha,wengi wamesema kuwa viongozi wao wamekosa uaminifu na wamekuwa wakikitumia chama kama mradi wao binafsi kujineemesha matumbo yao wao binafsi na familia zao ,huku chama kikiendelea kudumaa na kupoteza muelekeo na imani mbele ya watanzania.
Mimi binafsi nawaunga mkono wanachama wa CHADEMA wanaotaka kujuwa pesa zao zipo wapi? Maana hata mimi natambua ya kuwa viongozi wa chadema linapokuja suala la pesa ni watu hatari sana kama fisi mwenye njaa. embu jiulize ndugu yangu yamekwenda wapi na yamefanya kazi gani mamilioni kwa mamilioni ya pesa ambazo chadema ilikuwa ikipokea kama Ruzuku kwa miaka yote? Mbona wameshindwa hata kujenga ofisi? Ukija mikoani unakuta chama hakina hata ofisi tu ya kupanga na pale walipojitajidi kupanga unakuta ofisi zimefungwa na wenye nyumba baada ya kushindwa kulipa kodi.
Ukiwauliza kwanini hamna ofisi? jibu lao utasikia tunajenga kwenye mioyo ya watanzania.sasa huko kwenye mioyo ya watanzania ndiko wanachama wao wataleta kero zao? Ndiko watapatiwa kadi za chama? Ndiko watafanyia vikao vya mikakati ya ushindi? Ndiko wataandaa sera na ajenda? Ndiko watakutana kujadili masuala mbalimbali ya chama chao?
Majibu haya mepesi kwa maswali magumu yalikuwa ni katika kuwapumbaza wanachama wake ambao ilishawachukulia kama nyumbu wasioweza kufikiri sawasawa ili wasihoji juu ya utafunaji wa ruzuku kama mchwa anayehamia eneo fulani.
Nawashauri wanachadema kuendelea kupaza sauti zenu kuwataka viongozi wenu kueleza ziliko fedha zenu.msikubali kuwa kama manyumbu wala makasuku wa kuimba ngonjera zao wakati wao wakijineemesha kwa jasho lenu ,huku ninyi mkiendelea kuhenyeka kwa jasho na machozi kujenga chama Chenu halafu wao watafune tu bila jasho wala uchungu.kataeni ukasuku na unyumbu .amkeni na ikibidi haraka sana jikusanyeni na kuchukua kadi za CCM ili kwa pamoja tuijenge nchi yetu ,maana huku ndiko kuliko na jeshi la wazalendo wa kweli na wenye mapenzi mema na Taifa letu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kuna malalamiko na manung'uniko makubwa sana yanaendelea miongoni mwa wanachama wa CHADEMA juu ya michango yao ambayo walichangia chama chao maarufu kama join the chain.mpaka sasa haieleweki ni kiasi gani cha pesa kilikusanywa na kupatikana,kipo wapi,kimefanya nini na kwa utaratibu upi.jambo ambalo limewakatisha sana tamaa na kuwavunja moyo wanachadema.
Lissu akiwa Marekani baada ya kuhojiwa juu ya fedha hizo yeye ameruka kama mwewe aliyenyakua kifaranga kwa kusema kuwa yeye siyo katibu mkuu wala mhasibu wala mtia saini wa fedha ndani ya chama chake.jambo ambalo limeendelea kuzua sintofahamu na mkanganyiko ndani ya chama juu ya fedha hizo,huku wengi wakiwa na hisia kuwa itakuwa zimetafunwa na viongozi wa juu kama ambavyo Ruzuku za chama zimekuwa zikitafunwa kwa miaka mingi sana mpaka kufikia hatua chama kushindwa kujenga hata ofisi zake.
Kwa uchungu mkubwa sana huku wakibubujikwa na machozi wanachama wameeleza kukatishwa Tamaa na uaminifu mdogo ambao umekuwa ukionyeshwa na viongozi wao linapokuja suala la fedha,wengi wamesema kuwa viongozi wao wamekosa uaminifu na wamekuwa wakikitumia chama kama mradi wao binafsi kujineemesha matumbo yao wao binafsi na familia zao ,huku chama kikiendelea kudumaa na kupoteza muelekeo na imani mbele ya watanzania.
Mimi binafsi nawaunga mkono wanachama wa CHADEMA wanaotaka kujuwa pesa zao zipo wapi? Maana hata mimi natambua ya kuwa viongozi wa chadema linapokuja suala la pesa ni watu hatari sana kama fisi mwenye njaa. embu jiulize ndugu yangu yamekwenda wapi na yamefanya kazi gani mamilioni kwa mamilioni ya pesa ambazo chadema ilikuwa ikipokea kama Ruzuku kwa miaka yote? Mbona wameshindwa hata kujenga ofisi? Ukija mikoani unakuta chama hakina hata ofisi tu ya kupanga na pale walipojitajidi kupanga unakuta ofisi zimefungwa na wenye nyumba baada ya kushindwa kulipa kodi.
Ukiwauliza kwanini hamna ofisi? jibu lao utasikia tunajenga kwenye mioyo ya watanzania.sasa huko kwenye mioyo ya watanzania ndiko wanachama wao wataleta kero zao? Ndiko watapatiwa kadi za chama? Ndiko watafanyia vikao vya mikakati ya ushindi? Ndiko wataandaa sera na ajenda? Ndiko watakutana kujadili masuala mbalimbali ya chama chao?
Majibu haya mepesi kwa maswali magumu yalikuwa ni katika kuwapumbaza wanachama wake ambao ilishawachukulia kama nyumbu wasioweza kufikiri sawasawa ili wasihoji juu ya utafunaji wa ruzuku kama mchwa anayehamia eneo fulani.
Nawashauri wanachadema kuendelea kupaza sauti zenu kuwataka viongozi wenu kueleza ziliko fedha zenu.msikubali kuwa kama manyumbu wala makasuku wa kuimba ngonjera zao wakati wao wakijineemesha kwa jasho lenu ,huku ninyi mkiendelea kuhenyeka kwa jasho na machozi kujenga chama Chenu halafu wao watafune tu bila jasho wala uchungu.kataeni ukasuku na unyumbu .amkeni na ikibidi haraka sana jikusanyeni na kuchukua kadi za CCM ili kwa pamoja tuijenge nchi yetu ,maana huku ndiko kuliko na jeshi la wazalendo wa kweli na wenye mapenzi mema na Taifa letu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.