Katika tukio ambalo halikutarajiwa na la kushangaza vijana zaidi ya 50 waliokuwa wanachama wa CCM Tawi la Cairo mjini Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara wameishusha bendera ya Tawi hilo na kuipandisha ya CHADEMA huku kila kitu ikiwemo ofisi,samani na wanachama wote kuhamia CHADEMA.
Wanachama hao wamesema wameamua kufanya tukio hilo la kushangaza kutokana na kudai kwamba CCm imepoteza dira na mwelekeo hadi kusababisha maisha kuzidi kuwa magumu na mfumuko wa bei.Pia wamesema wameamua kumuunga mkono aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha James Ole Millya aliyejiondoa CCM na kujiunga na CHADEMA mwezi uliopita.
Akizungumzia tukio hilo kiongozi wa CCM kata hiyo Sifael Saitore mbali ya kushtushwa na tukio hilo aliahidi kutafuta kiwanja sehemu nyingine kwa ajili ya kujenga ofisi mpya ya Tawi kwani awali Tawi hilo lililojiunga na CHADEMA halikuwa katika eneo linalomilikiwa na CCM.
Source:Mwananchi Ijumaa Uk.10
Wanachama hao wamesema wameamua kufanya tukio hilo la kushangaza kutokana na kudai kwamba CCm imepoteza dira na mwelekeo hadi kusababisha maisha kuzidi kuwa magumu na mfumuko wa bei.Pia wamesema wameamua kumuunga mkono aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha James Ole Millya aliyejiondoa CCM na kujiunga na CHADEMA mwezi uliopita.
Akizungumzia tukio hilo kiongozi wa CCM kata hiyo Sifael Saitore mbali ya kushtushwa na tukio hilo aliahidi kutafuta kiwanja sehemu nyingine kwa ajili ya kujenga ofisi mpya ya Tawi kwani awali Tawi hilo lililojiunga na CHADEMA halikuwa katika eneo linalomilikiwa na CCM.
Source:Mwananchi Ijumaa Uk.10