screpa
JF-Expert Member
- Sep 10, 2015
- 10,792
- 15,693
Hivi Lavalava bado hawajaamua kumsapoti? Maana hata kibongobongo hajatoboaKuna vitu ambavyo wabongo lazima tubadilike na hii mitazamo ya utimu na kutafakari kwa bashasha kidogo...
Aslay angeenda wasafi ndo ingekuwa mahali pekee kwayeye kukua kimziki....dogo ana kipaji cha kipekee...lakini kuwa na kipaji tu haitoshi...unahitaji back up kubwa sana illi uweze kutoboa...
Kwani wangapi wana kipaji kama Aslay na wana miaka kibao kwenye gemu lakini bado wanasota tuu??
Halafu wangapi hawana hata vipaji (tena Aslay amewapita mbali sana kwa kipaji) lakini kwakuwa wapo WCB wao ndo wana mafanikio makubwa sana Bongo na hata Afrika wanasikika sikika??
Kubali,kataa,bisha,andamana, WCb ndo sehemu pekee kwasasa hapa bongo ambapo hata mimi nisiejua kuimba chochote na nikaenda pale basi wakiamua kunisupport lazima nitaonekana tu na nitatoboa kibongobongo.