mooduke
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 628
- 111
Kwa Mishahara midogo na kazi katika mazingira magumu wakati mwingine mazingira hatarishi nafikiri ingewa motivate sana Walimu Madaktari na Ma-Nurse kama serikali ingeweka sheria kuwa hizi nyumba za shirika la Nyumba hapa mjini kati ambazo kodi yake ni nafuu ni vema tungewapendelea watumishi wa serikali wa kada hizo nilizozitaja kulikoni kuwaachia wafanyabiashara wa kiasia ambao kwanza wanakipato kikubwa na wana uwezo wa kukaa sehemu yeyote bila kuathirika kimaisha kutokana na sehemu kubwa ya kipato chao kutumika kwa usafiri na gharama zingine zitokanazo na kuishi mbali na sehemu zao zakazi. Vilevile hii ingewafanya watu kamawalimu kuona ni kwa kiasi gani tunawathamini.
Hili ni wazo wazo waungwana mnaonaje...?
Hili ni wazo wazo waungwana mnaonaje...?