Nyumba za Kigamboni zinauzwa kwa kasi ya 5G, tupeane tahadhari

LICHADI

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
4,340
11,881
Kipindi cha hivi karibuni kumeibuka wauzaji wa nyumba huko Kigamboni kwa kasi kubwa na nyumba zinazouzwa ni nyingi sana na zina quality kwa bei rahisi.

Wajuzi wa mambo tutahadharishane hapa kama kule kuna shida ndiyo maana watu wanauza au kama hali ni shwari tuambizane pia ili wanunuzi wasiingie kichwakichwa.
 
Kuna jambo limejificha kwenye hizo nyumba, moja...

Wamiliki wake wanafanya biashara ya nyumba.

Pili, Nyumba zinaonekana nzuri kwa macho ila sicho macho inachoona.

Tatu, fuatilia aina ya ujenzi wa hizo nyumba zoote zina aina flani ya finishing ndipo zinauzwa.

Mwisho, chunguza urefu wa choo ukikuta 12feet, msingi imara na urefu wake kwenda chini.
 
Jenga Uza hizo, hakuna cha watumishi kuhamia dodoma wala nini, hazina ubora ukipiga ngumi ukuta unatoka ufa, kanunue uone muziki wake
 
Back
Top Bottom