Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,366
kama tulipata theluthi mbili kwenye bunge la katiba kwa nini nyumba hii isiwe na thamani hiyo?Wakuu,
Miradi ya Ujenzi katika Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, imeghubikwa na tuhuma za ufisadi, ambapo hivi karibuni imekabidhiwa nyumba ya Mwalimu yenye Vyumba viwili vya kulala na sebule, ikitajwa kugharimu sh. milioni 89, jambo ambalo limeibua utata na kumlazimu Mkuu wa Wilaya hiyo, Elibariki Kingu kuingilia kati.
Gharama ya ujenzi wa nyumba hiyo katika Shule ya Sekondari Ichana Kata ya Chabutwa ni sehemu ya Matumizi ya Milioni 219 zilizotolewa na Serikali kuu kupitia mpango wa maendeleo ya Elimu ya Sekondari[MMES] kwa ufadhili wa bank ya Dunia.
Wakuu naomba tujadili haya matumizi. Nimejaribu kuweka picha kutoka Gazeti la Tanzania daima la Leo.
![]()
Mia