Nyumba ya mil. 89/- yamtatiza DC

Nyumba ya mil. 89/- yamtatiza DC

Nyie bavicha tabu sana, yaani huto tuvisenti tu...serikali sikivu ya ccm inaboresha maisha ya waalimu kwa kutumia vijisenti vidogo tu hivyo nyie keleleeeeeeee, hiyo nyumba gharama halisi ni 150ml. hapo tumebana matumizi matumizi sanaaa ndiyo zikafikia 86ml. bavicha acheni wivu wa kike...hii ndiyo serikali ya ccm, maisha bora kwa kila mdanganyika.
 
labda ndani wameweka vito vya thamani ya pesa kubwa!, si wana mpango wa kuweka mazingira mazuri ili walimu wasikimbie kwenye vituo vya kazi zao?

Sure! Ndani imenakshiwa kwa dhahabu safi na vyooni kumepambwa kwa ruby aghali. Marumaru za chini zimetokana na mawe aghali ya kule Italy kama zile zilizopamba Hekalu la Suleman hapo kale; hata chombo cha kutupia condom kimetengenezwa kwa silver safi. Mbao zake ni mwerezi aghali wa Lebanon.
 
labda ndani wameweka vito vya thamani ya pesa kubwa!, si wana mpango wa kuweka mazingira mazuri ili walimu wasikimbie kwenye vituo vya kazi zao?

Ndani kuna AC 12, Thamani za ndani zote zimenakishiwa kwa madini ya Alumas na Dhahabu,chezea wajanja weweee.....
 
Hill mall litapita kama mengine
Binadamu wa mvivu zaidi kufikiri huenda alizaliwa Tanzania_Edo kumwembe
 
Ndani ya serikali ya CCM yote hayo yanawezekana...

Hapana Mkuu, yote hayawezekani kumbuka maisha Bora kwa kila Mtanzania yameshindikana, yapo mengi tu yameshindikana hasa ya jamii mfano kupiga marufuku Uvaaji wa hovyo hovyo (mlegezo) watu kuvaa suruali chini ya makalio wadada kuvaa vinguo vya ajabu, kwenye Maadili wamefeli, isipokuwa kwenye Uchakachuaji hawana Mpinzani Duniani.
 
mambo hayo yataleta utata tu,ikiwa waliopanga kupewa baadhi ya hizo pesa hawakupata
 
Ni upepo tu utapita ka ile nyumba ya gavana ya mabilioni ya pesa.
Watanzania ni wasahaulifu sana.
 

Acha nao wapige,kila siku wanasoma habari za ESCROW,EPA,etc na hawaoni chochote cha maana kilichofanywa zaidi ya blah blah.

Tulipofikia wewe ukipata fursa,piga kisawasawa ndo siri ya mchezo.
 
Swali ni baada ya DC kutatizika alichukua hatua gani? au ndo alitatizika mgao haukumfikia? viongozi wetu nao mzigo tu
 
Mapishi ya namna hiyo yanaanzia bungeni/serikalini. Bajeti inapitishwa kwa rushwa....Kura za kupata theluthi mbili zinachakachuliwa mchana kweupee na watz wanaona na wako kimya....TUNAYALEA SANA HAYA MACCM NA YATATUNYONYA MPAKA TUISHIWE DAMU
 
ule uzalendo uliokuwepo awali sasa hakuna tena! kila m2 mwizi, hakuna wa kumkemea mwenzake! nina hakika hawa maccm hata ukiwapa mia 2 ukawaambie wanunue wembe wataiba tu! ni kwamba "mind" yao imeathirika vbaya sana na wizi, yaani hawa wamekuwa "mateja" wa kuiba. tusishangae cku 2kaambiwa mkuu wa mkoa kamuibia mkuu wa wilaya leso yake walikuwa kikaoni...!
 
Mnalalamika nini?teketezeni kitu kama hicho!ni heri kisiwepo maana napata hasira......
 
Bila watu hawa kupigwa risali za kichwa ama kuvunjwa miguu hatutakaa tuione nafuu!
 
Chanzo ni Tanzania daima.Nyumba ya millioni 89 mlitaka iwe ya ghorofa?
 
Wakuu,
Miradi ya Ujenzi katika Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, imeghubikwa na tuhuma za ufisadi, ambapo hivi karibuni imekabidhiwa nyumba ya Mwalimu yenye Vyumba viwili vya kulala na sebule, ikitajwa kugharimu sh. milioni 89, jambo ambalo limeibua utata na kumlazimu Mkuu wa Wilaya hiyo, Elibariki Kingu kuingilia kati.

Gharama ya ujenzi wa nyumba hiyo katika Shule ya Sekondari Ichana Kata ya Chabutwa ni sehemu ya Matumizi ya Milioni 219 zilizotolewa na Serikali kuu kupitia mpango wa maendeleo ya Elimu ya Sekondari[MMES] kwa ufadhili wa bank ya Dunia.

Wakuu naomba tujadili haya matumizi. Nimejaribu kuweka picha kutoka Gazeti la Tanzania daima la Leo.
attachment.php

Mia

Kuna maswali mengi ya kuulizwa juu ya hili:-
1. Mkandarasi aliyejenga ni nani?
2. Nyumba iliyotakiwa kujengwa ilikuwa iwe ya aina gani? ni vema Ramani ikaonyeshwa
3. Je ujenzi huo ulipewa baraka na kamati ya fedha ya halmashauri(Finance)?
4. Wakati wa ziara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayofanywa na madiwani (CCM) hawakugundua kuwa ujenzi huo hauendani na gharama halisi zilizopitishwa katika vikao vyao?
5. Ni nani aliyeidhinisha malipo hayo huku akijua hayaringani na uhalisia wa kilichojengwa?
6. BOQ ya ujenzi huo inasemaje?
7. Je upatikanaji wa mzabuni huyo ulifuata taratibu zote?
 
Back
Top Bottom